Mkasa: Wema ni akiba, usiache kutenda wema

Mkasa: Wema ni akiba, usiache kutenda wema

Part Two
1963

Mwaka 1963 Walipata kijana wa kiume wakamuita Edward, furaha iliongezeka maana familia imepata mwanachama mpya.

Mwaka 1965 walipata mtoto wa pili wakamuita Edwin furaha ilizidi mara dufu. Familia ikawa na watu wanne.

Mwaka 1974 walipata mtoto wa tatu wakamuita Edson. Hapa sasa Anthony akaona kuna umuhimu wa kutafuta kazi ili aweze kumuda mahitaji ya familia.

Mwaka 1976 TAZARA walitangaza nafasi za kazi, Anthony alitumia nafasi hiyo kuomba kazi, bahati ikawa yake akapata kazi na kituo chake cha kazi kikawa kijiji cha kitete, wilaya mrimba, mkoa wa Iringa.
***
Hii ni simulizi ya maisha halisi ya Edson kijana wa tatu wa mzee Anthony na mama Antonia.
****
Naitwa Edson Anthony,nina haiba ya upole. Nimezaliwa mwaka 1974 katika kijiji 'X' wilaya 'X' mkoa 'X'. Mimi ni mtoto wa mwisho kati ya watoto watatu wa mzee Anthony na mama Antonia.

Kaka yangu wa kwanza anaitwa Edward (RIP) na mwingine ni Edwin.

Baba yangu ni mwenyeji wa 'X' mama yangu ni mwenyeji wa ''X'' lakini amekulia Arusha. Baba yake alihamia mkoa huo kutoka mkoa wake wa ''X'' .

Baba yangu mzee Anthony alikuwa ni mwajiriwa wa TAZARA (Tanzania and Zambia Railway) Kituo chake cha kazi kilikuwa kijiji cha kitete wilaya ya mrimba mkoa wa Iringa.

Maisha yalikuwa mazuri kiasi na yenye furaha na upendo. Baba alikuwa na ng'ombe wapatao 50 na buzi 70, pale kijijini kwetu. Kutokana na mifugo ikabidi mama abaki pale kijijini kwa ajili ya uangalizi wa mji.

Tulikuwa na mashamba ambayo tulikuwa tunajipatia chakula kama mihogo, viazi, mtama, uwele, ufuta yaani tulikuwa tunafanya kilimo mseto.

Napenda kuchukua nafasi hii kusimulia histori ya maisha yangu, kuanzia malezi, elimu, mapenzi, utafutaji wa pesa na mafanikio yangu maishani.
**********

1974-1989

Maisha ya utoto

Nimezaliwa na kulelewa pale kijiji cha 'X', kabla ya kuanza shule nilikuwa nachunga mifugo yetu.

Kaka zangu walikuwa wanaishi na baba Iringa. Nilibaki mimi kwa kuwa nilikuwa mdogo.

Maisha ya machungani yalikuwa mazuri sana maana tulikuwa tunakamua maziwa ya ng'ombe tunakunywa pindi tukisikia njaa na kiu, nakumbuka moments za kubeba viazi vya kuchoma kwenye mkoba wa ngozi, maziwa kwenye kibuyu n.k

Machunganii ilikuwa ni kawaida kukutana na wachungaji wengine, hapo michezo iliendelea na kufanya nipende kwenda kuchunga.

Mama alinipa malezi naweza sema mazuri sana, mama yangu sio mkali, muda wote sura yake imechanua tabasamu. Baba yangu alikuwa mkimya sana ila aside na masihara.

Safari yangu ya kwanza kwenda Songea

Mwaka 1981 nilipelekwa shule lakini nilishindwa kushika sikio nikarudishwa. Nilianza shule ya msingi mwaka 1982 katika shule ya msingi 'X' nikiwa na miaka 8. Kipindi hicho ilikuwa lazima ushike sikio ndio uandikishwe shule.

Nilikuwa na bidii sana shuleni, pia nilikuwa najua kusoma herufi a, e i o u na kuhesabu mpaka kumi. Ikiwa ni kazi ya mama yangu tukiwa nyumbani nyumbani.

'My mom was my first teacher.'

Nilipofika darasa la pili nilichukuliwa na kaka yangu mkubwa Edward, ambae alikuwa askari mkoa wa Ruvuma wilaya ya Songea.

Nakumbuka siku moja kabla ya safari, sikupata usingizi, nilikuwa nawaza kupanda gari kwenda nje ya mkoa wetu.Nilishawahi safiri kwenda Iringa kwa baba ila nikiwa mgongoni, sasa naenda kwa miguu yangu.

Kesho yake asubuhi mapema mama alinivalisha kisha akanipatia maziwa fresh na mkate nile, baada ya kula alitusindikiza mpaka barabarani. Tulipanda bus linaitwa 'X' kutoka hapo kijijini ''X'' kwenda Mwanza, nili enjoy sana kwa mara ya kwanza. Niliona miti inarudi nyuma kadri gari linavyo kimbia.

Kutoka ''X'' mpaka Mwanza ni masaa kadhaa tu, hatimaye tuliingi standi ya ''X'. Kaka alibeba mabegi yetu tukaenda kutafuta taksi ili kwenda station ya gari moshi, kipindi hicho mabasi yalikuwa yanapita Kenya yanatokea Arusha kwenda Dar-Es-Salaam,njia ya kati ilikuwa ni gari moshi maana barabara haikuruhusu.

Tulifanikiwa kupata tiketi za gari moshi daraja la tatu, kaka alilipia siti 3 ili nipate sehemu ya kulala. Ilibidi tusubiri safari saa 10 jioni. Ilipofika sa 9 tulianza kupanda kwenye gari moshi, saa 10 kamili ilipiga honi mara tatu likaondoka.

Gari moshi liliendelea na safari huku watu wakipiga soga, lilikuwa limejaza sana mpaka abiria wengine walikosa siti wakasimama.Mimi nililala kwenye ile siti, kaka akaenda behewa la askari wenzake kupiga soga.

Siku ya tatu asubuhi kama saa 3 tuliingia Dar-es-Salaam, tulishuka na kutafuta UDA ya kuelekea magomeni kota, kwa mdogo wake na baba…

Siku ya pili tulipanda basi kwenda mpaka makambako, nakumbuka jina la basi 'kiswele coach' lilikuwa linaenda songea ila sisi tulishukia makambako ili twende kwa baba pale kitete.

Makambako tulipanda gari moshi la TAZARA kwenda kitete kwa baba. Kaka aliniacha kwa baba, baada ya wiki moja, baba alinipeleka Songea. Kutoka makambako tulipanda costa, tulifika Songea usiku sana.

……..

Nilipelekwa shule ya msingi Misufini kuendelea na darasa la pili.Kaka yangu alikuwa amepanga nyumba mfaranyaki, (jirani na ilipokuwa Buhemba hotel sijui kama bado ipo.)

Maisha mapya hayakuwa na ugumu sana katika kuzoea mzingira.Kutokana na uchezaji wa mpira nilipata marafiki wengi sana kwa haraka.

Kipindi kile kaka alikuwa na redio kaseti aina Panasonic double decks,alikuwa anapenda sana nyimbo za kongo kina Franco Makiadi, Pepe kale, wengineo.

Alikuwa anapenda sana suruali za kitambaa raini na mashati ya dog dog Kama alivyokuwa wanavaa wana muziki wa kongo.

Kaka yangu alikuwa ni mtu wa hasira za haraka sana 'short-temper', hali iliyopelekea kuchezea kichapo mara kwa mara toka kwa mjeda yule.

Alikuwa ananifunga na pingu mikono na kunipiga kwa waya, mikanda na mateke, wakati mwingine alinibana korodani. Nilipitia mateso sana kipindi hicho.

Pamoja na kuwa alinifanyia ukatili mara kwa mara, alikuwa na upendo sana usipomuuzi, tatizo nilikuwa mtoto nahitaji kujifunza, hakunipa hiyo nafasi.

Kila nguo ikitoka ilikuwa lazima niivae kwanza kabla ya watoto wengine pale mtaani, hilo simlaumu.

Kipindi hicho tunatoka mfaranyaki kwenda standi kuu kula chips mayai. Hakukuwa na vibanda vya chips mitaani, na ni lazima kutumia uma kwenye sahani ya bati ha ha haaaa.

Baada ya kuuzoea mji nilikuwa nafurahia kijichanganya na watoto wemzangu katika michezo. Nilikuwa sikosi uwanja wa maji maji kuangalia mpira wa ligi kuu, kila inapokuja timu yoyote kucheza pale. Kilikuwa ni kipindi maji jami iko moto sana, simba na yanga zilikuwa ni kawaida kufungwa pale.

Kwa kuwa wasimamizi pale getini ni asikari, walikuwa wananipitisha bila malipo. Maisha yangu yote niliyoishi Songea sikuwahi kulipa kiingilio kwa tukio linalo lindwa na polisi pale maji maji.

Nilikuwa mtundu wa kimya kimya sana, nilipenda kujifunza vitu hasa ufundi. Nakumbuka kuna siku nilijifanya fundi nikafungua redio ndogo, kaka alikuwa anapenda kusikiliza mpira RTD. Nikashindwa kuifunga baada ya vitu kubaki, ikabidi nivitupe kupoteza ushahidi (i was a kid). Aliporudi kakuta redio haiongei , kesho yake akaipeleka kwa fundi.

Fundi akanisagia 'kunguni', akamwambia kuna vitu havipo, vikipatika itaongea , nikapewa kazi ya kuvitafuta mpaka jioni akirudi avikute.

Sikufanikiwa kuviona, ikabidi nisubiri kipigo akirudi, jioni aliporudi nikamwambia sijaviona. Alikuwa na kawaida akitaka kunipiga kama ameva kombat anavua shati anabaki na suruali na buti.

Siku hiyo nilifungiwa chumbani kipigo kikaanza, nilichezea mikanda na mateke ya mbavuni mpaka askari wenzake walikuja dirishani, wakaanza kumtisha kuwa wata mshitaki kwa mkubwa wao. Ndio ikawa pona pona yangu. Hiyo nyumba kulikuwa na wapangaji askari watatu.

Kesho yake nilipandisha homa kali, kutokana na kile kipigo cha jana yake. kufika jioni nikazidiwa ikabidi nipelekwe 'mzena dispensary'. Kabla ya kwenda nilipigwa biti kuwa ole wangu niseme nimepigwa.

Kaka alishauriwa na wenzake akaombe gari ya polisi anipele hospitali ya peramiho, ni baada ya hali yangu kuzidi kuwa mbaya. Mwanzo alipata ugumu maana aliogopa chanzo cha ugonjwa wangu kujulikana.

Kesho yake nikawa na hali mbaya zaidi, ikabidi wale wenzake wakaombe gari, jioni hiyo nikapelekwa peramiho, nikatundikiwa drip 3 na nili lazwa kwa siku 5.

Baada ya kupata nafuu nikaruhusiwa kurudi nyumbani, kaka alikuwa mnyonge sana baada ya lile tukio, na vipigo vilipungua sana.

Aliambiwa nimeumia mbavu, ilibaki kidogo moja ivunjike, kwa mateke ya my brother (RIP).

Maisha yaliendelea hatimaye nilipofika darasa la 3, yaani baada ya mwaka mmoja. Tulirudi likizo nyumbani, nikiwa likizo nilimwambia mama kuhusu vipigo ninavyopata. Mama alihuzunika sana, alimsema sana kaka kwa ukatili ule alionifanyia, mama aliamua nisirudi na kaka.

Nikahamishiwa shule kutoka misufini Songea, kwenda kitete Iringa kwa baba…

*******
View attachment 2552846View attachment 2552847View attachment 2552848View attachment 2552850View attachment 2552851
Kweli braza alikua noumaa kuharibu redio tu Ndio kichapo mpaka kutaka vunja mbavu mtu dahhh!!
 
Part Three: Nanusurika kuuwawa.

1983 - 1989

Nikaanza maisha mapya ya kijijini tena, kijiji kilikua kidogo sana. Nilikutana na changamoto nyingine pale kitete, hakukua na mashine ya kusaga, ilitubidi kwenda mgororo kwa gari moshi kusaga, na kununua mahitaji kama vile mafuta ya taa.

Nilipelekwa shule ya msingi kitete kuendelea na darasa la 3, nilisoma hapo mwaka mmoja tu.

Kutokana na kuwa kijiji ni kidogo, nikakosa wenzangu wa kucheza nao, (hapo kambini wototo wa rika langu walikuwa wachache, kijiji kilikuwa mbali na kambi) nilianza kwenda kutembea makambako kila jumamosi.

Ukiwa mgeni pale makambako , ukinunua chai, wanakupozea kabisa, maana kuna baridi kiasi kwamba wewe mgeni huwezi sikia moto wa chai, baadae mdomo utakapo babuka ndio utajua uliungua.

Kule makambako kulikuwa na mjomba, nae ni mfanyakazi wa TAZARA kituo cha makambako.
……..
Kwenda kila jumamosi ilikuwa rahisi kwa sababu familia za wafanyakazi wote wa TAZARA walikuwa na 'free pass' ya kupanda gari moshi kwenda kokote inapofika TAZARA.

Yaani unaweza kwenda Dar mpaka Mbeya bure tu. Nilitumia hiyo nafasi kushinda kwenye gari moshi, nachotakiwa kujua ni ratiba tu za gari moshi.

Nilipendelea sana kupanda schoma (schoema-lokomotiven), hizi hutumiwa na wafanyakazi kukagua reli na kubebea vifaa vya ufundi.

Zinakimbia sana, breki za haraka kama gari. Natoka asubuhi na schoma /gari moshi ya abiria inayoenda Zambia nashukia makambako, jioni narudi na gari moshi ya mizigo 'goods' tukawa tunaita 'gusi' naenda tu kwa station master na mwambia mimi ni mtoto wa mfanyakazi flani, naomba usafiri wa kwenda sehemu flani, basi ananipatia.

Siku moja nilichukuliwa na marafiki zangu kwenda kwenye kijiji cha jirani, wao walikuwa wenyeji. Pale kitete ilikuwa ni kambi ya wafanyakazi na kulikuwa na station ila wenyeji walikuwa wanakaa pembeni kidogo. Tulienda uelekeo wa mrimba kwa miguu.

Njiani tunapita kwenye mahandaki ambayo yana giza sana, mimi kutokana na ugeni wangu nilikuwa nabeba tochi kila tukienda huko. Kunakua na giza kiasi kwamba unaweza kupishana na mtu bila kujua, labda uwe na taa, au mkutane upande mmoja (mgongane).

Uzuri ni kua kila handaki lina vyumba vidogo vidogo vingi, just in case gari moshi likikukuta humo unaingia kwenye chumba, usipoingia linakusaga maana ni njia ni nyembamba.

Hakuna nyoka kwenye handaki na wala hawasubutu kuingia kwa sababu ya mafuta yanayomwagwa 'diesel' au oil.

Kuna handaki moja refu sana linaitwa 'handaki 14', niliwahi kusimuliwa kuwa kipindi Nyerere alipokuwa anazindua hiyo reli, alikataa kupita kwenye hilo handaki ikabidi apitishwe juu ya mlima kwa helicopter. Sababu ni refu sana, kwa wasiojua handaki wanachimba mlima kutengeneza njia ya gari moshi.

Siku hiyo nimeenda na rafiki zangu kutembea uko handaki 14, ilikuwa ni kipindi cha kiangazi. Kutokana na umbali na jua kali, niliamua kurudia njiani baada ya kuchoka, wale wenzangu walikuwa wametumwa huko kijijini, mimi niliunga tu tera.

Nikiwa narudi nilipita kwenye mahandaki madogo madogo, giza likiwa limetanda ingawa nje jua kali.

Nikiwa nimekaribi sehemu ambapo wakati tunapita tuliwakuta mafundi wakiendelea na kazi, nilianza kusikia michakato ya kitu kinakanyaga majani makavu. Nikisimama na kugeuka kuangalia sioni kitu wala kusikia michakato, nikitembea naisikia.

Mazingira ya hapo yalikuwa mimi natembea kwenye mataruma ya reli nje tu ya handaki, (kwa vile kutengeneza mahandaki wanachimba mlima) yale mataruma yalikuwa chini kuna kingo za udongo kila upande na juu ya mlima ndio kuna nyasi. Kwa hiyo ile michakato ilikuwa inashuka kutoka mlimani kuja chini niliko,mkono wangu wa kulia.

Wale mafundi walikuwa sehemu tambalale,lakini kuna kona, walikiona kile kilichokuwa kinanifata bila mimi kukiona . Ikawabidi wapande kilimani ili waone kile kitu kinawinda nini pale.

Hilo eneo kitete liko jirani na mbuga ya wanyama ya seluu. Wakiwa hapo mlimani waliniona mimi niko pale chini natembea huku nikigeuka mara kwa mara, umbali wangu na wao ulikuwa kama mita 70 tu.

Wakaanza kupiga kelele huku wakikimbilia huku niliko, kelele zao zikanishtua, ile nageuka nyuma ndio nikakiona kilichokuwa kinaniwinda. Alikuwa ni simba dume, alikuwa ananinyatia nikisimama anatulia , kwa vile majani ni marefu sana na makavu sikuwa nimemuona kabla.

Nilianza kukimbia kuwafata wale mafundi, pembeni yangu mkono wa kulia yule simba nae aliongeza spidi sasa akaacha kunyata maana nimeanza mbio. Akawa anashuka mlima ili aniwahi kwa mbele, tulikuwa sambamba ila mimi niko chini yeye juu ya mlima.

Bahati ilikuwa upande wangu maana wale mafundi walipiga risasi kule mlimani aliko simba ikabidi abadili uelekeo. Nikiwa kama mita 15 kuwafikia wale mafundi nilianguka nikapoteza fahamu kutokana na ile hofu.

Nilikuja kuzinduka mida ya jioni kama saa 10 maana muda ule wa tukio ilikuwa saa 6 mchana . Baada ya kupata chakula wafanyakazi wenzake baba walikuja kunipa pole kwa mkasa ule. Sikuwa na haja ya kueleze kitu chochote kwa kuwa wale mafundi walieleza kuhusu lile tukio zima.

Kumbe ilikuwa ni kawaida kipindi cha kiangazi, wakati wa mavuno kijijini, wanyama mbali mbali walikuwa wanaingia vijijini kutafuta chakula mashambani na maji. Mimi na ugeni wangu sikuwa nafahamu hilo.

Wafanyakazi wa TAZARA walikuwa na magobole kwa ajili ya usalama wao wawapo porini kwenye kazi zao.

Siku moja usiku mzee wangu alinionyesha simba waliokuja pale kijijini. Walikuwa wawili, macho yao yalikuwa yanawaka kama tochi usiku, wale simba walikuwa kwenye kilima wanashuka. Watu pale kambini wakapiga risasi hewani wale simba wakakimbia.
…………..

Ndani ya A city….
Baada ya tukio lile mama alipopata habari alimwambia baba nirudi nyumbani maana kule sio salama kwangu. Mzee wangu hakupinga maana na yeye alipata uhamisho kipindi hicho, kwenda makao mkuu pale TAZARA Dar es Salaam, kule kitete alikuwa station master. Alipanda cheo akahamishwa .

Mzee aliamua mama ahame kule kijiji ''X'' ahamie mjini afanye biahara. Alitaka mama amfate Dar lakini Mama alichagua kuhamia mkoa wa Arusha kwa kuwa alikuwa amekulia huko.Anaoufahamu vizuri kuliko Dar.

Pia ingekuwa rahisi kurudi nyumbani kuangalia maendeleo ya mashamba maana sio mbali kwenda ''X'' kulinganisha na Dar.

Mzee aliuza ng'ombe wote na mbuzi, alinunua nyumba eneo la Sakina Arusha.

Pia Alinunua shamba la migomba lililokuwa jirani na hiyo nyumba, akajenga nyumba za wapangaji.

Mama hakutaka kukaa kwenye nyumba iliyonunuliwa maana ilikuwa ya slope. Mzee akaibomoa na kujenga nyumba nyingine kubwa na nzuri pale pale.

Mimi nilihamia Arusha kwa mama, baada ya baba kuondoka kitete, nilipata shule ya msingi 'Sanawari' nilisoma hapo darasa la 4 mpaka nikamalizia hapo elimu ya msingi mwaka 1989.
……….

Mama alifungua biashara zake akawa anafanya, alikuwa na duka la nguo na restaurant maeneo ya mjini kati.

Matokeo yalipotoka nilipangiwa shule ya Songea boys,(miaka ile Sera ya Nyerere ya kutoa wanafunzi mikoa ya kaskazini kwenda kusoma
mikoa ya kusini, wa kusini anaenda kanda ya ziwa nk ilikuwa bado inafanya kazi) 'narudi tena kwa mjeda',

Mama aliwasiliana na kaka, alimweleza kuhusu mimi kupangiwa shule huko aliko . Mama alimuomba kaka asije kufanya kama yale ya nyuma , kaka yangu Edward alimhakikishia mama kutonifanyia ukatili wowote ule, alisema kipindi kile ni ile hali ya kutoka depo ilisababisha ila kwa sasa amekuwa.

**********

Next Jioni.
Table.jpg
Train%20inapita%20kwenye%20handaki.jpg
schoema-lokomotiven-schmalspurlokomotiven-03.jpg
Simba%20dume.jpg
Tazara_GE_U30C_Mlimba.jpeg.jpg
 
Back
Top Bottom