Mkoa wa Tabora kugawanywa na kuwa mikoa miwili

Mkoa wa Tabora kugawanywa na kuwa mikoa miwili

Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu
tangu waugawe mkoa wa arusha na kupata mkoa wa manyara, wananchi wamepata huduma zote? suala la kusogeza huduma kwa wananchi linategemea ni ufanisi na uwajibikaji. waongeze ufanisi kwanza, kisha wanaweza kugawa maeneo watakavyo!
 
na bora Dar ikawa wilaya ya mkoa wa Pwani kwani kaeneo kake mara nne ndiyo wilaya ya Nzega!
 
Ni ukweli kuwa huku ni kuwagawa watanzania na kupunguza moyo wa umoja na udugu miongoni mwa watu waliokua wanajiita watu wa Tabora ,hii familia moja sasa itagawanyika na kuwa watu wa nzega na Tabora.

Nilitegemea serikali iimarishe na kuboresha ofisi za makatibu kata na makatibu Tarafa na kuwaongezea mamlaka ya kiutendaji na kwa kuwa wako karibu zaidi na wananchi.

Wananchi wanataka huduma za shule,hospitali,maji,barabara, Wataalam wa kilimo na misitu n.k na sio kuwaongezea mizigo ya kutumia kodi yao kuwahudumia watawala.
Kama kila mkoa ungekua na jukumu la kuhudumia watawala wake niwazi kuwa Mikoa mingi isingekua na uwezo wa kibajeti wa kubeba mzigo wa kuhudumia wakuu wa mikoa na safu nzima za uongozi wa mkoa.
Ni mizigo tu kwa mwananchi wa kawaida.
Leo hii hata ungemwambia mtanzania akuchoree ramani ya Tanzania na mikoa yake hawezi.

Tumieni fedha za kujenga maofisi na kununua magari ya Vx v8 kuweka lami barabara za huko vijijini ili wananchi wasafiri kwa urahisi kufuata huduma.
Kama barabara ni mbovu hata kamkoa kadogo katakua tabu tu kufuata huduma.
Mfano tu ni wakati barabara ya Lindi Dsm ilipokuwa ya vumbi tulikua tunatumia mpaka siku mbili kufika Lindi toka Dsm.Leo hii ni masaa 5 tu.
Umbali sio tatizo suala ni miundo mbinu bora.
Vipi CCM kama mmeshindwa kazi wapisheni wengine waje na mbinu mpya.
 
Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu


Mkuu umesoma maoni ya wadau humu ndani kweli?
 
Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu

joseph, joseph, joseph ernei;
Ni huduma zipi za jamii huletwa na mkoa kugawanywa? Nakombuka enzi Mwl. anapokea nchi, tulikuwa na mikoa 7 Tanganyika yote. Leo mikoa 26+ hata kiwanda cha kusindikia asali cha taifa hatuna.
Huduma zinazohitaji mkuu wa mkoa mpya ni zipi ka si ulaji?? Toa fedha ya kutosha ya Maendeleo, ipelekwe kwenye sehemu husika, uone maajabu ya Musa. Zisimamiwe na mzalendo halisi au yule mwana kijiji aelezwe zimefika ngapi na ni za kufanya nini uone maendeleo.
Kugawa mikoa sijaona mantiki yake kutuletea maendeleo, bali kupeana ulaji tu. Ningeshauri tupunguze mikoa, haswa huko Zanzibar. Mkoa ukubwa wake haufikii kijiji chetu! Tuwekane wazi tu tusiogope, kama vipi, hata Manyara ni kubwa mno nayo iwe mikoa 3. Au katibu tawala wa huko anaishia ofisini tu, autembelee mkoa wake kama hatalala nje siku tatu
 
Ni upumbabu wa hali ya juu Mkuu, hawa wahuni kudai kwamba kugawanywa kwa mkoa mmmoja na kuwa mikoa miwili ni kurahisisha utoaji huduma muhimu. Tumeona mikoa mbali mbali iliyogawanywa toka mmoja na kuwa mikoa miwili lakini upatikanaji wa huduma muhimu bado ni mbovu kupita kiasi, mfano mkoa wa Dar na mkoa wa Pwani na mifano hii iko chungu nzima. Serikali inapiga kelele kila siku haina pesa halafu bado inafanya maamuzi ambayo yanaongeza gharama za uendeshaji kwa kiasi kikubwa sana mabilioni.

Anaejua faida ya kugawanya mikoa na kuiongeza naomba anipe darasa maana mie kila nikiangalia ninaona gharama zinazidi kuongezeka.. Au ndo kutengenezeana ulaji hapa na ajira..?
 
Hili jamaa tuliambiwa kwamba lilikuwa bado na umri mdogo kushika pale mahali sisi tukafikri mwalimu alikuwa namaanisha umri wa kuzaliwa!! Kwa ufupi mwalimu alikuwa anamaanisha huyu bwana tulimfanyia upasuaji wa kumwekea kichwa na kwa vile hatukupata kichwa cha binadamu tulimwekea Koroma la nazi, hana akili ya kuongoza, hivyo hawezi kuwaongoza ninyi wadanganyika!! Sisi tukapuuza tukamwaga kula kwa wingi sasa tunayaona machungu yake!!

Anyway, asante Yesu bado miezi 7 tuondokane na huu udhia, hatutarudia tena, tumekoma!! Mkoa wa Pwani unastahili kupigwa Ban kwenye kinyang'anyiro cha kiti hicho maana tumejionea wenyewe! Hawa wabaki kushabikia tu vigodoro haya mambo makubwa hawawezi!! Hivi wanaposema kuboresha huduma huwa wametathmini kuona unapoongeza mkoa au wilaya huduma zinaboreshwa kwa kiwango gani? Hiyo fedha inayoenda kugharamia hizo ofisi ingepelekwa moja kwa moja kwa wananchi si ingesaida pa kubwa? Fikria gharama ya majengo yanayojengwa kwa ajili ya ofisi na nyumba za maafisa wa serikali, magari ya maana yanayonunuliwa (maana hili Punda lilishamshinda, mbona kila uchao tunaona Ma-VX). Mishahara ya watumishi wapya (maana hapa kunakuwa na duplicate ya ule mkoa wa zamani). Sasa hizi gharama jamani tunaziweza sisi? Au kumbebesha mwananchi mzigo asiostahili? Wa-Tz tujifunze kutokana na haya makosa!
 
Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu
Hebu fafanua mawazo yako na sio ya wapenda ulaji...
Huduma kama zipi zinakosekana wakati kukiwa na mkoa mmoja na na zipi zitapatikana kukiwa na mikoa miwili! Maana Bajeti ya Taifa kwa Mikoa huangalia wingi wa watu na huduma zipi zinatakiwa zifike kwa jamii na sio sababu ya mkoa mkubwa maana Dar si kubwa kivile ila ina wakazi wengi na bajeti wanapata kubwa ila hamna la maana linalofanyika kwa mwendo huu wa kuwa na viongozi wavivu wezi tutagawa mikoa hadi ifike elfu moja na hatutaona tofauti.... STUKA!

Mkoa wa Nyanza Uligawanywa na kuwa Shinyanga na Mwanza wakaona huduma bado ni Shida ukazaliwa Mkoa mwingine Simiyu... Bado hali ni Tete watu shida zao zipo pale dawa ni uchapakazi na sio kusifia wajinga
 
Fikra za ulaji hizo, mikoa iliyopo tu ni mzigo kwa walipa kodi sasa tunataka tuongeze mikoa ili!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ukiugawa Mkoa Ndo Huduma Zitapatikana Kiurahisi?????!!,hii Hainiingii Akilini Kabisa Hizi Njia Njia Za Kupiga Hela Kiulazima Lazima Ni Ufisadi Unaonekana Waziwazi
Hapo hela inapigwaji hebu jaribu kubainisha mazingira ya upigwaji wa hizo hela.
 
Mimi napendekeza Tanzania igawanywe ziwe nchi nne ili kusogeza huduma karibu na wananchi.
 
Je pesa kuendesha Mikoa Miwili je itatoka Tabora au Dar es Salaam?

Yaani taabu tu.. kuna tija gani?

Hii nchi iwe a majimbo.. na kila jimbo lijitegemee 40% ya mapato yatoke huko2 majimboni na serikali kuu itoa tu 60% utaona kama kuna watu watagawa mikoa!

Kwa ufupi Gharama kuendesha mikoa mingi zinatoka Dar!
 
Uzoefu tulionao ni kuwa kuugawa mkoa kuwa miwili haiongezi tija wala maendeleo: Rejea (1) Lindi ilichomolewa kutoka Mtwara (2) Rukwa ilichomolewa kutoka Mbeya na Tabora (3) Manyara ilichomolewa kutoka Arusha (4) Katavi imechomoleawa toka Rukwa (5) Njombe imechomolewa toka Iringa (6) Geita imechomolewa toka Mwanza (7) Simiyu imecholewa toka Shinyanga. Licha ya chomoa chomoa hii hii mikoa mipya haijaonyesha dalili za maendeleo. Niko najiuliza, kama kugawanya kunaleta maendeleo, mbona huko USA California, Alaska au Texas hawajawahi kuwaza kuzigawagawa vipande vingi size ya Maine au New Hampshire???
 
Muda si mrefu unakuja ambao pato la taifa linakuwa tilion 20, lakini serikali matumizi ya kawaida mishahara, mashangingi, posho na kadhaa wa kadhaa inatumia tilion 18,shughuli za maendeleo tilioni 2
 
Back
Top Bottom