Ndugu Watanzania wenzangu.
Kipekee napenda kumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuiona tena siku ya leo.
Baada ya kuangalia na kutathimini mwenendo wa kampeni zinazoendelea kwenye vyama vyote, huku nikirejea kampeni za 2015, ni dhahiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu, 2020, Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakina upinzani madhubuti. Kama kichwa cha uzi huu unavyosomeka, zifuatazo ni sababu zilizopelekea kwa CCM kukosa upinzani madhubuti katika uchaguzi wa mwaka huu.
Mkono wa beberu Bob Amsterdam. Kwa mara ya kwanza watanzania tumeshuhudia CHADEMA ikiwa na ushirika wa wazi kabisa na mabeberu, na tumediriki hata kusema sasa chama hiki kimekengeuka na kuwa chama cha mabeberu. Ushirika huu umesababisha chama hiki kujitia doa ambalo litakuwa gumu sana kulisafisha labda kwa kuomba msamaha kwa wananchi. Chadema kilikuwa chama cha upinzani pendwa sana na wananchi tangu kuundwa kwake na muasisi wake Mzee Mtei.
Kilikuwa kinasifika kwa sera zake za kupambana na ufisadi ambao ulikuwa ni mtaji wake mkubwa sana, lakini mwaka 2015, kilianza kupoteza dira baada ya kumkaribisha Mh Lowassa amabaye kilimwita fisadi kwa miaka mingi na kumfanya kuwa mgombea uraisi. Baada ya uchaguzi uamzi huu ulikigharimu sana chama hiki, na kupoteza dira yake kabisa.
Aidha, ushirikia wa beberu Amsterdam na timu yake ndani ya Chadema kwenye uchaguzi huu, naamini utakuwa umefanya baadhi ya watanzania makini, na wazalendo kukisusa chama hiki kwa kitendo chake hiki cha ukibaraka ambao hatujawahi kuushuhidia katika chaguzi zetu na huu siyo utanzania kabisa. Kwa wanaomjua vizuri Mh. Mbowe wa 2015 chini ya Mh. Lowassa, siyo Mbowe wa 2020 chini ya Mh. Tundu Lissu. Kuna uwezekano Mbowe ameshapiga mahesabu yake na inaonyesha anaona giza nene kwa hatima ya Chadema kwenye uchaguzi huu chini ya Mh. Tundu Lissu.
Wapinzani kushindwa kuungana. Jambo hili limesababisha CCM kukosa upinzani madhubuti kama ilivyokuwa chini ya Lowassa 2015 ambayo ilikuwa Magufuli vs Lowassa, ulikuwa ni uchaguzi wenye mvuto sana na upinzani mgumu sana kwa CCM. Hapa limetimia neno lisemwalo umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Mwaka huu ndugu zetu hawa ni dhaifu haijawahi kutokea. Kushindwa kuungana huku kumesababishwa na kutanguliza maslahi binafsi ya vyama vyao.
Wakati wapizani watakuwa wakizigawana kura zao wenyewe, CCM itakuwa na kura zake imara zisozitikiswa, na mwaka huu CCM wapo wamoja sana tofauti na ilivyokuwa mwaka 2015, ambayo ilikuwa na mpasuko na ikapelekea Lowassa kutimuka na wapiga kura wengi sana waliopigia upinzani.
Nahitimisha kwa kusema, mkono wa beberu Bob Amsterdam na wapinzani kushindwa kuungana umesababisha CCM kukosa upinzani madhubuti katika uchaguzi huu, 2020 na inaenda kushinda kwa kishindo kikubwa sana. Kitendo hiki cha CHADEMA kuwa na ushirika na mabeberu kimekitia doa sana chama hiki na athari hii imeanza kuonekana wakati wa uchaguzi huu na itaendelea kuonekana mpaka pale watakapotubu mbele za watanzania, maana huu siyo utanzania.
Asante sana,
Nawasilisha,
Kejuu
Kipekee napenda kumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuiona tena siku ya leo.
Baada ya kuangalia na kutathimini mwenendo wa kampeni zinazoendelea kwenye vyama vyote, huku nikirejea kampeni za 2015, ni dhahiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu, 2020, Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakina upinzani madhubuti. Kama kichwa cha uzi huu unavyosomeka, zifuatazo ni sababu zilizopelekea kwa CCM kukosa upinzani madhubuti katika uchaguzi wa mwaka huu.
Mkono wa beberu Bob Amsterdam. Kwa mara ya kwanza watanzania tumeshuhudia CHADEMA ikiwa na ushirika wa wazi kabisa na mabeberu, na tumediriki hata kusema sasa chama hiki kimekengeuka na kuwa chama cha mabeberu. Ushirika huu umesababisha chama hiki kujitia doa ambalo litakuwa gumu sana kulisafisha labda kwa kuomba msamaha kwa wananchi. Chadema kilikuwa chama cha upinzani pendwa sana na wananchi tangu kuundwa kwake na muasisi wake Mzee Mtei.
Kilikuwa kinasifika kwa sera zake za kupambana na ufisadi ambao ulikuwa ni mtaji wake mkubwa sana, lakini mwaka 2015, kilianza kupoteza dira baada ya kumkaribisha Mh Lowassa amabaye kilimwita fisadi kwa miaka mingi na kumfanya kuwa mgombea uraisi. Baada ya uchaguzi uamzi huu ulikigharimu sana chama hiki, na kupoteza dira yake kabisa.
Aidha, ushirikia wa beberu Amsterdam na timu yake ndani ya Chadema kwenye uchaguzi huu, naamini utakuwa umefanya baadhi ya watanzania makini, na wazalendo kukisusa chama hiki kwa kitendo chake hiki cha ukibaraka ambao hatujawahi kuushuhidia katika chaguzi zetu na huu siyo utanzania kabisa. Kwa wanaomjua vizuri Mh. Mbowe wa 2015 chini ya Mh. Lowassa, siyo Mbowe wa 2020 chini ya Mh. Tundu Lissu. Kuna uwezekano Mbowe ameshapiga mahesabu yake na inaonyesha anaona giza nene kwa hatima ya Chadema kwenye uchaguzi huu chini ya Mh. Tundu Lissu.
Wapinzani kushindwa kuungana. Jambo hili limesababisha CCM kukosa upinzani madhubuti kama ilivyokuwa chini ya Lowassa 2015 ambayo ilikuwa Magufuli vs Lowassa, ulikuwa ni uchaguzi wenye mvuto sana na upinzani mgumu sana kwa CCM. Hapa limetimia neno lisemwalo umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Mwaka huu ndugu zetu hawa ni dhaifu haijawahi kutokea. Kushindwa kuungana huku kumesababishwa na kutanguliza maslahi binafsi ya vyama vyao.
Wakati wapizani watakuwa wakizigawana kura zao wenyewe, CCM itakuwa na kura zake imara zisozitikiswa, na mwaka huu CCM wapo wamoja sana tofauti na ilivyokuwa mwaka 2015, ambayo ilikuwa na mpasuko na ikapelekea Lowassa kutimuka na wapiga kura wengi sana waliopigia upinzani.
Nahitimisha kwa kusema, mkono wa beberu Bob Amsterdam na wapinzani kushindwa kuungana umesababisha CCM kukosa upinzani madhubuti katika uchaguzi huu, 2020 na inaenda kushinda kwa kishindo kikubwa sana. Kitendo hiki cha CHADEMA kuwa na ushirika na mabeberu kimekitia doa sana chama hiki na athari hii imeanza kuonekana wakati wa uchaguzi huu na itaendelea kuonekana mpaka pale watakapotubu mbele za watanzania, maana huu siyo utanzania.
Asante sana,
Nawasilisha,
Kejuu