Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

"Baadhi ya wanawake wanaroho mbayaa sana hapa kitaa hapa kuna jamaaa aliachana na mkewe akachukua single maza moja hivi mshikaji nae ana mtoto mmoja na huyu mtoto ndo mama yake na huyu mwamba walipambana wakajenga mji.Single maza kaja na mwanae lakini cha ajabu alikua anamtesa mtoto wa mwanaume ile mbaya ila mwanae anaishi nae poa tu."👆👆
Umeenda madarasa haya haya ya Tanzania au ni nje ya nchi?
Nimesomea ujinga 🤣🤣
 
Huyo mwanamke ana roho mbaya sana aisee ila ndivyo wanawake wengi walivo ukiona nduguzako hawapendi hata kuja kukusalimia ila ndugu wa mkeo wamejaa hapo kwako na wanakaa ujue umeoa shetani
 
Hilo ndio chaguo lako na ushazaa nae watoto wawili utakapomuacha fikiria mustakabali mzima wa watoto wako na wewe , Kama unaweza mtafutie shule nzuri ya boarding akakae awe anakuja nyumbani likizo tu. Na wewe uanze kuweka mipaka Kwa ndugu zake
Huyo hafai iko siku atamshindilia bisu mana anaroho kama jambazi...anampigia mtoto mdogo tofali hiyo n8 roho mbaya aliyonayo mtu mzima habadiliki
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
Mwanamke asiyeijali familia yako hafai hata kidogo.
Siku hata wewe usipokuwa na uwezo kifedha/ kumuhudumia basi jua utatendewa unyama pia
 
Yes, hii ndio njia nzuri na sahihi zaidi ya ku-deal na huyo mwanamke shetani.
Awe makini Sana huyo mume, siku moja atakuja kufanyiwa uovu wa namna hii hii au zaidi ya huo. Huyo Mwanamke ni adui mkubwa sana kwa usalama wa huyo mume na ndugu zake, akiendelea kuwa naye ipo siku moja maadui wa nje pia wataweza kumtumia huyo mwanamke ili amuangamize na kumuua huyo mume. Kulikuwa na kisa kimoja Cha ukatili wa namna hii kilichomhusu jamaa mmoja alikuwa anaitwa Oscar (Kama sijakosea Jina), nasikia alikuwa Mhasibu katika Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), naye alikuwa anaishi na mwanamke shetani wa namna hiyo hiyo. Mwisho wa siku nasikia huyo mwanamke wake alishirikiana na "wauaji" wa nje na kufanikiwa kumuua mume wake huyo, inasikitisha Sana kusikia kwamba yule jamaa aliuawa kikatili Sana, inasikitisha.
Naamini Watu wa HESLB wapo humu mtandaoni, wanaweza wakatupatia shuhuda nzuri zaidi kuhusu mkasa mzima wa kuuawa kikatili kwa huyo mfanyakazi mwenzao aitwaye Osca. Nafikiri watakuwa wanakumbuka vizuri tukio Hilo.

Kwa hiyo huyo bwana awe makini sana na huyo mke wake katili, siku zake naye zinahesabika.
Binafsi naamini huyo mwanamke atakuwa ameshafanya matukio mengi tu yanayofanana na hili, huyo anaonekana ana mkono wa kupiga na mdomo mchafu... yes, mtu mgomvi siku zote lazima awe na mtu wa matusi matusi.

Na hii tabia mbovu jamaa mwenyewe ndio atakuwa ameilea kwa kupuuza zile redfrags mwanzoni mwa mahusiano yao... yes, mwanamke mchoyo na mbnafsi asiyependa ndugu wa mume huwa anaonekana tu tangu awali.

Kitakachofuata endapo kma huyu jamaa ataendelea kubaki na huyo mwanamke ni dharau za wazi wazi na siku ikitokea akapitia tu changamoto zozote za kiuchumi kiasi cha kushindwa kutoa mahitaji hapo nyumbani na kumsomeshea hao ndugu wa mkewe, basi utakuwa ndio mwisho wa hiyo ndoa yao.

Kuhusu hilo tukio la muhasibu wa HESLB kwakweli inasikitisha, vijana wengi wanaangamia kutokana na machaguzi mabovu ya mke.... na bahati mbaya sana hata wakija kugundua mbeleni huyo mke waliyenaye hafai, wao wanaamua kukaza roho tu na kuendelea nae na matukio yake ndio tunakuja kuskia haya.
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
Nina kanuni za kusikiliza pande mbili linapokuja suala la migogoro ya wanandoa, lakini kwa kesi hii namna ilivyo, ninasikiliza upande mmoja tu na kushauri.

Huyo mamsap wako ana roho ya kuku jike ama ng'ombe ya kupenda watoto wake tu, ana tabia ya kinyama.

Kama umeshaelewa tabia yake halisi, basi na wewe mme badilika namna ya kuchunga na kuilinda familia yako.

Ingawa unashinda kazini, jipe jukumu la ufuatiliaji wa karibu wa kila siku usio na kikomo.

Maelezo yako yamejitosheleza, huyo mtoto ni wako 100% hauna pa kumpeleka, kumuondoa hapo nyumbani kwako kwa ajili ya mkeo ni kukikimbia kivuli chako ama kutishwa na kinyago ulicho kifinyanga kwa mikono yako.

Nimeona wadau wakishauri utafute pa kumpeleka ama boarding school!

Kumpeleka boarding ni mipango, lakini aende kwa heri na si kwa shinikizo la ukatili wa mke.
Mume utakuwa umeshindwa kuyatumia madaraka yako kama kichwa cha familia ipasavyo.

Kwa ufupi toa maelekezo kwa mkeo na akuelewe namna ya kuwalea watoto bila chuki.

Na pia aelewe kwamba, mtoto anayepata hifadhi ya malezi yenu hapo nyumbani, si mtu tegemezi wa muda wote maishani mwenu, awe wenu wa kuzaa ama yeyote mnayemlea ni wa muda mfupi, baadaye atajitegemea na maisha yake, hivyo kaeni nao kwa upendo, maana mtapozeeka nao watawasaidia.

Maana ya Mungu ni mengi, je ukipoteza maisha leo, huyo mwanamke anaweza kuilea kwa amani familia utakayokuwa umemwachia?

Kama hataweza kukuelewa na kukutii, basi atakuwa ni sikio la kufa lisilosikia dawa.
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
mpeleke kituo cha watoto yatima ! huyo mkeo n shetan
 
Mwanaume unatakiwa kua na authority kwako, mi siwezi kukaa na mwanamke eti kitu kidogo anatishia aende kwao, ungemuacha aende huko na usimfate mpaka arudi mwenyewe, la sivyo ashajua udhaifu wako, Kila mkigombana atakua anatishia kwenda kwao


Kuhusu huyo mtoto, kama Kuna ndugu mwingine anaweza kukaa nae basi fanya mpango huo wewe ugharamikie Kila kitu kwa makubaliano kabisa, kuanzia mavazi,elimu,chakula,matibabu etc... Mtoto kukaa sehemu anaponyanyaswa huathirika physiological.... Mnamletea shida tu za badae huyo mtoto



Hilo lishemeji ulilitoa wapi?
Nimeipenda hii
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
Huyo mkeo anaroho mbaya,Huyo ni kama mwanao.wengine kama Mimi nimelewa na mke wa mjomba hadi nina familia kwa Sasa na watoto wa huyo mjomba niliwalipia ada ya high school!Kaa nae mkeo Aacha roho mbaya .
 
Kama mwanamke hawezi kukaa na ndugu zako kwa Amani Huyo sio mke ullingia Choo cha kike, Mimi mwaka flan nilimfanyia mdogo wangu sherehe aliingia kumi Bora kitaifa kidato cha sita.

Mchumba wangu akanijia juu natumia hela vibaya , kwa kosa hilo nilimfuta kabisa na kuahirisha mipango yote. Kwangu Mimi Bora kosa lolote ila sio kushindwa kujali ndugu zangu
Yes, Ulifanya uamuzi wa maana sana family is everything na usiruhusu mpuuzi yeyote anayeonesha kutojali kuhusu familia yako adictate maisha yako.

Huyo mchumba wako si ajabu wakati anakambia hivyo siku za nyuma yake alikuomba umpe hela akachangie harusi za mashoga zake kwa kisingizio cha kwamba na wao wangekuja kuwachangia kwenye harusi yenu.
 
Muache. Mtu anayeweza kumchukia mtoto wa miaka minane sio mtu. Mrudishetu kwao kabla hajamtia kilema au zaidi huyo malaika. Inabidi uwaulize vizuri watoto wenzake unaokaa nao na uwaambie kabisa kukalia kimya ukatili na unyanyasaji hauna sehemu nyumbani kwako. Leo mke wako. Kesho hausgeli.

Amandla..
Nashauri jamaa ampige mkewe kwa tofali mguuni kama mtoto alivyofanyiwa... Ili mkewe ajue uchungu wa mfupa wa mguu kusogea na kuvalishwa P.O.P.. Akili ya huyo mwanamke itakaa sawa na kuheshimu watoto wa wanawake wengine.
 
Nashauri jamaa ampige mkewe kwa tofali mguuni kama mtoto alivyofanyiwa... Ili mkewe ajue uchungu wa mfupa wa mguu kusogea na kuvalishwa P.O.P.. Akili ya huyo mwanamke itakaa sawa na kuheshimu watoto wa wanawake wengine.
Akiondoka atampgiga sumu
 
Nakubaliana na wale wote ambao wamasema huyo umuhamishe hapo,tena fanya fasta,,hali ilipo fikia kuna makubwa yanakuja,usije kusema ningejua

Hapo ni hayo machache uliyoona na kusikia,je ni mangapi hujasikia?

Hapo huyo mkeo hata umwambie vipi hatobadilika,litakuja kichwani kwake,huyo mtoto na yeye nani ni bora kwako?

Natamani na ninakuomba mhamishe huyo malaika wa Mungu,mhudumie sehemu nyingine ambayo atapendwa na kuthaminiwa,na hakikisha unampeleka kwa mtu sahihi

Nimeguswa sana,je usingemsikia usiku huo unadhan ingekuwaje kwa huyo mtoto.

Nawapenda watoto sana,kwahiyo huwa nahumizwa na habar kama hizi

Bro tafadhali muhamishe huyo mtoto
 
Mkeo ana roho mbaya sana. Alivyotishia kuondoka ungemwambia nenda. Hapo siku ukimuacha huyo mtoto na huyo mkeo atampiga mpaka amvunje mkono.

Usikute dada yako ndio alikulea mpaka kufika hapo. Mpe heshima kwa kumlea mtoto wake sawasawa na watoto wako.
Hii ya kutishia imenikumbusha mshikaji wangu mmoja,mke mwingine wa baba yake alitishia kuondoka,baba yake akamwambia nakuwekea mafuta kwenye gari kama unataka kuondoka,mke kwani aliondoka? Alijua mwamba hataki ujinga
 
Back
Top Bottom