Mkurugenzi amsimamisha kazi Mwalimu aliyewatuma wanafunzi kupakia kuni zake wakapata ajali

Mkurugenzi amsimamisha kazi Mwalimu aliyewatuma wanafunzi kupakia kuni zake wakapata ajali

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mkurugenzi amsimamisha kazi Mwalimu aliyewatuma wanafunzi kupakia kuni zake wakapata ajali ya gari
IMG-20231004-WA0018.jpg
Njombe

Mwalimu Furaha Msule anayefundisha shule ya Sekondari Kidegembye iliyopo Lupembe halmashauri ya wilaya ya Njombe amesimamishwa kazi kwa kosa la kuwachukua wanafunzi na kuwapeleka kupakia kuni zake kinyume na sheria na kupelekea kupata ajali ya gari wakati wakirudi majira ya saa moja usiku.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Christopher Sanga ameeleza kumsimamisha kazi mwalimu Msule na kutoa wito kwa watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu.

"Ofisi ya mkurugenzi kwa kushirikiana na tume ya walimu TSC imechukua hatua ya kumsimamisha kazi mwalimu aliyehusika huku utaratibu,sheria na kanuni zingine zikiendelea"amesema Sanga

Sanga amesema mnamo October,1,2023 ofisi yake ilipokea taarifa ya kutokea ajali ambapo mwalimu Furaha aliwachukua wanafunzi na kwenda kupakia kuni zake lakini kwa sasa wanafunzi wote 11 wakiwemo 6 waliokuwa wakitibiwa katika hospitali ya Kibena wameruhusiwa na kurejea shuleni.
 
Nilimsikia juzi Dr Msonde akiongea walimu anasema mbona walimu wa Sasa wamekuwa hivi walivyo?Msonde analalamika Wanafunzi hawajui kusoma wala kuandika ,hivi unafikiri Kwa tangazo Hilo la mkurugenzi unafikiri mwalimu atafanya nini zaidi ya kwenda kufanya umbea shuleni na kurudi nyumbani kwake!!
 
Tuliwahi kupelekwa na Mwalimu mmoja kupakua asali mchana wa jua kali moto tuliokuwa tunawaleweshea nyuki ukatushinda ukatoroka msitu wa watu ukaanza kuungua, kumbe hata hao nyuki hawakuwa wake, tuling'atwa tukarudi nyumbani tumevimba macho hayaoni, mchana huohuo Mwl alitoroka hatukuwahi kumwona tena
 
Mkurugenzi amsimamisha kazi Mwalimu aliyewatuma wanafunzi kupakia kuni zake wakapata ajali ya gari
View attachment 2772019
Njombe

Mwalimu Furaha Msule anayefundisha shule ya Sekondari Kidegembye iliyopo Lupembe halmashauri ya wilaya ya Njombe amesimamishwa kazi kwa kosa la kuwachukua wanafunzi na kuwapeleka kupakia kuni zake kinyume na sheria na kupelekea kupata ajali ya gari wakati wakirudi majira ya saa moja usiku.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Christopher Sanga ameeleza kumsimamisha kazi mwalimu Msule na kutoa wito kwa watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu.

"Ofisi ya mkurugenzi kwa kushirikiana na tume ya walimu TSC imechukua hatua ya kumsimamisha kazi mwalimu aliyehusika huku utaratibu,sheria na kanuni zingine zikiendelea"amesema Sanga

Sanga amesema mnamo October,1,2023 ofisi yake ilipokea taarifa ya kutokea ajali ambapo mwalimu Furaha aliwachukua wanafunzi na kwenda kupakia kuni zake lakini kwa sasa wanafunzi wote 11 wakiwemo 6 waliokuwa wakitibiwa katika hospitali ya Kibena wameruhusiwa na kurejea shuleni.
Hii kazi sio poa

Walimu wakibweteka wanatukanwa (mshahara wa barmaid na watakufa maskini)

Wakijiongeza inakuwa shida, basi kila kitu ni shida
 
Hii kazi sio poa

Walimu wakibweteka wanatukanwa (mshahara wa barmaid na watakufa maskini)

Wakijiongeza inakuwa shida, basi kila kitu ni shida
Unajiongeza na watoto wa watu muda ambao wanatakiwa wajisomee wafanye vizuri ktk mitihani yao?
Angalau angetangaza kibarua cha kuwalipa ujira ningekuelewa kidogo ingawa bado ni kosa.
 
Hili suala la Walimu shule za Serikali, hasa vijijin kuwatumia wanafunzi Kwa shughuli zao binafsi, kama vile kilimo, kufatiwa maji ,Kuni , kufanyiwa usafi Majumbani kwao ,n.k.

Likomeshwe Mara Moja.
Nawaonea huruma sana coz wanakula uchafu,hasa maji madogo wanatemea mate[emoji23][emoji23][emoji23],
 
Tuliwahi kupelekwa na Mwalimu mmoja kupakua asali mchana wa jua kali moto tuliokuwa tunawaleweshea nyuki ukatushinda ukatoroka msitu wa watu ukaanza kuungua, kumbe hata hao nyuki hawakuwa wake, tuling'atwa tukarudi nyumbani tumevimba macho hayaoni, mchana huohuo Mwl alitoroka hatukuwahi kumwona tena
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nilifika shule mmoja mi na mwenzangu kuanza kazi ya kufundisha, tulikuta wenyeji wetu wakatupokea tukawa tunaachiana zamu kupika wawili wawili. Mchana tukawa tunapikiwa na wanafunzi wa kike wakubwa wawili. Walimu wawili walihama kambi tukabaki wawili na utaratibu wetu wa kupikiwa mchana na kuchotewa maji. Mwisho nilibaki mwenyewe nikaona isije kuwa balaa nikaachana na utaratibu wa kuhudumiwa na wanafunzi tena wanafunzi wenyewe wa kike wamekamilika kila idara miilini mwao. Pamoja na ku sense danger na kuachana kuwatumia wanafunzi lilipangwa jaribio la kunipakazia kuwa nawachakata wanafunzi hao, hao hao wanafunzi wakipangwa watoe ushaidi mbele ya school baraza. Ilikuwa nipakaziwe kashfa ya kulabua wanafunzi ila kashfa hiyo ilipanguliwa kwa nguvu zote na wanafunzi wenzao walioona nafanyiwa njama kwa chuki tu toka kwa walimu wenzangu niliowazidi kufundisha kwa weledi mpaka wanafunzi wakanipenda ikawa wivu
 
Mkurugenzi amsimamisha kazi Mwalimu aliyewatuma wanafunzi kupakia kuni zake wakapata ajali ya gari
Njombe

Mwalimu Furaha Msule anayefundisha shule ya Sekondari Kidegembye iliyopo Lupembe halmashauri ya wilaya ya Njombe amesimamishwa kazi kwa kosa la kuwachukua wanafunzi na kuwapeleka kupakia kuni zake kinyume na sheria na kupelekea kupata ajali ya gari wakati wakirudi majira ya saa moja usiku.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Christopher Sanga ameeleza kumsimamisha kazi mwalimu Msule na kutoa wito kwa watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu.

"Ofisi ya mkurugenzi kwa kushirikiana na tume ya walimu TSC imechukua hatua ya kumsimamisha kazi mwalimu aliyehusika huku utaratibu,sheria na kanuni zingine zikiendelea"amesema Sanga

Sanga amesema mnamo October,1,2023 ofisi yake ilipokea taarifa ya kutokea ajali ambapo mwalimu Furaha aliwachukua wanafunzi na kwenda kupakia kuni zake lakini kwa sasa wanafunzi wote 11 wakiwemo 6 waliokuwa wakitibiwa katika hospitali ya Kibena wameruhusiwa na kurejea shuleni.
Sidhani kama huyu Mkurugenzi yuko Timamu..
 
Mnahangaika na kelele za Katiba wakati sheria zenyewe mpaka paharibike kitu ndio mnafuata sheria, acheni unafiki na ujinga
Waalimu wangapi wanalimiwa mashamba ila mpaka mtoto aumwe na nyoka au afe ndio mnajua hayo

Wafungwa wanalima mashamba ya mabosi wao kila kukicha ila mpaka mmoja atoroke ndio tunajua
Halafu mnataka katiba tu
 
Back
Top Bottom