Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

Mke wangu ananilazimisha nimuombe msamaha mbele ya Kanisa

wanawake kama hao ndio wanatakiwa sasa,unahofia kudhalilishwa,wewe ulivyokua unachepuka hukua unamdhalilisha mkeo?
 
Mkuu wewe ni mpole sana man up tafadhali.
Halafu mbona mkeo ni mkoloni sana? Anataka kuonekana yeye kuwa yuko juu zaidi yako, na dini haisemi hivyo hata msamaha kwenye maandiko hauko hivyo, hapo changanya na za kwako.

Sasa naweza kuwaelewa wanaume kwa nini wakitukosea makosa wanabadilika wanakuwa wakali ni kwa sababu ya wanawake kama mkeo.

Upo sahihi boss we tia mgomo mambo ua kurekodiana tutakuona whatsapp unazagaa ovyo umepiga goti unaomba msamaha kanisa.
Mbona mnashidwa mtetea mwanamke mwenzenu?[emoji1][emoji1][emoji1]
 
Mke wako mjinga sana yani anafikiri akifanya hivyo aibu itakuwa upande wako tu, vipi kuhusu watoto au yeye mwenyewe? Mkuu nakazia tu usiombe msahama wa staili hiyo.
 
Kwani mlivyo hitilafiana mlikuwa kwenye huo umma wa kanisa mkuu
Kuwa mwanaume sio mvulana
 
Kwani hilo kosa/dhambi uliifanya kanisani mpaka ukaombee msamaha huko?
 
Kanisani unaenda kutubu kwa Mungu tu.mambo ya mke n.a. mme yanaishia chumbani.
Unless Iwe imeletwa n.a. nabii kwa njia ya ufunuo
Haya mengine ni ya kwake
 
M

Mkewe atakuwa akina Atuganile Mwakifulefule,,,unamkosea dada msamaha unaomba ukoo mzima [emoji23][emoji23][emoji23] pambana na hali yako.
Hahha afu itabidi tu uoe mnyaki; unatukubali sana kimoyomoyo
 
Nenda tu mzee baba Mbona Nape katubu na kadhalilishwa na mambo yanaenda?Just kidding kaka baki na msimamo wako!
 
Nenda nae kanisani,
Muombe msamaha na yote anayotaka uyafanye,
Hii itafanya upime ujinga wa mkeo,ujinga wa viongozi wa kanisa,
Halafu ukisha Fanya anayotaka tangaza hapo hapo kuachana nae mbele ya hao hao anaotaka waone unavyomuomba msamaha
Safi mwanamke gani huyo
 
Inawezekana kafanya makosa makubwa sana alafu humu watu wanampa kichwa[emoji3][emoji3][emoji3] inawezekana mtaa mzima unajua uovu wake,, mke lazima ampeleke mbele ya kadamnasi ili apate amani ya moyo na amwamini tena.. mbona siku ya harusi walienda humohumo kanisani.

Kwani kumwomba msamaha umpendaye mbele ya watu kunashida gani? Ninachojua kutakua kuna shida kama maombi hayamaanishwi.
Kwani akimuomba mkewe msamaha wakiwa ndani kuna ubaya gani?
Msamaha unatolewa kwa masharti hili la wakristo wa wapi??
Kwa hiyo anataka watu wote wajue mumewe ni mkosaji ili iweje??
 
Usifanye huo upuuzi bana!!

Tena ikiwezekana mwambie aondoke kwako akatufute mwanaume mwingine!
Shwaini sana huyo!
 
Nenda nae kanisani,
Muombe msamaha na yote anayotaka uyafanye,
Hii itafanya upime ujinga wa mkeo,ujinga wa viongozi wa kanisa,
Halafu ukisha Fanya anayotaka tangaza hapo hapo kuachana nae mbele ya hao hao anaotaka waone unavyomuomba msamaha
Safi sana ampige chini na yy mbele ya kanisa
 
Pole mkuu
Wakuu nawasalimu,

Niko katika hali hii kwa sasa.

Ni kweli nilimkosea mke wangu. Nilifanya dhambi kama binadamu wengine wafanyavyo dhambi. Nimejutia kosa langu na nikaamua kumuomba msamaha mke wangu ili maisha yaendelee.

Jambo la kushangaza ni kuwa mke wangu huyu wa ujanani amekataa kunisamehe. ametoa mashariti kadhaa ili niweze kupata msamaha wake. Mashariti hayo ni haya.

1. Jumapili hii twende kanisani nikaombe msamaha mbele ya kanisa.

2. Turekodi mkanda wa video ili hata watu wengine ambao hawatakuwepo kanisani waweze kuona tukio hilo hapo badae.

3. Amesema pia nikiwa namuomba msahama mbele ya kanisa nimuite mama na wala siyo mke huku nikiwa nimepiga magoti.

Wakuu, nimefikiri sana swala hili. Nia hasa ya mke wangu ni nini. Hivi ndivyo msamaha unavyoobwa?

Nimejiuliza tena kwani atapungukiwa nini kama atanisamehe tukiwa wawili tu bila kamera?

Nilichopanga ni hiki , nataka kugoma kufanya kitendo hiki. Ninagoma kwa sababu nataka kulinda utu wangu. Kufanya dhambi au kumkosea mke wangu hakuondoi utu wangu hata kidogo.

Siko tayari kuuza utu wangu kwa gharama ya kulinda ndoa. Utu huwekwa na Mungu ndani ya mtu. Kuuza utu wako kwa mtu ni kumfanya mtu huyo kuchukua nafasi ya Mungu katika maisha yako. Siko tayari.

Msamaha una misingi yake. Moja ya misingi hiyo ni kulindiana heshima.Msahama ni upendo .Upendo haudhalilishi wengine.

Kama ndoa ni ndoano , basi ndoano hii haitaninasa.
 
Kwani akimuomba mkewe msamaha wakiwa ndani kuna ubaya gani?
Msamaha unatolewa kwa masharti hili la wakristo wa wapi??
Kwa hiyo anataka watu wote wajue mumewe ni mkosaji ili iweje??
Kama hawezi masharti si aache, inawezekana mke hataki kumsamehe ndio maana kampa conditions asizoweza kufanya[emoji1][emoji1]
Binafsi mimi sioni cha ajabu kuomba msamaha kama nimekosa kwelikweli, tena ntatumia hiyo nafasi kuonekana mimi ndio mshindi (kama alilenga kunidhalilisha aibu itamrudia yeye)[emoji1][emoji1]
 
Back
Top Bottom