Mke wangu hapendi kuongozana na mimi barabarani

Mke wangu hapendi kuongozana na mimi barabarani

Kuna mambo magumu sana kuyafanya kwenye jamii za kiafrika. Hivi unaweza kusema namuacha mke wangu kwa sababu hafuatani na mimi? Wakati anapika, anaangalia nyumba, anaangalia wanao, na akienda kijijini na wewe anakaa nyumbani akipika na kusimamia mambo mengine na anakataa kuenda kubarizi na wewe mitaani?

Mtoa mada anapaswa kuongea na mkewe na kufanyia kazi majibu. Sio kuleta ubabe wa kiume. Mapenzi hayashikiliwi na plasta.
Yap hata mm nakuunga.mguu ooh sorry nakuunga mkono hapo jamaa hana sababu ya kumuacha cha msingi atafute mchepuko wa Ku toka nayee out hiloo tu maana hakuna lingine, wengine hao ndo tunawatakaga unatafuta mtoto mkali special kwa mitoko tuu
 
Ninachoamini mwanamke akikupenda suala LA mavazi sio issue kabisaaa atakushape aonavyo yeye kwa kukunua nguo anazoona zinafaaa, mpaka mke hatak uongee mbele ya rafiki zake mmh wengine elimu yake kubwa kuliko yako au hakutegemea kuolewa na ww imetokea bahati mbaya fanya upelelezi utagundua ukweli pengine anakidumu pemben mke gani huyo anakosa heshima? Ukimgegeda mdogo wake atasemaje
 
Hapo cha maana ni kuongeza upendo kwa mkeo ongea nae vizuri mjali jioneshe kuwa wewe ni mume mwema na acha kumuwazia mkeo mabaya
 
Kaka pole sana, ni dhahiri unampenda ila yeye hatambui uthamani wako. Fanya hivi, usimwoneshe vita ya wazi wazi pamoja na kwamba umeshamwambia hufurahii tabia yake. Piga magoti umwombe Mungu maana yeye anauwezo wa kumbadili mkeo unavyotaka wewe, wewe kama wewe hautoweza kaka. Pili inawezekana aliolewa na wewe kwa sababu fulani ambazo ni nje ya upendo wa kweli na sasa anashindwa kutoka humo ndani ya ndoa maana ishafungwa tena. Mimi ninachoamini ni kwamba "at some point a woman can learn to love". Endelea kumpenda wala usimdharau. Unapitia wakati mgumu najua lakini endelea kuwa mwaminifu Mungu atakusaidia. Mwombe MUNGU afunge hilo lango la uharibifu shetani alilolifungua kwenye ndoa yako. Nawe utashinda tu.
 
Mkuu wanawake wengi ni wazuri katika kufanya mawasiliano yasiyo dhahiri.Inaonekana kwa muda fulani mkeo amekuwa akikuonya kwa kutumia mawasiliano yasiyo dhahiri ('body languages') na wewe ima hukubadilika au hukuelewa. Huenda hata amehisi mahusiano yasiyofaa na shemeji yako lakini anashindwa kusema.. Na umeendelea kufanya yale asiyoyapenda, ambayo anaona yanamshushia hadhi bila kujua kiasi kwamba anaona unafanya kwa kusudi. Kwa hiyo hali hii huenda ikawa anakupa adhabu au anajiandaa kisaikolojia na kihisia kutengana na wewe halafu baadaye inakuwa 'physical separation'. Hivyo jiandae kwa lolote..
 
Wanandoa muongee kuhusu mahusiano yenu kama kuna tatizo make chini mliongee kwa pamoja. Hakuna tatizo la ndani ya ndoa ambalo litaponeshwa nje ya ndoa. La ndani liishie ndani mkifanya hivi mtafurahia ndoa yenu
 
Jibu rahisi kwako "umechokwa" na pengine tatizo sio wewe bali yeye kashaona vyenye kukuzidi kete
 
Wewe unapenda show offf ehhheee, yawezekana ulilishwa miguu ya kuku ukiwa tumboni.
Sasa ukianza kutembea unatembea kama upo kwenye parade mwndo kasi, hapendi kuchoshwa.
Kama tendo la ndoa anakupa bila wasiwasi hapo hamna shida,
Pia yawezekana una gubu, ukiwa na gubu huwezi kujijua,
Halafu unongea pumba kishenzi, sasa wewe unajiona upo sawa. Kweli kwa akili zako, sababu duniani kila mtu anijiona yeye ndio mwenye akili
 
Hahaha nimecheka kama mazuri!

Kwanza nianze na disclaimer. Binafsi i love flaunting my man around, kwa sababu siwezi kutoka na mwanaume ambae i am not proud of.

Hisia zangu ni kuwa huyu dada hakuwa hivi mwanzo. Atakuwa alimpenda kwa dhati huyu mtoa mada lakini ikafika mahali akawa hayuko proud tena na mumewe. Na suspicion yangu ya kwanza ni kuwa mwanaume anafanya ujinga (labda wa kuwa na affairs) hadharani kiasi kwamba dada anaona aibu kuitwa mke wa fulani.

Mahusiano ni mtihani. Ila mtihani mkubwa ni mwenza kutokuwa proud na wewe. Kama huwezi kurekebisha hiyo kasoro iliyomfanya aanze kukukimbia, jiandae kisaikolojia manake anakupigia mahesabu ya kukuacha aisee. Kama hujui sababu muulize mdogo wake ama rafiki yake wa kike. Wanaume huwa hawaoni sababu za wazi kabisa. Niamini, mwanamke hawezi kukukimbia kwa sababu ya muonekano ila kwa sababu ya how you make her feel!

Nakubaliana na wewe 100% hasa hapo katika sentensi ya mwisho.... "Naamini mwanamke hawezi kukukimbia Kwa sababu ya muonekano ila kwa sababu ya how you make her feel"
 
Wanandoa muongee kuhusu mahusiano yenu kama kuna tatizo make chini mliongee kwa pamoja. Hakuna tatizo la ndani ya ndoa ambalo litaponeshwa nje ya ndoa. La ndani liishie ndani mkifanya hivi mtafurahia ndoa yenu

Ushauri mzuri Sana huu....
 
Habari!

Popote ulipo mtoa mada. Ni miezi sita imepita tangu uombe msaada, natumai ushapata suluhisho.

Naomba mrejesho.
 
Utakuwa unavaa kama yule waziri wa maji wa sijui Sudan kusini!
Kwahiyo anaona soo kuongozana na wewe.
Mwanaume pigilia viwalo bwana.
 
Labda hauna social education ila dawa yake ni kutafuta mwanamke mzuri zaidi yake hlf just makusudically lose interest in her for a while, nenda likizo kdg yan ww jifanye km huna hisia nae tena, just kiddin au sanguine ww
 
Back
Top Bottom