Mke wangu hajali familia

Mke wangu hajali familia

Mwasapile

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2020
Posts
214
Reaction score
448
Habari wana JF!

Ebu wadau naombeni ushauri wenu. Nina mke na watoto wawili. Mke wangu ana changamoto moja hataki kupika na pia hajali watoto. Yaani tunaweza kukaa siku mbili tatu tunakula mikate na chai tu. Na yeye ni mama wa nyumbani sio kwamba ana shughuli kivile za kumkwamisha yeye kupika HAPANA.

Nikimwambia kwanini hapiki anadai sijaenda sokoni kununua vitu (asa nawaza si yeye ni jukumu lake kwenda sokoni) maana pesa za biashara tunazofanya ni yeye anashika kwahiyo sio kwamba haendi kwasababu hana pesa.

Kuhusu watoto ndio kabisa hawalishi wala hawaogeshi, na watoto ni wadogo chini ya miaka 5. Yaani watoto wasipojipambania wenyewe kula ndio basi hawali.

Kuna saa nakasirika kinoma lakini nakosa namna. NIFANYEJE
 
Ana umri gani huyo mkeo? kama ni kizazi cha instagramu na fecebook kazi unayo hapo ni wewe mume kuwa mbogo tu na sometime akiwa haelewai kwa kauli zako inabidi na makofi yahusike kidogo maana huyo inaonekana hana hofu na wewe kwa sababu anjua humgombezi, Kung’uta huyo akili imkae sawa
 
Mlikaa muda gani kwenye mahusiano kabla ya kuoana?

Hao ndio aina ya wanawake wana kucha ndefu kwenye mikono, nywele bandia,nyusi bandia hata kufua chupi zake huyo ni mtihani.
 
Kama mke hajali familia ijali wewe mkuu.

Watoto wana DNA kubwa ya kwako kuliko ya mama ingawa wao ni wa mama. I mean baba tuna transfer genes zetu kwa vizazi vijavyo ila owner wa watoto ni mama.

Jambo la pili, mwanaume ukitaka uishi maisha mazuri uzeeni hakikisha una watoto wengi wa kike, hao hawatakuacha.
 
Back
Top Bottom