Mke wangu amekosa choo kwa siku saba, nisaidieni

Mke wangu amekosa choo kwa siku saba, nisaidieni

Habari za usiku huu wana JF, naomba msaada wa haraka, mimi na mke wangu tupo mbali kidogo, leo ameniambia hajapata choo kwa siku saba, nimechanganyikiwa hapa sijui nifanyeje na tumbo linamuuma hatari
Nilikua nashida hii imenitesa MIAKA 2 maisha yangu yalikua ni kutumia bisacodl ilikua bila kutumia dawa bas siendi huko toilet,ilifika mahali nazo zikadunda, hapa ilibd niende hospital namshukuru yule dactar kwasababu hakunipima Chochote,akaniambia niludi nyumbani mimi ni mzima, akaniambia niseme mimi ni mzima kuanzia Sasa,
Toka mwezi wa 9 mwakajana napata choo kawaida,ila baada ya kubadlsha style ya maisha + vyakula na Kuna baadhi ya vyakula nimeacha kula kabisa

Dactar aliniambia hivi

Nile ugali wa dona mlaini sana,
Mboga za majani zizidi ugali, na maharage,
Nakunywa maziwa fresh au mtindi kilasiku,
katika Milo yangu mi 3 kwa siku m,Moja uwe matunda pekee hasa parachichi na papai,
Nisile wali,nisile vyakula vya ngano kama chapati,maandazi,tambi au chochote kinachohusu ngano,

Nakunywa maji mengi,

Kwahyo sasahvi napata choo kawaida,bila kutumia dawa tena
 
Habari za usiku huu wana JF, naomba msaada wa haraka, mimi na mke wangu tupo mbali kidogo, leo ameniambia hajapata choo kwa siku saba, nimechanganyikiwa hapa sijui nifanyeje na tumbo linamuuma hatari
Ale mapapai kila mara utakuja kunishukuru. Ale papain nzima kwa mlo mmoja. Halafu aache kula vyakula vikavu kama vile mikate, supergate mihogo n.k
 
Back
Top Bottom