#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

SAFARI ALIZOWAHI KUFANYA MHUSIKA AKIPANGIWA NA BOSSX

……………inaendelea


……” alikutana na watu watatu, staff-mates… Wawili walikuwa wanabadilisha ndege kwenda nchi nyingine na mwingine wa tatu alikuwa anasubiria ndege ya kurudi Tanzania.”

SAFARI YA PILI, NJE YA NCHI, NDANI YA AFRIKA


Safari hii lifanyika Desemba 2009, nje ya nchi, ndani ya Afrika, nchi jirani
  • Safari hii hakuifanya peke yake, walikuwa pamoja na Boss X
  • Ilikuwa ni kwa ajili ya kuchakata data za matetemeko ya Ardhi
  • Mkutano huu ulikuwa sawa kabisa na ule uliowahi kufanyika May 2007 ambao mhusika alisafiri peke yake nje ya nchi
  • Kwenye safari hii vile vile, wakiwa wapo airport siku ya kurudi baada ya mkutano huo kuwa umeisha,
  • ………………..walikutana na watu watatu, wawili staff-mates…na mmoja SENIOR RETIRED STAFF-MATE, ambao nao pia walikuwa wamekuja kikazi kwenye jiji hilo ambalo mhusika na Boss X walikuwa wamekwenda. Watu hawa nao pia walikuwa anasubiria ndege ya kurudi Tanzania.”
  • RETIRED SENIOR STAFF-MATE huyu alikuwa ni yule ambaye baada ya yeye kuwa amestaafu mnamo Desemba 2006, nafasi yake ilIchukuliwa na SENIOR MSTAAFU WA KIUME
  • Mwingine kwa wakati huo alikuwa ni Mkuu wa MAJOR UNIT aliyokuwa anafanyia kazi mhusika
  • Wa tatu alikuwa anatoka kwenye kitengo kimoja na mtu ambaye hivi karibuni, alikutana na mhusika mtaani akiwa na gari lenye namba zenye herufi BJV
  • Kipindi wakati mhusika akiwa yuko ndani ya jiji hilo wakiendelea na mkutano wao, hakuwahi kukutana na watu hawa, na wala alikuwa hana taarifa za uwepo wa watu ndani ya jiji hilo
  • Kwa hiyo alikutana na watu hawa jioni hiyo wakiwa wanasubiria ndege ya usiku ya kurudi Tanzania
Kabla mwandishi wenu hajaendelea zaidi na amelezo ya safari hii ya nje ya nchi……………

SAFARI YA MWISHO YA MHUSIKA


Hii aliifanya May 2012
Akiwa yupo Dodoma amepanda kwenye gari la kuja Dar es Salaam, kwa mara nyingine tena.....……” alikutana na watu watatu, staff-mates…

Watu hawa walimkuta mhusika akiwa tayari ameshapanda kwenye gari la kuja Dar es Salaam

Usiku uliokuwa umepita mhusika alilala Kiteto, na asubuhi yake ndiyo akawa amepanda gari kuja Dodoma, tayari kwa safari ya kurejea Dar es Salaam

Baadhi ya maelezo ya safari hii alishawahi kuyaleta humu jukwaani kupitia post hii hapa #504
  • Kati ya staff-mates hawa watatu ambao mhusika alikutana nao kwenye safari hiyo, mmoja wao walikuwa wanafahamiana na wanaongea lugha moja, mwingine wa pili alikuwa anamfahamu kwa sura tu na wa tatu alikuwa ni mgeni kabisa machoni kwa mhusika
  • Yule wanayefahamiana ndiyo alimtambulisha mhusika kuwa hata yule wa tatu naye pia alikuwa ni staff-mate
  • IWakati wanapata nafasi ya kutambulishana hivi, ilikuwa ni kipindi walipokuwa wanasubiria gai ikiwa inaendelea na matengenezo pale Dakawa
Gari hilo liliondoka Dodoma saa 5 asubuhi na hadi inakaribia ya saa 12 jioni, lilikuwa bado liko pale Dakawa Morogoro likiwa limeharibika na uwezekano wa kuondoka pale ulikuwa ni mdogo.

Kutokana na hali hiyo, mhusika alilazimika kuwaacha pale wenzake hao watatu wakiwa wanasubiria gari hilo, akachukua usafiri mwingine hadi Morogoro na kulala pale. Hakufanikiwa kufika Dar es Salaam siku hiyo, alifika kesho yake
  • Akiwa yupo Mororgoro kwenye lodge jioni hiyo, aligundua kuwa tiketi ya safari yake ilikuwa imepotea
  • Alipofika ofisini baada ya safari hiyo, alimjulisha Boss X kuwa tiketi yake ilipotea wakati wa safari
  • Boss X alimshauri mhusika afanye utaratibu wa kutafuta tiketi nyingine ili aje aitumie kwenye maswala ya kifedha ya ku-retire imprest
UPNEXT:

SAFARI YA PILI, NJE YA NCHI, NDANI YA AFRIKA


…..walisafiri wakiwa wawili na Boss X

……………..inaendelea
 
UPDATE:MONDAY 16 AUGUST 2013

NYONGEZA MUHIMU
KUHUSIANA NA WATU WAWILI WALIOWAHI KUPANDA GHAFLA NDANI YA GARI WALILOKUWA WANAFANYIA KAZI MHUSIKA NA WENZAKE, PALE SINGIDA MJINI


Watu hawa ni wale ambao mhusika tayari amewaongelea kwenye post hii hapa #757 na ambao siku hiyo walipelekea mabadiliko ya sehemu za malazi za watatfiti hawa, pindi walipokuwa bado wapo Singida mjini wakijaribu kukiweka sawa kituo cha matetemeko ya Ardhi mahali pale
  • Watu hawa wawili waliingia ndani ya gari ghafla muno, kiasi kwamba mhusika aliwaona wakati wanaingia tu na hakuwa amewaona kabla, walipokuwa bado wako nje
  • Gari haikupaki pembezoni mwa barabara ili kuwachukua watu hawa, bali ilifanya kusimama kwa sekunde chache tu bararbarani na hatimaye kuwachukua wakaingia ndani ya gari
Kwa hiyo watu hawa walifanikiwa kuingia ndani ya gari kwa uharaka fulani uliokaribiana na ule wa askari jeshi wanapokuwa wanapanda kwenye magari yao

Zaidi ni kuwa katika hali ya kawaida, watu hawa hawakuwa wanahitaji lift pia kwa sababu kutoka sehemu ile walipopandia gari na ofisini kwao, hapakuwa na umbali ambao wangehitaji kupanda lift, ukiachilia mbali ukweli kuwa watafiti hawa watatu na gari lao hawakuwa wanaelekea GST Singida

Kwa hiyo mpaka hapa inaonyesha kabisa kuwa watu wale walikaa mahali pale barabarani wakiwa wanawasubiria watatfiti hawa, na katika namna ambayo inaonyesha ni mhusika pekee ambaye alikuwa hana taarifa za uwepo wa watu hao mahali pale, isipokuwa taarifa hizo walikuwa nazo wenzake wawili aliokuwa nao, yaani Boss X na Dereva X
MUBARIKIWE TENA NA BWANA

UPNEXT:

SAFARI YA PILI, NJE YA NCHI, NDANI YA AFRIKA

…..walisafiri wakiwa wawili na Boss X
……………..inaendelea
 
UPDATE:MONDAY 16 AUGUST 2013

SAFARI YA NJE YA NCHI, NDANI YA AFRIKA, DESEMBA 2009

BOSS X NA MHUSIKA WALILAZIMIKA KUSAFIRI BAADA YA MAKOSA YA KIFEDHA KUWA YAMEFANYIKA; KAWAIDA MKUTANO HUU ULITAKIWA UFANYIKIE TANZANIA


Safari hii nayo pia ilikuwa ni kwa ajili ya Mkutano wa Kimatafifa wa kuchakata data za matetemeko ya Ardh, sawa kabisa na ile ambayo mhusika aliwahi kuifanya akiwa peke yake May 20007 kwenye nchi jirani nyingine.

Kawaida mkutano huu ulikuwa umepangwa kufanyikia Tanzania, lakini kwa bahati mbaya wafadhili wa mkutano huo wa mambo ya fedha, walikosea kutuma hela zilizokuwa zinahitajika kwa ajili ya mkutano huo. Badala ya kuzituma Tanzania kwa Boss X, walipitiwa na kuzituma kwa mtu mwingine, nchi jirani. Kwa hiyo kuanzia pale mkutano huo ikabidi ufanyikie kule ambako fedha zilikuwa zimetumwa
  • Kutoka Tanzania walisafiri Boss X na mhusika
  • Washiriki wake walitoka nchi karibia zote jirani na Tanzania, ukiondoa nchi mbili tu
  • Nchi nyingie moja isiyokuwa jirani na Tanzania nayo ilikuwa ni mshiriki pia
Boss X na mhusika na waliwasili nchi jirani majira ya jioni, wakafikia kwenye hotel ambayo mwenyeji wao alikuwa amewaandalia malazi.

WAKIWA TAYARI WAMESHAWASILI NCHI JIRANI AMBAYO MKUTANO HUO ULIKUWA UNAFANYIKIA……..

Kesho yake walilazimika kubadilisha hotel kwa sababu ile waliyokuwa wamefanyiwa booking na mwenyeji wao ilionekana kuwa gharama yake kwa siku ni kama mara 4-5 zaidi ukilinganisha na gharama za hitel zingine za hadhi hiyo na ambazo zilikuwa zinapatikana kwa urahisi tu jijini hapo walipokuwa wanafanyia mkutano huo

Ikumbukwe pia kuwa, katika ile safari yake ya kwanza aliyowahi kusafiri akiwa peke yake May 2007, mhusika aliwahi pia kufanya mchakato huu wa kubadilisha hotel na kwa sababu zile zile kama zilizojitokeza huku kwenye chi hii nyingine Desemba 2009. Kipindi hicho, waliobadilisha walikuwa ni kundi la watu kutoka nchi kadhaa, baada ya kuwa ameshawishiwa na mmojawapo wa washiriki kutoka nchi nyingine jirani ambaye alikuwa ni binti (tumwite binti X, kutoka nchi X)

Kwa hiyo kulipokuwa kumekucha, kesho yake waliamua kubadilisha hotel na kuhamia kwingine
  • Katika washiriki wote waliokuwa wamehudhuria mkutano huo, waathirika wa booking ya gharama ya kiwango hicho cha juu mno walikuwa ni watatu, yeye mhusika, Boss X na binti mwingine aliyekuwa ametoka nchi jirani (huyu tumwite binti Y, kutoka nchi Y)
  • Kwa bahati nzuri, washiriki wengine wote walikuwa wamebahatika kufanyiwa booking kwenye hotel nyingie moja iliyokuwa na bei za kawaida
  • Binti X sfari hii hakuwepo kwenye mkutano huo, isipokuwa kwa mtu mwingine alikuwepo kwa ajili ya uwakilishi wa nchi X
NAMNA MCHAKATO WA KUHAMIA KWENYE HOTEL ZA BEI ZA KAWAIDA ULIVYOKUWA

…………………inaendelea
 
NAMNA MCHAKATO WA KUHAMIA KWENYE HOTEL ZA BEI ZA KAWAIDA ULIVYOKUWA

…………………inaendelea


Wakiwa wapo pamoja na washiriki wenzao kadhaa ambao wao (washiriki hao) walikuwa wamefanyiwa booking kwenye hotel yenye bei ya kawaida, walianza mchakato wa kuzunguka jijini wakiwa kwenye magari wakisaka hotel

Baada ya kuwa wamepitia kwenye sehemu mbili au tatu hivi ambazo bado bei zake hazikuwafurahisha, hatimaye walifika kwenye hotel nyingine ambayo bei yake ilikuwa ni Dollar 40 (40USD) kwa siku, Bed nad Breakfast
  • Hii ilionekana kuwa ina bei ya chini zaidi kuliko zote zile ambazo walikuwa wamezipita awali siku hiyo
  • Boss X aliamua kubaki kwenye hotel hii
  • Mhusika naye pia hakuona haja ya kuendelea kusaka Hotel nyingine zaidi ya hii ukiingatia kuwa hii ilikuwa na bei ya chini kupita zingine zote zile walizokuwa wameziacha
Kwa hiyo mhusika naye aliamua kuchukua chumba kwenye hotel hii. Hata hivyo, Binti Y yeye alikuwa bado hajaridhika na bei hiyo, aliamua kutokuchukua chumba mahali pale

Boss X na mhusika walimuacha akaendelea na kwenda sehemu nyingine ambako alifanikiwa kupata hotel nyingine.

Siku hiyo, baada ya mhusika na Boss X kuwa wamepata hotel, mtu pekee aliyeendelea kubaki hana chumba baada ya hapo na hivyo kuendelea kutafuta chumba ni Binti Y pekee

Baada ya zoezi hili, mkutano uliendelea, ukaisha salama na hatimaye mhusika na Boss X kufanikiwa kuanza safari yao ya kurudi Tanzania. Kwenye siku hiyo ya kurudi kwao, walipofika kwenye Airport ya kuondokea, ndipo walipokutana na watu watatu, wawili staff-mates na mwingine wa tatu akiwa ni retired, senior staff mate wao

Ndege iliyowarudisha nyumbani iliwasili JNIA baada ya saa 4 au 5 sa usiku. Ilikuwa ni ndege ya usiku

UP NEXT:

BAADHI YA MAENEO YA MFANANO WA SAFARI HII YA DESEMBA 2009 NA ILE ALIYOWAHI KUIFANYA MHUSIIKA AKIWA PEKE YAKE MWAKA 2007
 
BAADHI YA MAENEO YA MFANANO WA SAFARI HII YA DESEMBA 2009 NA ILE ALIYOWAHI KUIFANYA MHUSIIKA AKIWA PEKE YAKE MWAKA 2007

MKUTANO WA MAY 2007


Kwenye mkutano huu wa 2007 ambapo mhusika alisafiri peke yake, kulikuwa na zoezi la kwenda kubadilisha fedha kutoka kwenye local currency na kuwa dollar
  • Muandaaji wa Mkutano huo alikuwa amebadilsha dollar na kuziweka kwenye local currency
  • Kawaida alitakiwa abaki na dollar na kuwalipa washiriki pesa ikiwa kwenye dollar
Kwa hiyo kuna siku washiriki walilazimika kwenda kupanga foleni kwenye misururu mirefu bank, wakiwa wanahitaji kununua dollar kwa kutumia local currency ya nchi hiyo

Kilichomfanya muandaaji wa mkutano huu kufanya hivi hakijulikani hadi leo. Hata Boss X baada ya kuwa amesikia kuwa ilifanyika hivyo, naye pia hakuweza kujua kwa nini muandaaji huyo aliamua kufanya hivyo
  • Kulikuwa na Binti X kutoka nchi X aliyehamasisha baadhi ya washiriki kuhamia kwenye hotel nyingine ambayo ilikuwa ni rahisi zaidi, na washiriki wote walikubali kufanya hivyo isipokuwa washiriki wawili waliokuwa wametoka nchi moja na mwingine mmoja kutoka nchi nyingine moja
  • Rates za hotel waliyokuwa wamefanyiwa booking na mwenyeji wao zilikuwa zinaonekana kuwa juu kuliko kawaida au zilikuwa overcharged, kitendo kilichokuwa kinawa-prompt baadhi ya waliokuwa wamefanyiwa booking hizo, kuhama kutoka kwenye hotel hiyo
  • Washiriki wote isipokuwa watatu, walibadilisha hotel

MKUTANO WA DESEMBA 2009
  • Muandaaji wa Mkutano huo naye pia alikuwa amebadilsha dollar na kuziweka kwenye local currency
  • Kawaida alitakiwa abaki na dollar na kuwalipa washiriki pesa ikiwa kwenye dollar
Kwa hiyo kuna siku washiriki walilazimika kusafiri umbali mrefu na kwenda kupanga foleni bank, wakiwa wanahitaji kununua dollar kwa kutumia local currency ya nchi hiyo.

Kwa bahati nzuri tu ni kwamba safari hii hapakuwa na msururu mrefu wakati wa kununua dollar, ila iliwabidi wasafiri kwa gari umbali mrefu kidogo kwenda jiji jingine la jirani ambako ndiko biashara hiyo ilisemekana kufanyika.

Mhusika hakuweza kujua kwa nini hawakuweza kufanya biashara hiyo kwenye jiji lile lile walilokuwa wanafanyia mkutano, ila badala yake iliwabidi wasafiri kwenda jiji jingine lililokuwa jirani
  • Kulikuwa na Binti Y kutoka nchi Y ambaye alionekana kama alikuwa anataka kupata attention kwa kutumia swal la kubadilisha hotel (fuata nyuki ule asali)
  • Rates za hotel waliyokuwa wamefanyiwa booking na mwenyeji wao zilikuwa zinaonekana kuwa juu kuliko kawaida au zilikuwa overcharged, kitendo kilichokuwa kinawa-prompt waliofanyiwa booking, hizo kuhama kutoka kwenye hotel hiyo
  • Washiriki wote isipokuwa watatu, walikuwa wamefanyiwa booking kwenye hotel yenye rate za kawaida hali iliyopelekea washiriki watatu kubadilisha hotel, mmoja wao akiwa ni Bint Y
MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE:TUESDAY 16 AUGUST 2013

NYONGEZA MUHIMU: STAFF-MATES AMBAO MHUSIKA AMEWAHI KUKUTANA NAO PINDI ALIPOKUWA YUPO SAFARINI


Mhusika amewahi kukutana na staff-mates watatu watatu kila safari kwenye jumla ya safari tatu.

SAFARI YA MAY 2007, NJE YA NCHI

Alikutana na staff-mates watatu alipokuwa akibadilisha ndege kwenye nchi jirani

SAFARI YA DESEMBA 2009, NJE YA NCHI

Alikutana na staff-mates watatu alipokuwa akisubiria kuPanda ndege ya kurejea nchini Tanzania

SAFARI YA MAY 2012, DODOMA

Alikutana na staff-mates watatu na alipanda nao basi moja kurudi jijini Dar es Salaam

Migongano hii ya safarini inaweza kuwa ni coincidences za kawaida tu, especially mtu anapokuwa ana chances nyingi za kusafiri safIri. Hata hivyo katika kujaribu kukwepa biaseness kwenye namna ya kuzitafsiri coincidences hizi, mhusika, alilazimika kutaja majina ya watu hawa kwa “SPECIALST”, kiongozi yule ambaye mhusika aliwahi kufanya naye mazungumzo ya kina mwanzoni mwa mwaka 2016

Kwa hiyo mpaka muda huu, mtu pekee anayewajua watu hawa ni “SPECIALST”. Boss X yeye anawajua wale wa safari ya 2009 tu

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Nikikutana na watu wa iana hii tukaongea kidogo nawaambia nimebandika maharage jikoni nawahi yanaanza kuungua. Au nina wahi kuchukua dawa boss lady hayuko vizuri.
 
UPDATE:THURSDAY 19 AUGUST 2013

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA VITUO VYA MATETEMEKO VYA ENGARESERO, KETUMBEINE NA ENGARUKA


Kwa mara ya kwanza, vituo hivi viliwekwa Julai 2007
  • Vituo hivi vilitakiwa kukaa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu tu na baada ya hapo vitolewe
  • Utaratibu huu ulifuatawa na kweli ilipofika Desemba 2008, vituo hivyo viliondolewa na havijawahi kuwepo tena hadi leo hii
Ukiondoa safari ya mwisho kabisa kwenye vituo hivyo ambayo mhusika ndiyo alishiriki kwa mara ya kwanza; safari ambayo ilihusiana na kuviondoa moja kwa moja vituo hivyo, safari zingine zote kuanzia ya kwanza (iliyohusisha kwenda kuviweka vituo hivyo) zilimhusisha Staff X

Mpaka hapa, kwa amoni yake yeye mhusika, anadhani kuwa pengine hapakuwa na haja sana ya mhusika ku-swap na Staff X kwa wakati huu wa safari hii ya mwisho ukizingatia kuwa Staff X tayari alikuwa ameshakuwa na uzoefu na eneo hilo; ambalo kwa wakati huo lilikuwa linakabiliwa pia na chnagamoto za kiusalama kwa kutokuwa na mawasialiano ya simu

Kwa maoni yake yeye mhusika, anaona kuwa swapping ya mhusika na Staff X ingeweza kufanyika:
  • Aidha safari mbili au tatu nyuma, kabla ya safari ya mwisho ya kwenda kuondoa vituo hivyo, ili kumfanya mhusika naye awe na uzoefu na mazingira ya huko na pia kumfanya ajue na tahadhari za kiusalama anazotakiwa kuwa anazichukua pindi anapokuwa anafanya kazi maeneo hayo
  • Au, baada ya vituo hivyo kuwa vimeondolewa, kumwepusha mhusika kufanya kazi kwenye mazingira mageni ya huko na ambayo alitakiwa afanye kazi huko kwa mara moja tu
Kwa hali hiyo, hapakuwa na haja ya msingi sana ya kumpeleka mhusika kwenda kufanya kazi kwenye maeneo hayo na kwa mara moja tu!.

AIDHA alitakiwa awe ameshafanya safari kadhaa za huko kabla ya muda wa vituo hivyo kuwa umeisha, ili awe-oriented na mazingira ya kule AU alitakiwa asifanya kazi kabisamaeneo hayo kwa sababu vituo hivyo vilikuwa ni vya muda mfupi tu huko

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE:THURSDAY 19 AUGUST 2013

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA VITUO VYA MATETEMEKO VYA ENGARESERO, KETUMBEINE NA ENGARUKA


Kwa mara ya kwanza, vituo hivi viliwekwa Julai 2007
  • Vituo hivi vilitakiwa kukaa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu tu na baada ya hapo vitolewe
  • Utaratibu huu ulifuatawa na kweli ilipofika Desemba 2008, vituo hivyo viliondolewa na havijawahi kuwepo tena hadi leo hii
Ukiondoa safari ya mwisho kabisa kwenye vituo hivyo ambayo mhusika ndiyo alishiriki kwa mara ya kwanza; safari ambayo ilihusiana na kuviondoa moja kwa moja vituo hivyo, safari zingine zote kuanzia ya kwanza (iliyohusisha kwenda kuviweka vituo hivyo) zilimhusisha Staff X

Mpaka hapa, kwa amoni yake yeye mhusika, anadhani kuwa pengine hapakuwa na haja sana ya mhusika ku-swap na Staff X kwa wakati huu wa safari hii ya mwisho ukizingatia kuwa Staff X tayari alikuwa ameshakuwa na uzoefu na eneo hilo; ambalo kwa wakati huo lilikuwa linakabiliwa pia na chnagamoto za kiusalama kwa kutokuwa na mawasialiano ya simu

Kwa maoni yake yeye mhusika, anaona kuwa swapping ya mhusika na Staff X ingeweza kufanyika:
  • Aidha safari mbili au tatu nyuma, kabla ya safari ya mwisho ya kwenda kuondoa vituo hivyo, ili kumfanya mhusika naye awe na uzoefu na mazingira ya huko na pia kumfanya ajue na tahadhari za kiusalama anazotakiwa kuwa anazichukua pindi anapokuwa anafanya kazi maeneo hayo
  • Au, baada ya vituo hivyo kuwa vimeondolewa, kumwepusha mhusika kufanya kazi kwenye mazingira mageni ya huko na ambayo alitakiwa afanye kazi huko kwa mara moja tu
Kwa hali hiyo, hapakuwa na haja ya msingi sana ya kumpeleka mhusika kwenda kufanya kazi kwenye maeneo hayo na kwa mara moja tu!.

AIDHA alitakiwa awe ameshafanya safari kadhaa za huko kabla ya muda wa vituo hivyo kuwa umeisha, ili awe-oriented na mazingira ya kule AU alitakiwa asifanya kazi kabisamaeneo hayo kwa sababu vituo hivyo vilikuwa ni vya muda mfupi tu huko

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
Cjui Ni akili yangu au n mm tu ndo nawaza hvyo maana kila nikisoma hiii kitu namuwaza mtu 1 tu... Ngoja niendelee kula mtoriiii nyama ntakuta chini mkuuu
 
USHAURI MUHIMU KWA WAKUU WA KAZI WA MHUSIKA

Hizi hela zake zisipokuwa zimelipwa, MR X hawezi ku-behave kama binadamu wa kawaida. Ataendelea tu kufanya mambo ya ajabu. Ili aweze kurudi katika hali yake ya kawaida, mhusika anashauri maslahi yake haya yalipwe. Na kama hayapo, basi apewe jibu hilo
Kwa mfano, kwa kipindi cha hivi karibuni, MR X amekuwa akitengeneza wake na wachumba bandia wa mhusika kuanzia maeneo ya ofisini hadi Kanisani.

Awali, mhusika alidhani kuwa wanaohusika na hili walikuwa Kiongozi Mkuu tu na yule mwenzake mhubiri special, kumbe hapana. Hata MR X naye pia yumo. katika hili, tayari mhusika ameshaona kitu kikiwa kinaendelea maeneo ya ofisini ambacho kimemuhakikishia kuwa yalikuwa ni maandalizi yaliyofanywa na MR X

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
Sema ifike mahali mhusika aoe ili aondokane na hizi changamoto ndogo ndogo
Imagine amekuwa single hadi anatengenezewa wachumba fake😅
 
UPDATE:WEDNESDAY 25 AUGUST 2021

BADO ANAENDELEA KUSUBIRIA MALIPO YA MALIMBIKIZO


Tofauti na kipindi cha awali, safari hii anasubiria malipo ya malimbikizo kwa hamu kubwa sana. Angalau anatamani ayapate ili aweze kununua ki-engine kingine ili afunge kwenye gari lake, maana hii engine nyingine aliyofungiwa kama zawadi, hana uhakika kama inaweza kumfikisha hata Kibaha, just in case ameamua kwenda huko

Anatamani apate hela ili afunge ki-engine kingine ambacho knaweza kumpeleka angalau Chalinze, kama akiamua kwenda huko

Mwishoni mwa mwezi uliopita wa saba hajaona kitu, jana pia notification ya sms imeingia kwenye simu yake ikiwa haina chochote kipya

Angalau anaomba apewe hizi hela, na kama hapewi basi ajulishwe kuwa hapewi, au hazipo

Inashangaza kidogo kwamba hizi hela anapoamua kuacha kuzifuatilia, wanapatikana watu wa kumhamsisha azifuatilie. Akianza kuzifuatilia, zinaanza tena kuonyesha dalili kuwa hazipo. Inashangaza sana

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UP NEXT:
STORI KUTOKA KWENYE KORIDO ZA OFISINI:
ALICHOWAHI KUTONYWA MHUSIKA KUHUSIANA NA “SPECIALIST"
 
TUKIO LA KWANZA NDANI YA JENGO: LILIMHUSISHA MKUU WA IDARA WA KIPINDI HICHO MNAMO OKTOBA/NOVEMBA 2015

Tukio hili la kwanza lilimhusisha Mkuu wa Idara wa kipindi hicho


  • Llilitukia kati ya Oktoba/ Novemba 2015
  • Wakati linatokea, Mkuu wa Idara huyu alikuwa bado ni mpya kabisa kwenye nafasi hiyo kwa sababu alianza kutumika kwenye nafasi hiyo mnano Julai 2015
  • Lilitukia katika kipindi ambacho wanafunzi walikuwa bado wako likizo
Kwa kifupi ni kwamba kuna mtu wa ajabu alitokea ndani ya jengo siku ya J2 na kumshambulia Mkuu wa Idara, almanusura amuue

  • Mtu huyo alikuwa anajaribu kuiba Kompyuta aina ya Mac, na ambayo japo ilikuwa ni ya gharama kubwa kidogo, lakini si watu wengi wanaojua kuzitumia au wanapenda kuzitumia, hali inayopelekea kuutokuwa na soko zuri sana hapa nchini kwetu
  • Siku huiska, hapakuwa na mtu mwingine ndani ya jengo. Mkuu huyu alikuwa peke yake
  • Inakadriwa kuwa ilikuwa ni mchana, kwenye mida ya takribani saba hivi
  • Mkuu Ilibidi aruke kutoka ghorofa ya kwanza hadi chini ili kuokoa miasha yake
Tukio hili la kwanza ndani ya jengo, ndiyo lilikuja baadaye tena, lika-trigger tukio jingine la pili ndani ya jengo hilo hilo, ambalo LENYEWE (TUKIO LA PILI) HALIKUMHUSISHA TENA MKUU WA IDARA, BALI MHUSIKA.

Kwa hiyo tukio la kwanza lililowahi kumpata Mkuu wa Idara, Oktoba/ Novemba 2015, ndiyo hilo hilo lilikuja baadaye tena kupelekea mhusika naye kupatwa na tukio jingine ndani ya jengo hilo hilo

Maelezo ya kina kuhusiana na matukio haya mawili, yatafuata mufa mfupi ujao



TUKIO LA PILI NDANI YA JENGO: LILIMHUSU MHUSIKA MWENYEWE: JANUARY 2016

  • Mtu yule yule wa ajabu aliyewahi kumshambulia Mkuu wa Idara alirudi tena ndani ya jengo
  • Safari hii alirudi kama mgeni wa kawaida tu, ndani ya ofisi ya Mkuu wa Idara, kitendo kilichopelekea Mkuu kufanikiwa kumtambua mtu huyu kwa sura na kwa umbile lake pia
  • Siku hiyo, mhusika aliingia ofisini kwa Mkuu na baada ya muda kitambo mtu huyo naye akawa amefika ofisini humo
  • Mkuu wa Idara ambaye ndiye aliwahi kushambuliwa na mtu huyo, akamtambua hasimu wake huyo na hapo hapo akatoa amri kuwa watu wote waliokuwa humo ndani ya ofisini yake wasitoke nje
  • Mhusika naye pia alikuwa mmojawapo wa watu hao waliokuwemo humo ndani. Na hakuwa na hata zaidi ya dakika mbili tangu aingie ofisini humo
Baada ya hapo, badala ya Mkuu wa Idara kupiga simu Polisi ili Polisi waje wamchkue mshukiwa wake, Mkuu huyo alitoa amri akimwambia mhusika pamoja na dereva wake Mkuu, na Mkuu mwenyewe, kwamba watatu hawa kwa ujmla wao wamchukue mtu huyo na kumpeleka Kituo cha Polisi.

Hata hivyo, mhusika siyo Polisi na hajawahi kuwa Polisi, na wala utaratibu wa kukamata mshukiwa huwa hauendi hivyo. Mkuu wa Idara alitakiwa apige simu Polisi kisisrisiri na kuwaomba waje wamkamate mtuhumiwa huyo



………………..inaendelea
SAHIHISHO MUHIMU KWENYE TAARIFA ILIYONUKULIWA HAPA JUU:
Tukio la kwanza ndani ya jengo lililoelezwa hapa lilitokea kati ya Julai /August 2015 na si kati ya Oktoba na Novemba 2015 kama ilivyoelezwa kwenye maelezo haya
 
Kweli hii ni ya wenye muda wa kupoteza.
 
UPDATE:FRIDAY 03 SEPTEMBER 2021

STORI KUTOKA KWENYE KORIDO ZA OFISINI: ALICHOWAHI KUTONYWA MHUSIKA KUHUSIANA NA “SPECIALIST”


Kwa wasomaji wa siku zote wa uzi huu, huyu “SPECIALIST” ni kiongozi kwenye taasisi anoypfanyia kazi mhusika, ambaye mhusika aliwahi kuelekezwa kwake ili ampatie kiongozi huyu taarifa alizokuwa nazo na ambazo kwa wakati huo zilikuwa ni za siri. Lengo hasa lilikuwa ni “SPECIALIST”aweze kuziwasilisha taarifa hizo kwenye mamlaka nyingine za juu ili ziweze kufanyiwa kazi

Tayari mhusika ameshamwongelea kiongozi huyu na mojawapo ya posts alizomwongela ni hii hapa #514

Mhusika alifanya kama alivyokuwa ameelekezwa na waliwahi kufanya mazungumzo yaliyochukua muda mrefu kidogo, akiwa anawasilisha taarifa zake kwa “SPECIALIST”; taarifa ambazo kwa wakati huu, anadhani kuwa (zote au sehemu kwa sehemu kubwa) “SPECIALIST”; hakuzifikisha kule ambako zilikuwa zinatakiwa kufikishwa; kitu kilichopelekea mhusika kuanza kutuhumiwa kuwa na dalili za kuugua ugonjwa wa akili kuanzia pale

Kile alichowahi kutonywa mhusika akiwa mazingira ya ofisini:
  • Ni kwamba Julai 2015 “SPECIALIST” aliwahi kuhusika kwenye hoax” iliyomhusisha Mkuu wa Idara wa kipindi hicho aliyewahi kuanguka kutoka juu ghorofa ya kwanza,habari ambayo mhusika tayari ameshaiongelea humu kwenye post hii hapa #505
  • Tukio hili lilitokea kwenye miezi kati ya Julai na August 2015
  • Baada ya tukio hili kutokea na mhusika kutoridhishwa na mazingira yake kwa kuona kuwa lilikuwa ni la kutengenezwa, “SPECIALIST” akiwa kama mmojawapo wa waandaaji wa tukio hili, akawa yuko kwenye hofu kwa sababu set-up ya mtego wake ilikuwa imeshindwa kuwa fool proof
  • “SPECIALIST” wakati huo akiwa anajua kuwa mhusika naye pia alikuwa ana tuhuma za tangu May 2014 ambazo mpaka Septemba 2015 zilikuwa bado zipo, kwamba aliwahi kukaidi maagizo ya kazi kutoka kwa wakuu wake wa kazi, “SPECIALIST” akaona sasa the only alternative ni kukaa chini na huyu mtu ili ikiwezekana kuwe na reconciliation itakayopelekea uwepo wa cancellation effect; kwamba wawili hawa waweze ku-negotiate ili mhusika afutiwe tuhuma zake zinazomkabili ofisini, ili asiendelee kupifga kelele kuhusiana na swala la Mkuu wa Idara aliyewahi kuanguka kutoka juu ghorofa ya kwanza
Kutokana na hali hii, ilipofika mnamo July/ August 2015, wanafunzi wakiwa wako likizo, “SPECIALIST” alimpigia simu mhusika ili waweze kuonana na kuongea
  • Wakati huo mhusika alikuwa hajui chochote kile kuhusiana na uhusika wa “SPECIALIST” kwenye maswala haya
  • Nia yake nhusika kwa wakati huo ilikuwa ni kuonana na uongozi wa juu kabisa wa taasisi na kuupatia uongozi huo taarifa hizo
  • Baada ya mhusika kuonana na “SPECIALIST”, hakuridhika kuongea na “SPECIALIST” peke yake, bali alitamani pia hata viongozi wengine wa juu waweze kuwepo kwenye maongezi hayo
Baada ya siku hiyo kuwa imepita, mhusika na “SPECIALIST” wakiwa hawajafikia muafaka wa namna ya kufanya maongezi yao,kukawa kumekuwa kimya kwa muda. Hata hivyo, ilipofika siku ya kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015; mhusika akakakoswa koswa kwenye shambulio jingine la hatari akiwa mazingira ya ofisini, karibu na pale kilipokuwa kituo chake cha kupigia kura. Details za tukio lililomsibu siku hiyo anaziwthhold. Ilikuwwa ni siku ya Jumapili

Ilipofika February 2016, mhusika alifutiwa tuhuma zilizokuwa zikimkabili na akaelekezwa aende akaonane sasa na “SPECIALIST” ili waweze kuongea

Wakati huo huo, Mkuu wa Idara aliyewahi kuanguka kutoka ghorfa ya kwanza akahamishwa idarani na kupelekwa Central Administration

Details zaidi za tukio hili zitafuata baadaye

…………itaendelea

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: TUESDAY 14 SEPTEMBER 2021

AUDIO CLIP NYINGINE YA KILE ALICHOWAHI KUKIONGELEA MHUSIKA KWENYE POST HII HAPA #85


  • Ni makofi yanayotumika kama secret code ya kurusha mapepo Kanisani
  • Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (KM-A) ndiyo kiongozi mkuu wa makofi ya aina hiyo
  • Makofi hayo huwa yanapigwa baada ya sala ya kufungua au kufunga Ibada ya Kusifu na Kuabudu
  • Huwa yanapigwa kabla ya waumini kuwa wametamka neno “Amina”
  • Waumini wakishatamka neno “Amina”, na makofi ya aina hiyo yakiwa tayari yameshapigwa, hakuna makofi mengine tena ambayo huwa yanapigwa baada ya hapo
Katika hali ya kawaida, makofi yote huwa yanapigwa baada ya waumini kuwa wametamka neno “Amina”

Audio clip iliyoambatanishwa hapa chini ni ya kwenye Semina iliyowahi kufanyika Kanisa A January 2013

Kwa mara nyingine tena wasomaji wa uzi huu mnaombwa kuisikiliza audio clip hiyo

NB: Audio clips zingine za awali ziko kwenye post hii hapa #248 kwa wale ambao hawakuwahi kuzisikiliza

MUBARIKIWE TENA NA BWANA

UP NEXT: ALICHOWAHI KUTONYWA MHUSIKA KUHUSIANA NA “SPECIALIST”

……………….inaendelea

 
UPDATE:WEDNESDAY 15 SEPTEMBER 2021

SAHIHISHO MUHIMU


AUDIO CLIPS ZILIZO KWENYE POST HII HAPA #248 ZIMEFANANA

Audio clips hizo zilitakiwa kuwa tofauti. Kwa hiyo mojawapo ya audio clips hizo ina miss, yaani haipo

Clip hiyo inayomiss ni hii iliyoambatanishwa kwenye post hii hapa chini

 
Sikiliza pia audio clip mpya kwenye post hiyo hapo juu #780 , inayohusiana na secret code ya kupiga makofi kabla ya waumini kuwa wametamka neno "Amina"
 
UPDATE: THURSDAY 16 SEPTEMBER 2021

AUDIO CLIP NYINGINE YENYE “MAKOFI VERY SPEIAL”


Audio clip hii nayo pia ina makofi yale ambayo huwa yanapigwa baada ya sala ila kabla ya neno “AMINA”, kuwa limetamkwa. Hata hivyo, makofi yaliyoko kwenye audio clip yako very special kwa sababu yenyewe hayakufuatiwa kabisa na “AMINA” baada ya kuwa yamepigwa kwa maana kuwa makofi pekee ndiyo yalihitimisha sala hiyo bila ya neno “AMINA” kuwa limetamkwa mwisho was sala hiyo.
Kwa hiyo basi, kwenye sala hiyo siku hiyo:
  • Neno “AMINA” halikutamkwa kabisa siku hiyo baada ya sala hiyo. Makofi pekee ndiyo yaliitimisha sala hiyo
  • Mtoa sala alikuwa ni Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (KM-A)
  • J2 hiyo, KM-A aliwaomba waumini wapige makofi hayo kabla hajasema neno “AMINA”
  • Baada ya waumini kupiga makofi, neno “AMINA” halikupata nafasi tena ya kutamkwa mwishoni mwa sala hiyo
Kwa hiyo makofi pekee ndiyo yalihitimisha sala hiyo. Ilikuwa ni J2 ya sikukuu ya watoto, mwezi May 2012 wakati wa Ibada ya kwanza ambayo ilikuwa ni ya Kiingereza

HALI ILIVYO "KANISA A" KUHUSIANA NA DVD AMBAZO ZIMEKUWA ZIKIREKODIWA KWENYE SIKU MAALUM AU SIKU ZA SIKUKUU

Kwa hali ilivyo sasa, sikukuu hizo zikemuwa zikirekodiwa lakini DVD zake hazitengenezwi tena, na kama zinatengenezwa basi haziletwi tena sokoni kwa ajili ya kuuziwa waumini

Kwa hiyo siku hizi ni mara chache sana wanarekodi na kuuza DVD za aina hii, na wakifanya hivyo basi inakuwa ni kwa mhudumu anayetoka nje ya Kanisa. Sikukuu za watoto hazina tena DVD kama ilivyokuwa zamani. Tangu mhusika arudi kutoka uhamishoni Kanisa B mwezi April 2017, hajawahi kufanikiwa tena kuona DVD zinauzwa kwa sikuku za aina hiyo, hazipo tena

Possibly KM-A amezipiga marufuku baada ya kuona zinaweza kuja kutumika kama ushahidi wa kuuthibitisha ujinga wake ambao bado anaendelea kuufanya akiwa amepanda madhabahuni.

….”mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu…….”

Halafu wakifariki viongozi anakuwa wa kwanza kupanda kwenye madhabahu hiyo hiyo anayoitumia kipumbavu; kwa ajili ya kutoa neno la faraja. Kwenye post hii #592 mhusika aliwahi kumpongeza sana KM-A kwa fundisho lake alilowahi kulitoa kwenye Ibada ya J2 ya tarehe 22.03.2021

Na anajua kweli namna ya kutoa neo la faraja mpaka kuna kipindi mhusika ilibdi ampongeze kwa hilo

MUBARIKIWE TENA NA BWANA



UP NEXT: ALICHOWAHI KUTONYWA MHUSIKA KUHUSIANA NA “SPECIALIST”

……………….inaendelea
 
Back
Top Bottom