Mke wangu ndiye ukoo wangu, ndugu huna nyongeza yoyote

kumekuwa na desturi za ndugu na jamaa kuingilia Mambo ya NDOA za watu na kutoa ushauri utadhani wao walisona vyuo vya ndoa.
Ninavyojua Mimi ndoa haiwezi kua na amani maisha yenu yote Kuna siku mnatofautiana
Nilichojifunza katika maisha mpaka sasa ni kwamba, watu hupenda kuzungumza yale yanayoweza kuwafurahisha nafsi zao hata kama wewe yanakukera.

Mtu anaweza kukusema vibaya kwa kuwa ndoa yako haina mtoto, lakini yeye mwenye watoto amezaa vibaka na makahaba watupu ila wewe usiya na watoto unafanya kazi BOT kama Manager na yeye ni fundi seremala huko Mbagala na humsemi vibaya.
 
Nakumbuka mama mkwe wangu aliwai kuja kusimamia kijana anifukuze eti acha akusanye kila kilichochake, mpishe kwanza....akamchukua wakatoka akijua kijana kanipa muda hatorudi siku iyo analala kwao 🤣🤣🤣🤣🤣 jioni mr akarudi Kwake km kawaida na mahaba na kuomba msamaha juu eti ndugu zangu waache ndoa ni mimi na wewe! Mama akagundua kijana hakulala kwao asubui saa 12 kafika eti mumeo yupo nkamwambia yupo akamfuata chumbani bado amelala hana habari nliona mama anatamani kulia
 
Pole sana mkuu. Akina mama wengi hupenda watoto wao wa kiume waoe kwenye familia za mashosti zao lakini akina baba hawana time na hilo. Baba ukimpelekea mwanamke yoyote hana noma ilimradi mmependana tu baaas inatosha.

Kama kuna jambo linawatesa sana sisi akina baba ni kufanya mama mzazi, mke na dada zetu waive chungu kimoja. Huu ni mtihani mkubwa sana kwetu wababa.
 
Khaaaa jamani, mwisho aingie chumbani akute upo juu ya kijana wake....
 
Itafute Hekima sana.kwa hiyo akili hata kuishi na mke huwezi
Kutafuta hekima Kuna namna nyingi siyo Kama unavyofikili
Nina miaka 11 kwenye doa uvumilivu machungu nayajua vyema
Waulize wanawake ambao Hawana watoto utajua namaanisha Nini
Sijakurupuka kuja kuandika hapa
 
Ahsante sana....ila walishalazimika kunyamaza tunaishi ivo ivo kinafki
 
Ahsante sana....ila walishalazimika kunyamaza tunaishi ivo ivo kinafki
Bora siku ziende tu hilo ndilo la maana. Wake wa watoto wako wa kiume na wewe watakuja kukufanyia hivyo hivyo, na wao pia watoto wao watapitia hayo hayo yaaani ni cycle isiyoisha.
 
Ila wakati unamuoa ulitushirikisha
 
Limbwata @ work. Kila mtu ana sehemu na umhimu wake. Mke kwa wakati wake na ndugu kwa wakati wao.

Ndugu ndio walikuwa wanauza mihogo walipe ada hadi ukakutana na huyo slay queen.
Umenenaa kweliii,ni wanaume wapumbavuu tu wanaooa na kusemaa nduguzao hawawahitaji zaidi ya mke wakee ni ushenzi wa hali ya juu

Na ajabu mke anawajali nduguzake zaidi hahahahaaa wanaumee nyieeeeeeeee
 
Huna ulijualo kuhusu undugu na urafiki. Ni kweli usiruhusu ndugu wakaingilia mambo ya ndoa yako. Lakini mke si ndugu yako, huyo ni rafiki yako wa karibu sana, japo siku moja mkitengana anatajawa 'alikuwa mkewe'. Haitatokea ndugu yako ikasemwa 'alikuwa nduguye'. Ndugu ni watoto wako, si mkeo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…