Mkoa wa Mbeya Wavunja rekodi ya Makusanyo ya Mapato kwa asilimia 105% Mwaka 2021/2022

Boss ni Mwanza ipi unayosema Mwanza ya Somalia, Karagwe, Mpitimbi, Dareda , Malinyi au Kibondo? kwani Mwanza we umewahi kufika au umeona picha tu za mnara wa samaki kwenye mji mdogo unaoitwa Jiji...
Butimba kona adi huko butimba ttc si kuna lami kabisaa 5km. Pia buhongwa adi nyashishi mbona kuna lami pia barabara ya makongoro ambayo ni njia nne mbona hujaihesabu🤣🤣🤣.

Umenifurahisha sana kusema mwanza ina barabara mbili pia haina viwanda ata kipofu atashangaa kwa hili.
Labda hiyo barabara ya kuanzia airport adi igomba pamoja na ya kisesa adi kayenze japo kisesa ipo nje ya jiji.
Wahusika wamekusikia.
 
Butimba kona adi huko butimba ttc si kuna lami kabisaa 5km. Pia buhongwa adi nyashishi mbona kuna lami pia barabara ya makongoro ambayo ni njia nne mbona hujaihesabu🤣🤣🤣...
ILe ya Makongoro ya njia nne mi naihesabu kama Kenyatta road toka Buhongwa tu Airport ndo maana sikuihesabu!!

Ukitoka Butimba unakata left just 10 minutes kutoka city centre kuna vumbi road inaanza hadi Sweya aibu tupu jiji au mji!

Huko Kanyerere sijui Maina just ten minutes kwa gari kutoka city centre mavumbi tupu jiji gani
 
Butimba kona adi huko butimba ttc si kuna lami kabisaa 5km. Pia buhongwa adi nyashishi mbona kuna lami pia barabara ya makongoro ambayo ni njia nne mbona hujaihesabu🤣🤣🤣...
wahusika wanajua nimesema ukweli na barabara nilizowatajia huwa wanapita na magari na kuwatimulia raia vumbi!!

Mtu ukiwa Dar ukaambiwa unaenda Jijini Mwanza unarukaruka ukifika jiji hulioni mavumbi tupu yanatimka unapotoka tu kwa hizo two main roads Kenyatta na Nyerere!!
 
ILe ya Makongoro ya njia nne mi naihesabu kama Kenyatta road toka Buhongwa tu Airport ndo maana sikuihesabu!!
...
Kumbe ata kenyata road huijui mkuu, kenyatta road ni barabara inayoenda shinyanga adi Dar na inaanzia pale Mwanza zero, nyerere road ni barabara inayoenda musoma adi Nairobi.

Je kuna uhusiano gani kati ya makongoro road na kenyatta road? utakuwa umevurugwa sio bure.
 
ujumbe umefika habari ya kuvurugwa ni kweli jina kubwa mji mdogo vumbi tupu
 
Unataka kila eneo lipitiwe na barabara ya lami kwa huko Dar hakuna sehemu zenye vumbi? Kuwa muungwana na ushukuru kwa kidogo na kaa ukijua serikali inaangalia majiji mawili ya Dar na Dodoma hizo barabara za mitaa kuja kufikiwa sio leo, pia kuna mradi wa tactic utapunguza adha ya vumbi kwa barabara za mwanza mf. Kutoka Buhongwa adi igoma kupitia kishiri 14km, pia barabara ya nyamongholo adi buswelu 9.5km pia na hiyo ya mkuyuni adi nyakato kupitia mahina na kanyerere.
Otherwise utakuwa unayako unayoyatafuta.
 
This is purely an opinion of an outsider from Mara!

I have no intention of nothing!I

I had a lovely picture of Mwanza as a big and rich city in my mind but when I saw the town's rough roads I laughed and thought of the role of Members of Parliament fr5om Mwanza constituencies kuwa "kazi yao kupiga meza tu"!!
 
ujumbe umefika habari ya kuvurugwa ni kweli jina kubwa mji mdogo vumbi tupu
Haya nitajie jiji lako lilikloamilika kwa miundo mbinu ya barabara hapa Tanzani, kiufupi wewe ni mpumbavu, nimepoteza muda kukujibu,mtu mwenye chuki na wivu wako binafsi.
Kiufupi wewe ni fala usiyejitambua na wala huijui Mwanza pili mwanza huwa haina watu mapopoma wenye akili za panzi kama zako.
 
mi fala bin farasi ila ukweli unauma sindano na dawa vimeingia. mi si wa Mwanza boss ni kweli ndo maana nimeona mapungufu yenu kwetu Mara tunakula kichuli!
jiji gani limejaa barabara za vumbi nje kidogo tu ya city centre! punguzeni vumbi mjini!!
Omeraaa
 
Vichache ulivyoandika vinaukweli ila Mbeya bado wanalakujifunza Mwanza , Mwanza naifahamu vizuri sana mkuu huwez nidaganya hata kidogo unaweza kwenda Buhongwa kutoka kisesa ukapitia bypass ya usagara hiyo ni lami, ukienda Buswelu waweza pitia sabasaba au kule national njia zote ni lami.

Kutoka Nyegez kina mpk malimbe kote huko ni lami na sasa wanaendelea na ujenzi had Luchelele huko, ukitaka kwenda nyasak waweza pitia njia ya buzuruga au kupitia pasias kote huko ni lami. Hata maeneo ambapo hawajaweka lami wamejenga kwa mawe..

Kuhusu buashara ya dagaa na samaki kuwa ya msimu huo pia ni uongo mtupu labda uweke ufafanuzi nami tafafanua.
 
nyie piganeni na ukweli tu! mi nawasaidia kuboresha mji wenu!

viwanda vya kusindika minofu ya samaki kwishney , samaki na dagaa wamehamia Kenya!

waulize wenyeji!
 
Utapoteza muda kubishana na popoma, yupo hapa kufanya propaganda mbaya dhidi ya jiji la Mwanza.
 
Mtu sijui katoka wapi anakuja kutema ushuzi et mwanza inaviwanda vya dagaa na samaki tu🤣🤣
Mwanza kiwanda ambacho hakuna ni cha cement tu, ata viwanda vya kutengeneza meli, feries na boats vipo.
Samaki na dagaa et wameamia kenya🤣🤣🤣 hao kenya hapo hapo kisumi wanaumiliki wa ziwa victoria kwa asilimia ngapi kama si 12% ya ziwa victori et leo hii Mwanza izidiwe na kenya soko la samaki at miaka 200 ijayo haiwezi kutokea.
Mwanza pekee inasafirisha tonne ngapi za samaki nje ya nje na inaingiza kiasi gani cha pesa nchini.
Wivu chuki dhidi ya Mwanza hakuwezi kuwaletea aheni wanatakiwa kijifunza kwa waliowatangulia.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ni muongo ndiye alitoa taarifa za kisushi na mimi nikanukuu..

Anatakiwa kutoka hadharani na kuomba radhi.
Si unawafahanu tena Wanasiasa!

Ndio maana waungwana wanakwambia Mwanasiasa akikwambia habari za usiku inabidi utoke nje ujiridhishe kweli huu muda ni usiku.

Kuna attachment kuna mtu ameiweka inaonyesha hayo ni makusanyo ya kuanzia Julai 2021 hadi Machi 2022, hapo bado kuna miezi 3 haijaweka, inawexeka hiyo miezi 3 ilipowekwa kuna mikoa wamekusanya zaidi wakaipiku Mbeya.

Nimeiweka tena hapa.
 
Weka na viambatanisho vya makusanyo ya Sasa hivi.
 
Siku hizi watu wengine hutumia takwimu kupotosha kwa malengo ya kisiasa au ushabiki wa kijinga tu.
Tunahitaji elimu na pia ufahamu wa jumla (general knowledge) ili tupate maendeleo endelevu.
 
Najua umeandika haya kwa utani tu,hauwezi kuwa siriasi...ila kwa kuwa jukwaa hili ni la Mambo siriasi,na Mimi nimechukulia siriasi Hadi nimeamua kukunukuu.

Unasema Serikali ijenge "flyover" uyole, kwa ajiri ya Nini pale uyole,ili watu wawe wanavuka kwenda soko mjinga pale kingani??

Mafiati "flyover" ni kwa ajiri ya kuflyia kitu gani pale,magari hata yakiwa na foleni kubwa sanaaa, hayazidi magari 100 pande zote .

Et Mbalizi kujengwe "flyover". Ya kutoka wapi kwenda wapi pale labda?ungewasaidia wakazi wa Mbalizi Kama ungependekeza hayo mapato tunayotamba tumeongoza,wajengewe barabara za lami za mitaa waepukane na vumbi Kali linalokuja mwezi huu wa nane huu.

Hizi sifa tunazojipa sisi wana Mbeya,asilimia kubwa ni za uongo,mji wetu bado Sanaa,.hizi sifa tunazojivika ndiyo zinafanya mgeni akija huku,mkiwa pale uhindini ( mjini katikati) mgeni anauliza swali linalotukera sisi wenyeji. Huwa wanauliza " mjini ndiyo wapi?", Kumbe tuko mjini katikati,unamoa mgeni wako jibu kuwa ni hapa hapa tulipo

Halmashauri zetu ziongeze Kasi ya kujenga miji yetu badala ya kufuja pesa zinazoletwa na Serikali na wanazokusanya wenyewe
 
Mama, We love you
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…