Mke wako wako asikuzidi jina, nyumba yako itambulike kwa baba au mzee fulani na sio kwa mama au bibi fulani

Kuna watu mnapata shida sana na vitu vidogo dogo tu.Mnapenda kukuza jambo..mm kwangu panatambulika kwa mama masanja maana kuna frem pale na mke wangu ana duka pale kwa hiyo wateja mm hata hawanifaham wamezoea jina la mke wangu mpaka boda boda ukiulizia jina langu ni shida ila ulizia hata vitue vitatu nyuma naenda kwa mama masanja fasta tu unapelekwa bila hata kuelekeza.Kuna vitu mnavipa umuhim lakini ni vidogo sana.Nyumba nyingi mtaani zinatambulika kwa majina ya wanawake maana wao ndo washinda nyumbani.
 

Zîpo Nyumba mamilioni Kwa mamilioni Wanaume hawaishi nyumbani na hawashindi majumbani na bado zinatambulika Kwa Majina Yao.

Kutokushinda nyumbani siô kigezo cha wewe Nyumba yako isijulikane Kwa Jina Lako.

Watu wàpo nje ya nchi Miaka na Miaka na bado Majina Yao yanaishi kwèñye Nyumba wanazozijenga.
 
Kunatofauti kubwa sana ya aina ya maisha kutoka eneo moja hadi lingine

Huku kwetu uswahili karibu nyumba zote zinajulikana kwa mama fulani

Huku kwetu uswahili wanaume wote asubuhi na mapema karibu wote tunatoka kwenda kwenye mihangaiko yetu nje ya mitaa yetu na tunarudi usiku.
Majumbani wanabaki wanawake zetu tu na watoto..... watauziana vitumbua na maandazi, watasutana na kuchambana, wanavikoba vyao, wanaombana chumvi na unga, wanakopeshana na kuazimana vijora nk nk..... sasa wewe baba Jijo anakujua nani?
Hapo utakuta hapo mtaani wewe hujui lakini mkeo Mama Joji ni maarufu balaa kwa kukopa halafu mtata kulipa 😂😂
 
Aisee
Jina huja automatic
Huwezi kuforce
Kuna watu wana nyotaa kaliii huwezi shindana nao.
Akifika mtaani tu jina lake linawaka Huwezi control watu utahangaika sana

Kama Mkeo anakuzidi Ñyota Jua wewe Umeolewa na yeye ndiye kichwa cha Nyumba.
Úkiwa kichwa cha Nyumba automatically Nyumba yako lazima ibebe jina Lako
 
Hapana wanaume hatushindi manyumbani na hatupigi umbeya.

Kwani hao ambao majina Yao yanabeba Nyumba zào wanashindwa nyumbani?

Kûna Watu wanaishi Mjini na wamejenga Nyumba Huko kijijini Kwao wanaishi ndugu zào au Watu back na bado Nyumba inaitwa Kwa Mzee Fulani. Tenà Wengine hawajawahi kumwona na hawamjui
 

Hata Sasa wanawake wanabebwa Majina ya waume zào wengi tuu lakini lazima huyo Mwanaume awe Mwanaume
 
Na hasa kama unatokea kanda maalum
 
Hahahah bro, maisha sio marahisi hivyo na sio magumu pia namna hiyo. Bro wangu na mkewe walipojenga huko Bunju wameweka na shule ya watoto hapo hapo na mkewe kwa sababu ana taaluma ya ualimu ndiye mkuu wa shule na ndiye anafahamika zaidi mahali hapo. Unavijua hivi vi daycare vya mtaani, ilianza bila jina, madam Winnie ni maarufu sana mahali pale.
Kwa faida ya kibiashara, familia na n.k bro ameendelea kuwa anonymous na maisha yanaendelea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…