DOKEZO Mkurugenzi wa AUWSA asaini Mkataba wa kifisadi wa TZS 36.3 Bilion na Mchina bila Ridhaa ya Bodi ya Ununuzi ya AUWSA na wafadhili AfDB

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Shamba la bwana heri,na ngombe wa bwana heri!!watu Wana kula kwa urefu wa kamba!!
Pesa tamu jamani,ukizicheki hizo billions,harafu ukajua kabisa,ukicheza kama Pele hapa,ukosi milioni 50+!!lazima utajilipua,maana kichwani unakuwa unaona Vogue lileee!!apartments zangu zileeee!!unaona kampuni yako ya logistic ileeee???!!!
Nchi hii ni tamu na chungu,inategemea upo wapi,
 
Mkuu Moshi town, thanks for this, it's a good whistle blowing article. Huu ndio uzalendo wa kweli kwa nchi yako!.
P
 
Yani hao jamaa waya zishatembea na msainishaji amefanya hilo kwa kujiamini kwamba wanaipiga hio 16B iliozidi hapo. Sijajua kwenye mgao itakuwaje ila kuanzia waziri hadi huyo mkurugenzi wanakula share ya zaidi ya billion kila mmoja wao.
Hii inaenda kwa kwa Waziri wa fedha mkuu kila mtu analamba
 
Kama ni kweli basi atakuwa na cover inayomlinda la sivyo angekuwa anachungulia kwenye dirisha dogo
 
Kama ni kweli basi atakuwa na cover inayomlinda la sivyo angekuwa anachungulia kwenye dirisha dogo
Dili ya hela ndefu huwezi kula mwenyewe. Hio ni chain ya wahuni 😂😂😂 yani hapo hafungwi mtu. Kwa huo mzigo mahakama gani itakufunga hapa nchini? Jaji akilamba 500m tu wote mnapeta uraiani!
 
Yani hao jamaa waya zishatembea na msainishaji amefanya hilo kwa kujiamini kwamba wanaipiga hio 16B iliozidi hapo. Sijajua kwenye mgao itakuwaje ila kuanzia waziri hadi huyo mkurugenzi wanakula share ya zaidi ya billion kila mmoja wao.
Ni Genge la viongozi wengi wapigaji kuanzia Waziri wa
maji Aweso, KM wa
maji Eng Sanga Mkurugenzi wa Maji Mjini Mama Msiri, Kamanda wa PCCB Mkoa Ruta, Mwakilishi wa AFDB Tanzania anayesimamia Miradi ya Maji Eng Rwetabula
 
Majungu
 
Ni Genge la viongozi wengi wapigaji kuanzia Waziri wa
maji Aweso, KM wa
maji Eng Sanga Mkurugenzi wa Maji Mjini Mama Msiri, Kamanda wa PCCB Mkoa Ruta, Mwakilishi wa AFDB Tanzania anayesimamia Miradi ya Maji Eng Rwetabula
Organized Crime ndio inayolitesa hili taifa kwa sasa. Inauma sana ikiwa kuna watu hata kula yao ni ya tabu wengine kufia reception kwa kukosa huduma halafu unaskia taarifa kama hizi kuwa kuna wana wamepiga billions na wamegawana
 
Kuna upotofu mkubwa wa hili jambo, siwezi kuelezea yote ila mtoa mada hajui mikataba hii mikubwa sii sawa na miradi ya mamlaka ya maji. International tender na tender docs ni tofauti.
 
Kuna upotofu mkubwa wa hili jambo, siwezi kuelezea yote ila mtoa mada hajui mikataba hii mikubwa sii sawa na miradi ya mamlaka ya maji. International tender na tender docs ni tofauti.
Itakuwa wewe ndiyo haujui Sheria ya mikataba Kimataifa.

Sheria ya Mikataba ya kimataifa inaelekeza Zabuni kutangazwa ili apatikane Mshindi halali,

Zabuni ya Construction of water blending system for FLOURIDE reduction aikutangazwa na Mkandarasi kampuni ya China Sinohydro wamepatiwa zabuni bila kupitishwa na Bodi ya Zabuni ya AUWSA ( AUWSA Tender Board) ,

Sheria ya zabuni inaitaji kabla ya Mkandarasi kusaini Mkataba unaozidi 1 Bilion Mkataba uende kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya Veting hii aikufanyika , Mkataba umeandaliwa na Mchina Eng Rujomba akasaini bila hata ya kupata Ushauri wa Wanasheria wa AUWSA Advocate Sabas na Namayani, Kwa Lugha Raisi Mkataba umesainiwa bila kufanyiwa Vetting na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Mkataba Umesainiwa bila kupata No Objection kutoka AFDB, Sheria inaitaji kabla ya Mkataba Kusainiwa PE ( AUWSA) itume taarifa ( Evaluation report) kwenda wa Donor ( AFDB) kumfaamisha Mchakato umefanyika kwa kufuata Procedure zote za Tender kwa maama Tender Imetangazwa, Evaluation team wamepitia na Tender Board imekaa na Kuridhia, Haya yote ayakufanyika na hadi leo AFDB wamegoma kutoa barua ya No Objection..

Mkataba umesainiwa kisiri Siku ya
Ambayo siyo ya kazi Tarehee 7 Julai
2022 Lengo ikiwa ni isigundulike.. Sheria
Inataka mikataba isainiwe siku ya kazi na kwa uwazi and not otherwise.

Mkataba umesainiwa bila kushuudiwa na Wajumbe wa Bodi ya AUWSA

Mkataba Umesainiwa bila kushuudiwa na Management

Gharama za Ujenzi umeongezeka kutoka 20 bilion hadi 36 bilion kuna ongezeko la 16 bilion.. Mkandarasi Mshauri ( Consultancy) kampuni ya Cheil consultancy iliandaa BOQ ya Ujenzi wa Mradi iwe Tzs 20 bilion Engineer Rujomba amesaidi Tzs 36 bilion.

Project Manager Eng Mkawe Akushirikishwa katika Process ya kumtafuta Mkandarasi hii ni hatari inakuwaje MD na HPMU wanafanya Proces ya Kumtafuta Mkandarasi na kusaini Mkataba Project Manager hana taarifa?

Huu Mkataba ni kama Richmond , Mwaka 2008 Karamagi alisaini mkataba kisiri na kampuni ya Richmond Siku ya Public Holiday Nje ya Nchi.
 
Kuanza kukuelimisha humu ndani ni shida haya endelea na mapambano yako yasiyo na mashiko unapoteza muda kwa kutokujua contract. Jua tu sio contract zote zinatawaliwa na PPRA na specifications zake.
 

Haiwezekani DG awe mzembe hivyo asaini mkataba wa Bil 38 bila bodi ya manunuzi kuidhinisha... Labda kuna kitu kipo nyuma ya pazia hujui
 
Haiwezekani DG awe mzembe hivyo asaini mkataba wa Bil 38 bila bodi ya manunuzi kuidhinisha... Labda kuna kitu kipo nyuma ya pazia hujui
Issue kubwa hapa sio hizo management procedure ni uhalali wa mkataba husika accoding to the contract husika (AfDB/FIDIC contract documents je inaruhusu jambo hilo ( threshold = should be less or equal to 25% of the original contract) Je hili lilizingatiwa hayo mengine yote siasa na husuda tu.
 
Mradi wa Ujenzi wa New Water System ni tofauti kabisa na Construction of water blending system for FLOURIDE reduction

Kwa akili ya kawaida utampatiaje Mkandarasi wa New water System Kandarasi ya kujenga Construction of water blending system for FLOURIDE reduction kuwa ni Extension of Work?
 
Haiwezekani DG awe mzembe hivyo asaini mkataba wa Bil 38 bila bodi ya manunuzi kuidhinisha... Labda kuna kitu kipo nyuma ya pazia hujui
Nina uhakika 100% hii tender aikupita Tender Board na Mkataba umesainiwa bila Kibali kutoka kwa Mfadhili AFDB (No Objection)

Kuna Fisadi Mmoja yupo AFDB Ofisi ya Tanzanina anaitwa Eng Rutabula anawadanganya kuwa atasimamia kila kitu wapate No Objection . Huu ufisadi ni kama Richmond
 
Kuanza kukuelimisha humu ndani ni shida haya endelea na mapambano yako yasiyo na mashiko unapoteza muda kwa kutokujua contract. Jua tu sio contract zote zinatawaliwa na PPRA na specifications zake.
Tender ya Ujenzi wa ofisi za Kanda AUWSA ya Tzs 5 bilion ilitangazwa kwanini Tender ya 36 bilion aikutangazwa?

Zabuni ya Kujenga Vyoo vya kisasa vya Tzs 1.5 ilitangazwa kwanini tender ya TZs 36 bilion aikutangazwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…