Mkataba wa Dubai na Tanzania kuhalalisha Kambi 88 za Masetla wa Kiarabu nchini Tanzania?

Yani Faiza na the boss wako hoi muda huu kwa nondo za mtoa mada
Duh kwa hiyo nyie furaha yenu ni kuwaweka watu hoi na huku wakiendelea tu na msimamo wao.
Ndo mana nasema kwa tz hii hatuna wapambanaji. Tuna watu wanaoridhika kabisa kuwa eti tumewapiga nondo
 
Jibu lako hili chini👇👇
Mikataba ya huko ni sawa na huu wetu? Huu wetu usiokuwa na ukomo ni halali mtu akisema 'masetla' kwakuwa haawana ukomo wa kuwepo ni permanent.
 
Eti hakiondoki kitu hapa. Utadhani kweli kumbe ni nyuma ya keyboard tu
 
Leo umeugusa sana moyo wangu.
Dijaeahi kukuunga mkono katika bandiko lako kama leo.

Uishi mama
Ibarikiwe sana.

Tuungane kukemea huu uhayaeani
Jazaneni tu maujinga na kujifariji, wenye bandari yao washaiuza na wako kimya...
 
Hii ndo itasaidia wasichukue bandari?
 
Kilichosainiwa sio mkataba ni azimio la makubaliano ya kuja kufanya biashara. Hatua inayofuata sasa ndio kusaini mikataba yenyewe.

Huu ndio wakati wa kuwa makini katika kutanguliza maslahi ya Tanzania yetu kibiashara. Wakati wa kusaini hizo HGA ni muda wa kwenda kwa umakini kipengele kwa kipengele.

Tukumbuke kuwa IGA haina nguvu kwani haiwezi ikawekwa kila masharti yetu kama nchi, ni katika hii mikataba ya kibiashara ndio tunakuwa na sauti ya kipi kiandikwe na kipi kisiandikwe.

Watanzania ni wajuaji mno, na kila mtu anakuja na upotoshaji anaojisikia kuufanya.
 
Duh!
 
Shida yenu ni waarabu mengine ni kutafuta kwa kujifichia tu

Siku anaachia madaraka huyu mama watamlilia sana na kumkumbuka kwa mazuri, hawa wanatakiwa kutawaliwa na dikteta asie na huruma na wananchi wake, muda utaongea wee subiri tu
 
Shida yenu ni waarabu mengine ni kutafuta kwa kujifichia tu
Shida yao pia ni urais wa Samia, umekuwa unawauma sana tangu JPM alipofariki dunia, hakuweza hata kuwaza kwamba Magufuli angeaga dunia kipindi kile wakawa wanajitanua huko kwenye nafasi zao za juu serikalini.

Kifo chake kikawapiga butwaa wakabakia wamechanganyikiwa hawajui washike lipi waache lipi.
 
JF ondoeni uzushi huu wa kipuuzi, au nanyi mnafaidika na upuuzi huu? Kumbukeni tuna nchi moja na mauaji ya kimbari ya Rwanda yalianza na chuki km hizi na uwongo mwingi uliopaliliwa na vyombo vya habari. Tambueni wajibu wenu km mhimili wa nne wa dola
Wewe nazani utakuwa ni ndugu yake nape mpo vizuri sana kupinga bila hoja
 
Kuwa na hoja na kuandika uongo ni sawa?
Kambi za masetla? Dpworld wako Rwanda ..kuna kambi ya masetla?
Dpworld wako Uk na German kote huko kuna kambi za masetla? seriously??

Unajua terms walizoingia rwanda na dp?
 
Inajirudia historia.

Zamani wakoloni walifika kwa kubahatisha wakitumia majahazi na merikebu katika pwani za nchi geni na kuwalaghai watu walioowakuta.

Leo hii sisi wenyewe tunajipeleka hadi kwao kuwalilia waje waokoe jahazi kuwa tumishindwa kuendesha kampuni, shirika la umma na kuwa wizara husika haina maono ya kuwezesha waTanzania waendeshe mfano bandari n.k

Ama kweli historia inajurudia sisi kukimbilia nchi za kaskazini na mashariki ya kati na Mashariki ya mbali kuwa wenyewe hatujiwezi .


Ghengis Khan wa Mongol, waTuruki, WaDachi na waAzetc wa kale walisema ogopa sana wageni wanaoonekana wakija kwenu huku wakiwa wamepanda farasi au wamefika pwani kwa vyombo kama majahazi au merikebu.

Watu hawa wageni wa kutoka mbali hadi kuifunga safari hiyo ujue wana kitu wanakitafuta maana hawawezi kukatiza nyika, majangwa, milima, mabonde au bahari kuu za Hindi, Atlantic, Pacific kwa ajili ya matembezi huku wameacha familia, wake, watoto, wazazi na kwenda nchi ngeni




Merikebu ya kutoka Portugal iliyotumika kukusanya taarifa zilizopelekea kutawala makoloni nchi za mbali


A 15th century Portuguese caravel. it had three masts and a lateen or triangular sail which allowed the caravel to sail against the wind Conquerors: How Portugal Forged the First Global Empire by Roger Crowley (2015)

Sisi tunapokea bila tahadhari yoyote na kuwahesabu kuwa hawa ni wadau wa maendeleo kuwezesha tujikwamue tulipo kwana. Tunaongozwa na kauli za niamini, nina nia njema nimekuja kuwakomboa kutoka katika kila changamoto ya kijamii kuanzia muachane na miungu yenu ya mizuka, zolelanga tuwachimbie visima vya maji, elimu isiyoendana na uwezo wa kuwakwamua mlipo kwama hadi mpige hatua.

Kifupi tume sarenda mioyo, akili na historia yetu na kusahau kwa makusudi mazima kuwa tuliweza kupambana na mazingira yetu mfano tukichimba visima vya maji vijijini kwa ujuzi tuliorithi kutoka kwa mababu bila kutegemea mfadhili wa kutoka nje, tulilima, kutunza mazingira na kujichimbia mifereji ya kumwagilia mashamba n.k n.k Leo hii hatujiwezi kabisa tumekuwa na ulemavu usio wa kuzaliwa wala ajali ya kuangukiwa na jabali n.k
 

Chuki na roho mbaya itawamaliza enyi mliojawa chuki vifuani mwenu dhidi ya waarabu na uislamu kwa ujumla, kisa aliepewa bandari ni mwarabu na ni muislamu . Mbona wazungu wenu, wachina na wahindi wenu wamemiliki migodi n.k na mpo kimya wala kutia neno!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…