Mke mwenye miaka 15 aumizwa vibaya na mume kisa kumwaga dawa ya mbuzi

Mke mwenye miaka 15 aumizwa vibaya na mume kisa kumwaga dawa ya mbuzi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
FdQA9t6XoAAKYvA.jpg

Mesoni Kashiro (15) Mkazi wa kijiji cha Gelailumbwa, kata ya Gelailumbwa, tarafa ya Ketumbeine wilayani Longido mkoani Arusha, ameshambuliwa na mume wake Namendea Lesiria kwa kushirikiana na rafiki yake ambaye jina halijafahamika kwa kosa la kumwaga dawa ya mfugo aina ya mbuzi.

Ofisa Ustawi wa Jamii wilayani hapa, Atunagile Chisunga akieleza kuwa watuhumiwa wapo kituo cha polisi Longido na hapo kesho wanatarajia kufikishwa mahakamani huku akisistiza mama huyo yupo kituo cha afya Longido akiendelea kupatiwa matibabu zaidi.

"Huu ni ukatili kabisa kwanza ameolewa akiwa na umri mdogo, wamempiga wakiwa wamemfunga kamba na kumtundika kwenye miti," alidai Chisunga.

Chanzo: Dira

================

Namendea Lesiria, Mkazi wa Kijiji cha Gelailumbwa, Tarafa ya Ketumbeine Wilayani Longido Mkoani Arusha anatuhumiwa kwa kumshambulia mkewe mwenye umri wa miaka 15 na kumsababishia majeraha makubwa.

Namendea anadaiwa kutenda kosa hilo kwa kushirikiana na rafiki yake chanzo kikitajwa ni binti huyo kumwaga dawa ya mifugo (mbuzi).

Ofisa Ustawi wa Jamii wa Longido, Atunagile Chisunga amesema “Watuhumiwa watapandishwa Mahakamani Septemba 23, 2022, pia mama wa binti tunamshikilia kwa kumkeketa mwathirika.”
 
Aseee Pole Sana mtoto,hii haikubaliki.

Sheria za Mtoto zinamlinda vizuri na naamini atawekwa mikono salama.
 
Aseee Pole Sana mtoto,hii haikubaliki.
Sheria za Mtoto zinamlinda vizuri na naamini atawekwa mikono salama.
...Hao Wakanyee TU Debe Kwa Ukatili Huu,,,!![emoji35][emoji35][emoji35]
 
Hao majamaa hawachomoki hapo, japo mmoja jina lake halifahamiki licha ya kuingizwa kwenye detention book.Mtoto wa miaka 15,unamfanyaje awe mama?

Ukute hata hakujua kama ni dawa ya mbuzi,maana ni mtoto huyo.

Miaka 15 hata ladha hamna, ukiangalia hata umbo la mvuto, hana.

Sheria ichukue mkondo wake, na jina la huyo ambaye halijafahamika, japo kazuiliwa polisi,liwekwe bayana,nguvu ya ya haki za watoto, watu wa ukatili wa kijinsia, na akina mama,uone watakavyodili nae.

Tena nimeona kwenye group la WhatsApp, mbunge ndiye kaipost, lazima wale mvua.
 
Back
Top Bottom