Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Du, Basi umeutoa sadaka muda wako, siyo mchezo. Mungu akubariki
 
Nashukaaa nayo
 
Nashuka
 
Nasongaaaa
 
Nakubaliana na Ww hii Story iliruka EFM na Sio RFA,,Hata ukiingia Youtube unaikuta
 
Ubarikiwe kwa muda wako
 
Kule ambapo Rojas alichimba pesa, ilionekana kuna pesa zingine aliziacha, vipi?

Mbona kipindi cha kumzika yule mfungwa, hatukusikia hata nduguzake wamesemaje? Hatukusikia watoto wa mfungwa na wanawake wote wawili wa mfungwa walisemaje?

Pia, yule mfungwa alipata wapi hizo pesa?
 
Mkono mmoja nisaidie kujibu haya maswali.
 
Kwa maelezo ya mhusika hakufafanua moja kwa moja ila kule kijijini hakuacha pesa kwani matranka yote yaliyokuwepo aliyabeba,kuzikwa kwa mfungwa inaonekana hakutaka kuwajuza watoto kwani alihofia kuwaumiza kisaikolojia,wale wanawake na hasa yule mama wa watoto hakujua kuwa chanzo cha misaada yote ni mzazi mwenzake na Rojas hakutaka kuianika siri hyo na hakumjuza kuhusu kifo chake kwani huyu mwanamke kwanza hakujali nafasi ya yule mzazi mwenzake na pia rojas nahisi alikataa kumjuza nadhani alijua akijua anaweza waambia watoto,kuhusu yule mwanamke mwingine kumbuka Rojas alitembea nae na nafsi yake ikajutia sana na kujiona ni kama mwenye hatia kwa rafiki yake na mahusiano yao kati ya Roja na yule mdada yaliharibika nadhani ndio chanzo cha kutomjuza kuhusu kifo cha yule jamaa.
Kuhusu ndugu zake kutohudhuria mazishi kwa upeo wangu nadhani Rojas kama unakumbuka uondokaji wake baada ya kupata pesa hvyo hakutaka tena ukaribu na jamii ya kule
 
Kuhusu alipozipata pesa ni siri aliyokufa nayo mwenyewe kwani hata Rojas hakufanikiwa kulijua hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…