Mke wangu wa ndoa kapewa Mimba na mtu mwingine

Kwa scenario hii hata Rc wanavunja hii ndoa unless hutaki ivunjwe,uamuzi ni wako
 
King'asti nachoomba ushauri je naweza oa kwa ndoa tena kwa hyo scenario


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Huyu Mwanaume Anatufanya Sisi Watoto!eti Sikupewa Likizo Miaka Mitatu Mara Oooh Sikukutana Na Mke Wangu Miaka Kadhaa,yaani Unataka Kusema Na Mkeo Nae Hakupewa Likizo Pia?na Je Huyo Bosi Asiyekupa Ruksa Kwenda Kwa Mkeo Yupo?mimi Nahisi Huko Mkoani Ulipata Demu Mpya Ukasahau Mkeo Dar,nae Akakuchukia,matokeo Yake Wote Mkaangukia Pua Ktk Mahusiano Yenu Ya Nje!ww Utakuwa Umeachwa Na Unapoachwa Unakuta Kurudi Kwa Mke Hakufai Kashajazwa Mimba!kifupi Hapa Hakuna Mke Wala Hakuna Mume!wote Hovyooooo!
 
Nadhan ww ni mmoja kati ya ambao manfanya jamii forum isiwe jukwaa la watu wanao fikir
Unachosha mkubwa...hii kitu wala si ya kuleta JF..kila kitu kipo so open like vazi la kahaba then huna macho ya kuona...!!
Hata ushauri unaoutaka hautakusaidia chochote kama primarily wewe mwenyewe hujitambui!!
 
Piga chini huyo mzinzi!! Ushauri tu kwa akina mama waliolewa au wanawake walio na commited relationship!! Ni kwamba hawara anakupenda ukiwa kama ulivyo kwa kuwa anajua kuna mwanaume anakupa msaada au vinginevyo!! Siku ukiachika kwa mumeo au ikitokea umepata mimba na ukikataa kuitoa jua ni mwishoa wa kukukimbia jumla!! Hapa mkeo ameshakimbiwa na sasa anatafuta pa kukimbilia na si mapenzi toka kwako!! Ila nashangaa kwa upuuzi huu bado unauliza ushauri!! It is straight forward hata kwa dini za kikristu mke huyo anapaswa talikiwa!!!
 
Pole sana kaka, kwanza ujue huyo mwanaume wake ameshampiga chini ndio maana anajifanya kukunyeyeke.
Wewe nenda kamuone aliyekufungisha ndoa kama unataka kufunga ndoa nyingine, huo ni uzinzi ambao ni sababu inayopelekea ndoa ya kikristo kuvunjika. Ameona kumbe upendo wa dhati unao wewe, ila yeye ni mwanamke ambaye hana msimamo na mzinzi mkubwa tena hafain katika jamii, unaweza kulea mtoto cos hana kosa, ila kwa style hiyo mnayoishi baada ya mwaka atakuwa na mimba nyingine kisha atajinyenyekeza kwako ili ulee mtoto wa watu kwa mara nyingine, halafu akikutana na bwana ake wanakucheeeka na kuchekaga.

Fanya uamuzi wa kiume, na hilo si kosa mbele za Mungu kwa kuwa huyo amezini, n i aibu ilioje kwa mwanaume aliyeoa kulea mimba ya mwenzake na kisha kuendelea na mwanamke huyo!! huyo lipo lililompata kwa huyo mwanaume, kama anaomba msamaha akuombe wewe, wachungaji kanisani na familia zote mbili!
 
sali salam maria mara saba,kisha mwambie Mungu asante kwa kujua Ukweli then usimtafute kabisa huyo mke endelea na shughuli zako
 
Yaani duh!kweli tunatofautiana!! kuna cha kuuliza mara mbili kweli hapo?...mwanamke hana matatizo ,ni wewe mwanaume una udhaifu ambao ndio anautumia......muda si mrefu atakuzalia mtoto wa pili , watatu nk
 
pole sana story yako kidogo ifanane na ya uncle wangu, yeye alianza na vikao na familia mbili yani ya mke na yake
Baada ya vikao hivyo akaandika barua kanisani kwao wakaa vikao kadhaa na. Wazee wa kanisa na padri baada ya hapo wakapata kibali cha kupeleka kesi mahakama ya usuluhishi kurasini baraza la maaskofu then hapo ndipo wakabatilisha ndoa ndio akaenda mahakamani ila unaitaji mda sana sababu yeye ametumia miaka miwili ndio amepata kibali cha kuoa tena.



Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Yaani daaah! Yaani diiih! Yaaani duuuh! Huyo mkeo kimeo hachana nae kama mimba kakuletea ya nje hata ngoma atakupa na zaidi utaletewa mpaka mtoto mchina huyo kicheche uliharakisha kuoa... Ndoa si mchezo ndoa sio lelemama mtu wa kuoa inabd umsome kitambo ndo ufanye maamuzi ya agano la maisha kumbuka ww ni mkristo kuwa hakuna kitakachowatenganisha zaidi ya kifo na ndo maana sasa unapata shida... Ila haina jinsi mpige chini amekuzalilisha sana anza kurasa mpya!!!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
 
Wewe utakuwa kilaza, huyo mtoto ni wa kwako ,kitanda hakizai haramu kamfanyie shopping haraka..
 
Kama kuna sumu hatari duniani ni mapenzi. Mtoa uzi anampenda sana mkewe. Pamoja na kuzaa na mwingine yeye bado anampenda. Watoa ushauri mtambue hilo na mlizingatie ktk ushauri wenu. Hii fani mie naiogopa kidogo
 
Kitanda hakizai haramu, we tunza mimba nawewe upachike ya kwako.
 

Kwa maelezo yako inaonyesha unampenda sana mkeo-good,mtu mwingine wa nini tena?kama umeweza kumvumilia katika yote hayo.....na una uhakika gani huyo utakayefunga naye ndoa naye hatakuwa na vituko zaidi ya huyu wa sasa.cha msingi na cha maana kwa sababu ameonyesha kujirudi endelea kuishi nae.ILA kuwa mwangalifu inawezekana huyo mkeo alikuwa si mwaminifu toka mkiwa marafiki hadi unamwoa NA SIO KWELI kwamba ameteleza na inawezekana akaendelea kukusaliti mbeleni.AKIRUDIA TENA UNARUHUSIWA KUMWACHA ASIJE AKAKATISHA UHAI WAKO KWA GONJWA HILI.
 
Sasa unatafuta mke au?si useme moja kwa moja tu mpaka utusimulie
Mtafute na wewe mke wake au demu wake mpe mimbaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…