Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa NEC, Dkt. Mahera apumzishwe haraka, anaweza kutupeleka kwenye matatizo makubwa

Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa NEC, Dkt. Mahera apumzishwe haraka, anaweza kutupeleka kwenye matatizo makubwa

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Kila ninapomsikiliza huyu Mkurugenzi napata wasiwasi kabisa na uwezo wake wa kuifanya tume ya uchaguzi ikafanya haki. Kwanini isichukuliwe kuwa yeye ndiye chanzo cha hizi engua engua?

Huyu si watu wengi wanamtuhumu kuwa ni kada wa CCM? Si ndio kuna tuhuma kuwa alikua kwenye list ya Wakurugenzi Makada wa CCM iliyoandaliwa na Bibi Chacha Wangwe na Fatma Karume?

Kwani wagombea kutunishiana misuli na kukejeliana majukwaani nyakati za kampeni si kawaida?

Kwenye uchaguzi huwezi kupanga kusikiliza unayoyataka wewe, hakuna kitu cha namna hiyo labda ugombee wewe pekee yako.

Huyu bwana ajifunze kwenye tume za kina nani Damian Lubuva. Alitukanwa sana mzee Lowassa lakini hatukuona mtu akiitwa kwenye kamati za maadili.

Nimemsikiliza mara nyingi mwenye vikao vyake na vyombo vya habari inaonekana ni mtu asiyekipenda kabisa CHADEMA na mgombea wake.

Huyu tusipoangalia anàweza kuleta matatizo makubwa nchini siku za usoni. Awe makini sana NEC ni chombo kinachotazamwa na Jumuiya zote za kimataifa, asiongee kama bado yupo Arusha DC.

Amesikika akisema kila kila wakati kuwa tume haishinikizwi kutoka nje, hii kauli inalenga nini hasa? Ni nje ya wapi inataka kuishinikiza tume na kupitia nani?

Nasikitishwa na upinzani wa nchi yetu kwanini wasingeshinikza huyu bwana aondolewe kwenye tume kabla ya uchaguzi? Wanamuamini kwa kiasi gani kutokana na kauli zake hizi?
 
Kila ninapomsikiliza huyu mkurugenzi napata wasi wasi kabisa na uwezo wake wa kuifanya tume ya uchaguzi ikafanya haki. Kwanini isichukuliwe kua yeye ndiye chanzo cha hizi engua engua?...
Hii tume ambayo msingi wake mkubwa ni double standards...Tundu Lissu asiende tuone kitakochofanyika.

Hii tume ambayo yenyewe haina maadili...ninewupe kama pamba. Wametoa hukumu gani kwa wagombea ubunge na udiwani wa CHADEMA kwa muda huu wote. There are all working in tandem with all the deds to ensure that winner is Magufuli.
A bunch of sycophants dancing at magufuli's tune all the time.

Magufuli has breached all the codes or regulations of this election and nothing has been said or done against him.

He has not followed the timetable during the electioneering, speaking in the local dialect as he pleases during this campaign, dealing with construction of road projects during the campaign, giving money to people.

This is absurd and yet no significant statement has come from NEC to condemn what Magufuli is doing. The only help we need is ICC at the Haque.
 
Mahera anashikilia nafasi nyeti ya kitaifa. Na alitakiwa aonyeshe yupo 'neutral' wakati anatoa tangazo la kumuita Tundu ajieleze. Naona ametoa tangazo kwenye vyombo vya habari kwa papara na hasira na hiyo imeleteleza kujianika wazi kuwa ana upande. Mbona hakukasirishwa na mgombea kujinadi kwa lugha za kikabila? Mbona hakukasirishwa na mgombea kutisha wapiga kura wasipomchagua?
 
Kila ninapomsikiliza huyu mkurugenzi napata wasi wasi kabisa na uwezo wake wa kuifanya tume ya uchaguzi ikafanya haki. Kwanini isichukuliwe kua yeye ndiye chanzo cha hizi engua engua?...
Hajishtukii mwenzake Jaji Kaijage kajikalia kimya tu yeye ndo analopoka hovyo. Keshaingia kwenye records za wenye dunia na saivi wanamfuatilia 24/7. Andelee kujifanya mjinga hajui kinachokuja mbele yake
 
Mimi naona TUME kumwita TAL ni kumuongezea umaarufu. Wana muhujumu Magufuli. JPM anatakiwa awe makini na hatua hizi. Kwa sababu kimsingi JPM amevunja kanuni nyingi za uchaguzi kuliko TAL. Hivyo alitakiwa aitwe kwanza. TAL ataenda kuwatoa jasho wabaki na aibu
 
Huyo hapo tume ataleta vurugu nchii hii mimi nimemwona tangu zamani sana. Huwa kuna watu wenye roho fulani wasio na utu ndio wanawekwa maeneo kama hayo. Watu hawa hawana utu wala aibu. Huwezi kumweka pale tume mtu mwaninifu na mwenye akili zake timamu hataweza kufanya ushenzi unaotakiwa pake. Na huyu ana nguvu kuliko hata Jaji Semistocles.
 
Watanzania ni watu wanafiki na watu wa kuburuzwa tu

Hata Kama mambo hayako sawa utasikia tu wakisema hali iko sawa tu
 
Tataizo NEC huwa wanawekwa watu ambao hawakuwa na matumaini yoyote, Mahera alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri lakini hajitambui mpaka DC wake Muro alikuwa anamtukana hadharani kwasababu ya Umbumbumbu
 
Back
Top Bottom