Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 29
Kumbukumbu za nyuma ziliuteka ubongo wangu,…nikakumbuka yaliyotokea huko nyuma, yaliyompata huyu msamaria mwema, tena kwa ajili yangu, akafikia hadi kufungwa na wazazi wangu, …nikaapa kuwa siku nikikutana naye, nitajitahidi nifanye lolote kumlipa fadhila zake, sasa nitamlipa nini, …na nilishamsahau, nikujua hayupo tena duniani…na siku hiyo, ndio nikakutana naye, nikiwa na docta mtoto wa watu akiwa ni mpenzi wangu…je nilifanya nini, angalia mitihani hii ya maisha…
***********
Nakurejesha nyuma kipindi nikiwa binti mdogo, wa miaka kumi na tano,…kipindi hicho ndio nilimuona kijana mmoja mara kwa mara akiwa anakuja kuonana na mzee mmoja aliyekuwa mlinzi wa nyumba yetu. Yeye kiumri alikuwa mkubwa kuliko mimi…nikaanza kuzoeana naye tu..
Kuna kipindi baba yake alikuwa akitulimia shamba, basi na yeye anakwenda kumsaidia baba yake mimi, nikawa nafika shamabi kuchukua matunda, nawakuta wakiwa wawili, nawapatia chochote, mwanzoni sikuwa naongea naye sana, kutokana na hali ilivyokuwa wakati huo. Wazazi walikuwa wakali hawakupenda kabisa nizoeane naye, au kuwa karibu naye,…
Kila huyo mvulana akija, nilimgundua akiniangalia sana, na ikitokea tukikutanisha macho anayakwepesha kwa haraka na kujifanya kama alikuwa haniangalii, ikawa kama mchezo fulani wa utu-rika,.. na tukajikuta tunamezoeana kinamna hiyo, lakini sio ile ya ukaribu ya kukaa pamoja na kuongea.
Ni ikaja muda hata mimi nikikaa nyumbani, namuwaza yeye, fikiria ni mtoto wa mkulima, mfanyakazi wetu tunaweza kusema wa ndani…lakini mimi sikulijali hilo, nilimuona sawa na wavulana wengine. Sio kwamba nilikuwa na tabia mbaya, ya kuwa na mazoea na wavulana, hapana..ila nilijali sana usawa na utu, hata nikiwa msichna mdogo.
Basi kwa ile hali ya kunyanyapaliwa na wazee, kuwa wakifika wanakuwa na sehemu yao, hawaruhusiwi kuingia ndani, sikulipenda hilo kabisa, nikaona lazima nifanye jambo, la kuwasaidia hawa watu wawili…nilimjali sana huyo baba yake, alikwua na tabia nzuri tu,…huruma na upendo,.
Basi…huyo kijana akifika, ninajua wapi nikae ili aweze kupita na kuniona, kwa haraka nikakuwa na zawadi yoyote ya kumpa, chakula au matunda,…maji ya baridi ili wakinda sahamba wapate kuyatumia yeye na baba yake..na nilijithidi sana wazee wangu wasiweze kuona hayo…
Lakini ikatokea tukio, liloharibu kila kitu, na baada ya tukio hilo, tukaachana na familia hiyo sisi baadaye tukahama na kuja kuishi Dar, ambapo baba yangu alihamishia kampuni yake, na huko kijijini tukawa hatufiki mara moja moja tu. Na sikuweza kuwaona tena. Tukio hilo kwakweli liliniumiza sana kiasi kwamba niliwaona wazazi wangu kama ni watu wasio na utu-wema.
*************
‘Kwanini hukunitafuta, ulipoachiwa kutoka jela...?’ nikamuuliza, nikikatiza mawazo yangu ya kumbukumbu za huko kijijini….
‘Kwanini nikutafute..ulitaka niendelee kuumia, maana mimi ningelisemaje kwako, ..hebu nijishushe hapo, baada ya tukio lile, ningelionekana na wewe tena, si ndio ningepeleka tena jela nikafie huko.., nakumbuka niliwahi kuandika barua kuja kwako, lakini sikuwahi kupata majibu...’akasema.
‘Barua,…. hahaha..nani ana mipango ya barua siku hizi, ulindika hiyo barua kuja kwangu ukampa nani..mbona sijawahi kuona barua yako yoyote,...?’nikamuuliza, niliona kama ananitania tu.
‘Basi nahisi kuna mtu alikuwa akizipokea na kuzichana, mimi niliandika, nyie si mna box la barua, na kuna mtu alisema anakuja huko kwenu , nikampa barua, lakini nikajua umeshatekwa na familia yako, na huenda hata wewe hutaki hata kuniona tena, kwa jinsi watu walivonivumishia ubaya....’akasema akitikisa kichwa kusikitika .
‘Kwanini usingelinipigia, angalau hata simu...?’ nikamuuliza
‘Nikupigie simu!!! Hahaha…, simu hiyo ningeliipata wapi, huko kijijini, hivi unayafahamu maisha yetu yalivyokuwa...anyway, hayo yameshapita na wewe una mume wako, ...naona nisikupotezee muda, ...’akasema na kutaka kuondoka, mimi nikamshika mkono asiondoke.
‘Nimeshakuambia yule sio mume wangu, ni mchumba wangu, hatujaoana bado…Sikiliza, ..ahadi yangu ipo pale pale…’nikasema na hapo akaniangalia kwa macho yenye kushangaa.
‘Kwahiyo unataka kusema nini…?’ akaniuliza
‘Ahadi yangu ya kufanya lolote ilimradi niwe nimelipa fadhila zako, najua inaweza isikidh haja, lakini angalau na mimi niwe nimfanya jambo kwako la utu wema..sasa mimi nataka tuje tuongee tena nione nitakufanyia nini…’nikasema, na nikaona kama ananywea, hakuridhika na maneno yangu hayo.
‘Hapana, mimi sihitajii msaada wako, sitaki kuwa mfanyakazi wenu, au ….kuwategemea nyie tena, hapana…hilo sitaki, …’akasema
‘Najua ni kwanini unasema hivyo, ila mimi natamani zile siku zirejee tena, kiukweli mimi sijaolewa, na sisemi hivyo kwasababu kuwa nataka uwe ...mpenzi wangu, hapana mapenzi hayalazimishwi, na…mimi na mchumba wangu hatujafikia huko, bado kuna mipango mimi, yeye na mimi pia, lakini mimi ninaweza kufany ajambo la kukusaidia ukafika mahali, usilipuuzie hilo..’nikasema
‘Hilo la kukutana kuongea tena, ni wewe, kama huogopi huyo mpenzi wako, sitaki kuja kuwaharibia mahusiano yenu, ikawa ndio sababu ya kufichua yale yaliyopita, sipendi hilo kabisa,…’akasema
‘Kiukweli unanidai sana, mengi umenifanyia, lakini sijaweza kulipa chochote kwako, kwangu mimi naona ni deni, na nataka uwasamehe wazazi wangu, hata bila ya wao kufahamu, na hilo naweza kufanya nionavyo mimi, niamini tu,…usijali kabisa kuhusu hisia za wazazi wangu, nafahamu ni kwanini wanafanya hivyo,....’nikasema
‘Hahaha, hapana , niliapa kuwa sitaajiriwa kwa watu kama mfanyakazi wa upendeleo, mimi nataka nihangaike kivyangu…sawa nashukuru kwa kuonana nawewe, mengine tuyaache kama yalivyo, vipi maisha na mchumba wako, katulia siku hizi..?’ akaniuliza
‘Mchumba wangu hana matatizo, ni mzungu kwakweli, muhimu nimuambie ukweli tu, hata akiniona tunaongea, yeye atadai nimuambie wewe ni nani, na ni hivyo, sina shaka naye, ila hayo hayana msingi, wewe sifikiria wako langu la kukuwezesha, unalionaje hilo…’nikasema
‘Mhh…sivyo nitakavyo, najua hutanielewa, ndio maana nasema tuyaache tu, yabakie kama yalivyo, kwa maana mimi nilikufanyia nini kikubwa, ni kawaida tu, na yaliyotokea hadi wazazi wako kufanya hivyo, ni…naweza kusema hata mzazi mwingine huenda angelifanya hivyo…’akasema
‘Hapana lile tukio lilikuwa kubwa, na kiukweli nakiri wazazi wangu walikosea, sana,..maana hawajui ulivyofanya, uliweza kuniokoa mikononi mwa wabakaji, mijitu mikubwa, na wewe ulikuwa sio umbile lako kabisa, ukapigana na wao kufa na kupona, hawakuliona hilo.
Kiukweli mimi..sitalisahau hilo kamwe, nilikuona kama mtu maalumu sana kwenye maisha yangu ndio maa niliahidi siku nikikutana nawe, nitafanya lolote lililondani ya uwezo wangu, ili na wewe uone kuwa nakujali…...’ nikamwambia.
‘Mhh…nilishaipata hiyo zawadi inatosha., wewe wasalimie wazazi wako na mchumba wako, mungu akipenda tutakuwa tunaonana, lakini nisingelipenda wafahamu kuwa tumekutana nafahamu watakavyojisikia, huenda ikaja dhahama kubwa zaidi ya ile…japokuwa sasa nimekuwa mkubwa siogopi, nafahamu haki zangu...’akasema
‘Jamani ina maana hujatusamehe tu…’nikasema
‘Usijali sana ndio ubinadamu ulivyo,..nilishawasamehe mbona…kwa hivi sasa nimeliona hilo, kuwa yale waliyoyafanya wazazi wako walikuwa na maana kwao, kwa ajili ya kulinda heshima ya familia yenu, na walitaka kutoa fundisho kwa jamii, na nasikia familia yenu imekuwa ikiogopewa sana,..ni sahihi, yamepita yapite.
‘Tatizo wewe hufahamu jinsi gani niliumia...lakini ikafika mahali nikasema basi tena, mungu ndiye atakupeni yale yote mliyotutendea wewe na baba yako, na nikatubu sana kwa niaba ya wazazi wangu…kiukweli baba yako nilimuona kama baba yangu mkubwa...sikupenda kumuita babu, kama walivyozoea kumuita wengine, mimi ninajua kuzeeka kwake haraka ni kutokana na hali ya maisha, umri wake haupo mbali na umri wa baba yangu, …mimi nilipenda kumuita baba mkubwa.....’nikasema.
‘Nashukuru kusikia hivyo, ni wewe tu ulikuwa tofauti na wengine, sijui kwanini wazazi wako, walikuja kutuchukia hivyo..niliona kabisa hawakupenda, hata nikukaribie..na nahisi ilipotokea lile tukio, ndio wakaonyesha hisia zao dhidi yangu. Ni sawa, labda nisiwalaumu sana, maana huenda hata sisi tungelikuwa kwenye hiyo hali tungelifany ahivyo hivyo..hata hivyo nawashukuru wazazi wako, kwani pamoja na hilo tukio lakini walitusaidia sana kimaisha...’akasema.
‘Mimi nilikutafuta sana, lakini sikutaka wazazi wangu walifahamu hilo, nilitaka kukulipa fadhila zako, niliahidi moyoni kuwa nikija kuonana na nawewe, nitafanya lolote na nimekkuona naomba usilipinge ombi langu....’nikamwambia.
‘Mimi sihitaji msaada wenu, ….’akasema
‘Hapana ni lazima nifanye wema wowote, nakumbuka kama isngelikuwa ni wewe..sijui ingelikuwaje, na….’hapo tena ndio lile tukio likazama kwenye ubongo wangu nikawa naliona lilivyotokea….
**********
Ilionekana wazo hao vijana watukutu, walikuwa wakinivizia siku nyingi, na siku hiyo gari la baba lilichelewa kuja kunichukua shuleni, nikaamua kutembea na wenzangu, na kwa vile shule ilikuwa mbali, wenzangu wakawa wametawanyika kila mmoja na njia yake, ikafikia mahali nimebakia peke yangu, na ghafla ndio nikavamiwa na vijana wanne, na kunibeba juu kwa juu.
Walinibeba juu kwa juu, hadi vichakani, na wakaanza kunivua nguo, na ukumbuke nilikuwa binti mdogo tu, nasoma sekondari..nilikuwa binti, nimeshavunja ungo, lakini sikuwa na mawazo hayo kabisa, na sikujua ni kitu gani kitakuja kunitokea,..japokuwa nilifahamu kuwa wanatka kunifanya kitu kibaya.
Nilijitahidi kupigana lakini sikuweza kufurukuta kwa vijana hawa wenye nguvu zaidi yangu, na kabla hawajafanya lolote mara akatokea mtu, kijana..machozi yalishatanda usoni sikumuone vyema, akawa anapigana nao, akiwa na kigongo hivi kama rungu, alipambana nao kiume mpaka anakuja kuwazidi nguvu, ilikuwa ni kwa msaada wa mungu tu maana wote walikuwa wakibwa zaidi yake…ikafikia muda, ikabidi wakimbie, baada ya kusikia kelele za watu, wakikaribia eneo hilo..na yule kijana akapiga ukelele kuomba msaada. Wale vijana wakakimbia huku wakilaani kuwa watahakikisha wananifanyia hivyo, siku yake...
Sikuweza kuongea nililia hadi nyumbani, nikiwa nimechafuka, nguo zimechanwa, nnipo kama nudu uchi…na huyo kijana alinsiindikiza hadi nyumbani, nikawahadithia wazazi wangu, na wao kwa haraka wakaifahamisha polisi na hawo vijana wakaanza kutafutwa lakini hawakupatikana kwa siku hiyo hata ya pili yake. Walihama kabisa, kijini hapo.
Cha ajabu wazazi wakaongea na polisi wakaja kumshikilia huyo kijana kuwa atakuwa anawafahamu hawo watu, na alitakiwa kuwataja, na aliposhindwa kuwataja, wakamshitakia kuwa ni muhusika wa tukio hilo, ..wanasema walivyomuhoji, alivyojieleza inaonekana kama analifahamu hilo tukio na yeye alikuwa mwenza wao, japokuwa alikana kabisa.
Baadae akafunguliwa mashitaka, na yote hayo wakati yanaendelea mimi nilikuwa sifahamu kinachoendelea kwani ilibidi niondoke hapo kijijini kwa usalama wangu, kwa vile walitishia kuwa ni lazima watanifanyia tena..ikabidi baadae wazazi wangu wanihamishe kabisa kwenda kusomea sehemu nyingine.
Nilikuja kusikia kuwa kijana huyo kafungwa, na nilikuja kufahamu hilo baada ya muda, mtu alishahukumiwa kufungwa..kwani vijana wale waliofanya hivyo hawakuweza kupatika,ila mmoja wao alipatikana na alipofika mahakamani, akadai kuwa kijana huo alikuwa mmoja wa wenzao, walipanga wote, kulifanikisha hilo, nay eye ndiye alitoa maelekezo jinsi gani wanaweza kumpata huyo bint.
Baba wa huyo kijana akawa anafika mara kwa mara kwa wazazi wangu kuomba kijana wake asamehewe, lakini haikusaidia kitu, na alichoambulia ni kufukuzwa kazi...hayo yote nilikuja kuyafahamu baadaye, na nilipolifahamu hilo nikawaambia wazazi wangu kama hawatamuachia huyo kijana aliyeniokoa basi mimi nitajiua...
Hilo nilidhamiria kweli…
Kumbukumbu za nyuma ziliuteka ubongo wangu,…nikakumbuka yaliyotokea huko nyuma, yaliyompata huyu msamaria mwema, tena kwa ajili yangu, akafikia hadi kufungwa na wazazi wangu, …nikaapa kuwa siku nikikutana naye, nitajitahidi nifanye lolote kumlipa fadhila zake, sasa nitamlipa nini, …na nilishamsahau, nikujua hayupo tena duniani…na siku hiyo, ndio nikakutana naye, nikiwa na docta mtoto wa watu akiwa ni mpenzi wangu…je nilifanya nini, angalia mitihani hii ya maisha…
***********
Nakurejesha nyuma kipindi nikiwa binti mdogo, wa miaka kumi na tano,…kipindi hicho ndio nilimuona kijana mmoja mara kwa mara akiwa anakuja kuonana na mzee mmoja aliyekuwa mlinzi wa nyumba yetu. Yeye kiumri alikuwa mkubwa kuliko mimi…nikaanza kuzoeana naye tu..
Kuna kipindi baba yake alikuwa akitulimia shamba, basi na yeye anakwenda kumsaidia baba yake mimi, nikawa nafika shamabi kuchukua matunda, nawakuta wakiwa wawili, nawapatia chochote, mwanzoni sikuwa naongea naye sana, kutokana na hali ilivyokuwa wakati huo. Wazazi walikuwa wakali hawakupenda kabisa nizoeane naye, au kuwa karibu naye,…
Kila huyo mvulana akija, nilimgundua akiniangalia sana, na ikitokea tukikutanisha macho anayakwepesha kwa haraka na kujifanya kama alikuwa haniangalii, ikawa kama mchezo fulani wa utu-rika,.. na tukajikuta tunamezoeana kinamna hiyo, lakini sio ile ya ukaribu ya kukaa pamoja na kuongea.
Ni ikaja muda hata mimi nikikaa nyumbani, namuwaza yeye, fikiria ni mtoto wa mkulima, mfanyakazi wetu tunaweza kusema wa ndani…lakini mimi sikulijali hilo, nilimuona sawa na wavulana wengine. Sio kwamba nilikuwa na tabia mbaya, ya kuwa na mazoea na wavulana, hapana..ila nilijali sana usawa na utu, hata nikiwa msichna mdogo.
Basi kwa ile hali ya kunyanyapaliwa na wazee, kuwa wakifika wanakuwa na sehemu yao, hawaruhusiwi kuingia ndani, sikulipenda hilo kabisa, nikaona lazima nifanye jambo, la kuwasaidia hawa watu wawili…nilimjali sana huyo baba yake, alikwua na tabia nzuri tu,…huruma na upendo,.
Basi…huyo kijana akifika, ninajua wapi nikae ili aweze kupita na kuniona, kwa haraka nikakuwa na zawadi yoyote ya kumpa, chakula au matunda,…maji ya baridi ili wakinda sahamba wapate kuyatumia yeye na baba yake..na nilijithidi sana wazee wangu wasiweze kuona hayo…
Lakini ikatokea tukio, liloharibu kila kitu, na baada ya tukio hilo, tukaachana na familia hiyo sisi baadaye tukahama na kuja kuishi Dar, ambapo baba yangu alihamishia kampuni yake, na huko kijijini tukawa hatufiki mara moja moja tu. Na sikuweza kuwaona tena. Tukio hilo kwakweli liliniumiza sana kiasi kwamba niliwaona wazazi wangu kama ni watu wasio na utu-wema.
*************
‘Kwanini hukunitafuta, ulipoachiwa kutoka jela...?’ nikamuuliza, nikikatiza mawazo yangu ya kumbukumbu za huko kijijini….
‘Kwanini nikutafute..ulitaka niendelee kuumia, maana mimi ningelisemaje kwako, ..hebu nijishushe hapo, baada ya tukio lile, ningelionekana na wewe tena, si ndio ningepeleka tena jela nikafie huko.., nakumbuka niliwahi kuandika barua kuja kwako, lakini sikuwahi kupata majibu...’akasema.
‘Barua,…. hahaha..nani ana mipango ya barua siku hizi, ulindika hiyo barua kuja kwangu ukampa nani..mbona sijawahi kuona barua yako yoyote,...?’nikamuuliza, niliona kama ananitania tu.
‘Basi nahisi kuna mtu alikuwa akizipokea na kuzichana, mimi niliandika, nyie si mna box la barua, na kuna mtu alisema anakuja huko kwenu , nikampa barua, lakini nikajua umeshatekwa na familia yako, na huenda hata wewe hutaki hata kuniona tena, kwa jinsi watu walivonivumishia ubaya....’akasema akitikisa kichwa kusikitika .
‘Kwanini usingelinipigia, angalau hata simu...?’ nikamuuliza
‘Nikupigie simu!!! Hahaha…, simu hiyo ningeliipata wapi, huko kijijini, hivi unayafahamu maisha yetu yalivyokuwa...anyway, hayo yameshapita na wewe una mume wako, ...naona nisikupotezee muda, ...’akasema na kutaka kuondoka, mimi nikamshika mkono asiondoke.
‘Nimeshakuambia yule sio mume wangu, ni mchumba wangu, hatujaoana bado…Sikiliza, ..ahadi yangu ipo pale pale…’nikasema na hapo akaniangalia kwa macho yenye kushangaa.
‘Kwahiyo unataka kusema nini…?’ akaniuliza
‘Ahadi yangu ya kufanya lolote ilimradi niwe nimelipa fadhila zako, najua inaweza isikidh haja, lakini angalau na mimi niwe nimfanya jambo kwako la utu wema..sasa mimi nataka tuje tuongee tena nione nitakufanyia nini…’nikasema, na nikaona kama ananywea, hakuridhika na maneno yangu hayo.
‘Hapana, mimi sihitajii msaada wako, sitaki kuwa mfanyakazi wenu, au ….kuwategemea nyie tena, hapana…hilo sitaki, …’akasema
‘Najua ni kwanini unasema hivyo, ila mimi natamani zile siku zirejee tena, kiukweli mimi sijaolewa, na sisemi hivyo kwasababu kuwa nataka uwe ...mpenzi wangu, hapana mapenzi hayalazimishwi, na…mimi na mchumba wangu hatujafikia huko, bado kuna mipango mimi, yeye na mimi pia, lakini mimi ninaweza kufany ajambo la kukusaidia ukafika mahali, usilipuuzie hilo..’nikasema
‘Hilo la kukutana kuongea tena, ni wewe, kama huogopi huyo mpenzi wako, sitaki kuja kuwaharibia mahusiano yenu, ikawa ndio sababu ya kufichua yale yaliyopita, sipendi hilo kabisa,…’akasema
‘Kiukweli unanidai sana, mengi umenifanyia, lakini sijaweza kulipa chochote kwako, kwangu mimi naona ni deni, na nataka uwasamehe wazazi wangu, hata bila ya wao kufahamu, na hilo naweza kufanya nionavyo mimi, niamini tu,…usijali kabisa kuhusu hisia za wazazi wangu, nafahamu ni kwanini wanafanya hivyo,....’nikasema
‘Hahaha, hapana , niliapa kuwa sitaajiriwa kwa watu kama mfanyakazi wa upendeleo, mimi nataka nihangaike kivyangu…sawa nashukuru kwa kuonana nawewe, mengine tuyaache kama yalivyo, vipi maisha na mchumba wako, katulia siku hizi..?’ akaniuliza
‘Mchumba wangu hana matatizo, ni mzungu kwakweli, muhimu nimuambie ukweli tu, hata akiniona tunaongea, yeye atadai nimuambie wewe ni nani, na ni hivyo, sina shaka naye, ila hayo hayana msingi, wewe sifikiria wako langu la kukuwezesha, unalionaje hilo…’nikasema
‘Mhh…sivyo nitakavyo, najua hutanielewa, ndio maana nasema tuyaache tu, yabakie kama yalivyo, kwa maana mimi nilikufanyia nini kikubwa, ni kawaida tu, na yaliyotokea hadi wazazi wako kufanya hivyo, ni…naweza kusema hata mzazi mwingine huenda angelifanya hivyo…’akasema
‘Hapana lile tukio lilikuwa kubwa, na kiukweli nakiri wazazi wangu walikosea, sana,..maana hawajui ulivyofanya, uliweza kuniokoa mikononi mwa wabakaji, mijitu mikubwa, na wewe ulikuwa sio umbile lako kabisa, ukapigana na wao kufa na kupona, hawakuliona hilo.
Kiukweli mimi..sitalisahau hilo kamwe, nilikuona kama mtu maalumu sana kwenye maisha yangu ndio maa niliahidi siku nikikutana nawe, nitafanya lolote lililondani ya uwezo wangu, ili na wewe uone kuwa nakujali…...’ nikamwambia.
‘Mhh…nilishaipata hiyo zawadi inatosha., wewe wasalimie wazazi wako na mchumba wako, mungu akipenda tutakuwa tunaonana, lakini nisingelipenda wafahamu kuwa tumekutana nafahamu watakavyojisikia, huenda ikaja dhahama kubwa zaidi ya ile…japokuwa sasa nimekuwa mkubwa siogopi, nafahamu haki zangu...’akasema
‘Jamani ina maana hujatusamehe tu…’nikasema
‘Usijali sana ndio ubinadamu ulivyo,..nilishawasamehe mbona…kwa hivi sasa nimeliona hilo, kuwa yale waliyoyafanya wazazi wako walikuwa na maana kwao, kwa ajili ya kulinda heshima ya familia yenu, na walitaka kutoa fundisho kwa jamii, na nasikia familia yenu imekuwa ikiogopewa sana,..ni sahihi, yamepita yapite.
‘Tatizo wewe hufahamu jinsi gani niliumia...lakini ikafika mahali nikasema basi tena, mungu ndiye atakupeni yale yote mliyotutendea wewe na baba yako, na nikatubu sana kwa niaba ya wazazi wangu…kiukweli baba yako nilimuona kama baba yangu mkubwa...sikupenda kumuita babu, kama walivyozoea kumuita wengine, mimi ninajua kuzeeka kwake haraka ni kutokana na hali ya maisha, umri wake haupo mbali na umri wa baba yangu, …mimi nilipenda kumuita baba mkubwa.....’nikasema.
‘Nashukuru kusikia hivyo, ni wewe tu ulikuwa tofauti na wengine, sijui kwanini wazazi wako, walikuja kutuchukia hivyo..niliona kabisa hawakupenda, hata nikukaribie..na nahisi ilipotokea lile tukio, ndio wakaonyesha hisia zao dhidi yangu. Ni sawa, labda nisiwalaumu sana, maana huenda hata sisi tungelikuwa kwenye hiyo hali tungelifany ahivyo hivyo..hata hivyo nawashukuru wazazi wako, kwani pamoja na hilo tukio lakini walitusaidia sana kimaisha...’akasema.
‘Mimi nilikutafuta sana, lakini sikutaka wazazi wangu walifahamu hilo, nilitaka kukulipa fadhila zako, niliahidi moyoni kuwa nikija kuonana na nawewe, nitafanya lolote na nimekkuona naomba usilipinge ombi langu....’nikamwambia.
‘Mimi sihitaji msaada wenu, ….’akasema
‘Hapana ni lazima nifanye wema wowote, nakumbuka kama isngelikuwa ni wewe..sijui ingelikuwaje, na….’hapo tena ndio lile tukio likazama kwenye ubongo wangu nikawa naliona lilivyotokea….
**********
Ilionekana wazo hao vijana watukutu, walikuwa wakinivizia siku nyingi, na siku hiyo gari la baba lilichelewa kuja kunichukua shuleni, nikaamua kutembea na wenzangu, na kwa vile shule ilikuwa mbali, wenzangu wakawa wametawanyika kila mmoja na njia yake, ikafikia mahali nimebakia peke yangu, na ghafla ndio nikavamiwa na vijana wanne, na kunibeba juu kwa juu.
Walinibeba juu kwa juu, hadi vichakani, na wakaanza kunivua nguo, na ukumbuke nilikuwa binti mdogo tu, nasoma sekondari..nilikuwa binti, nimeshavunja ungo, lakini sikuwa na mawazo hayo kabisa, na sikujua ni kitu gani kitakuja kunitokea,..japokuwa nilifahamu kuwa wanatka kunifanya kitu kibaya.
Nilijitahidi kupigana lakini sikuweza kufurukuta kwa vijana hawa wenye nguvu zaidi yangu, na kabla hawajafanya lolote mara akatokea mtu, kijana..machozi yalishatanda usoni sikumuone vyema, akawa anapigana nao, akiwa na kigongo hivi kama rungu, alipambana nao kiume mpaka anakuja kuwazidi nguvu, ilikuwa ni kwa msaada wa mungu tu maana wote walikuwa wakibwa zaidi yake…ikafikia muda, ikabidi wakimbie, baada ya kusikia kelele za watu, wakikaribia eneo hilo..na yule kijana akapiga ukelele kuomba msaada. Wale vijana wakakimbia huku wakilaani kuwa watahakikisha wananifanyia hivyo, siku yake...
Sikuweza kuongea nililia hadi nyumbani, nikiwa nimechafuka, nguo zimechanwa, nnipo kama nudu uchi…na huyo kijana alinsiindikiza hadi nyumbani, nikawahadithia wazazi wangu, na wao kwa haraka wakaifahamisha polisi na hawo vijana wakaanza kutafutwa lakini hawakupatikana kwa siku hiyo hata ya pili yake. Walihama kabisa, kijini hapo.
Cha ajabu wazazi wakaongea na polisi wakaja kumshikilia huyo kijana kuwa atakuwa anawafahamu hawo watu, na alitakiwa kuwataja, na aliposhindwa kuwataja, wakamshitakia kuwa ni muhusika wa tukio hilo, ..wanasema walivyomuhoji, alivyojieleza inaonekana kama analifahamu hilo tukio na yeye alikuwa mwenza wao, japokuwa alikana kabisa.
Baadae akafunguliwa mashitaka, na yote hayo wakati yanaendelea mimi nilikuwa sifahamu kinachoendelea kwani ilibidi niondoke hapo kijijini kwa usalama wangu, kwa vile walitishia kuwa ni lazima watanifanyia tena..ikabidi baadae wazazi wangu wanihamishe kabisa kwenda kusomea sehemu nyingine.
Nilikuja kusikia kuwa kijana huyo kafungwa, na nilikuja kufahamu hilo baada ya muda, mtu alishahukumiwa kufungwa..kwani vijana wale waliofanya hivyo hawakuweza kupatika,ila mmoja wao alipatikana na alipofika mahakamani, akadai kuwa kijana huo alikuwa mmoja wa wenzao, walipanga wote, kulifanikisha hilo, nay eye ndiye alitoa maelekezo jinsi gani wanaweza kumpata huyo bint.
Baba wa huyo kijana akawa anafika mara kwa mara kwa wazazi wangu kuomba kijana wake asamehewe, lakini haikusaidia kitu, na alichoambulia ni kufukuzwa kazi...hayo yote nilikuja kuyafahamu baadaye, na nilipolifahamu hilo nikawaambia wazazi wangu kama hawatamuachia huyo kijana aliyeniokoa basi mimi nitajiua...
Hilo nilidhamiria kweli…