Mkubwa Fella awaita wandishi wa habari kuwaonyesha majumba aliowajengea Yamoto Band

chinchilla coat

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
5,107
Reaction score
10,969
Mkubwa Fela amewaita waandishi wa habari kuwaonyesha nyumba alizowajengea Yamoto Band huku akisema kuwa project yake ya Mkubwa na Wanawe imekuwa na mafanikio makubwa, amemshukuru pia Rais mstaafu Jakaya Kikwete na Ruge wa Clouds kwani pia alimsaidia sana kwenye mradi wake huo wa Mkubwa na Wanawe
Nyumba hizo amesema zitakuja kuzinduliwa na Kikwete
 
Alichoandika insta ata hakieleweki mtu huelewi ni nyumba za ya moto band kila mtu na yake au ni kambi ya yamoto

Hata mi sijapenda hiyo saresare maua.

Utadhani nyumba za kota...

Halafu sasa haya makundi huja kuvunjika. Likivunjika hilo kundi sijui ndo itakuwaje..

Ila kwa ujumla wake ni jambo jema.
 
Wakuu nisaidieni jibu.
Hivi anawasaidia, au ni nguvu zao na ni halali yao ???
 
kwanza kabisa nimpongeze Huyu Bwana Fella, japo mimi siyo shabiki wa miziki hii ya vijana.

Hila amefanya jambo zuri na la kupongezwa sana amekuwa mfano wa kuigwa.

Wanamiziki hii ya kidunia yawapasa waige jambo hili kuliko kulewa misifa na kuandikwa magazetini.
Mwisho wa siku wanaishia kuomba omba.
 
Kama kweli ni za hao vijana basi kazi nzuri na ziwe zao kihalali sio kundi likivunjika mtu anaporwa nyumba kwa hili ni big up coz kuna wasanii wakubwa tu na wa kitambo hawana hata room moja,.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…