Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Hivi huyu aliokotwa wapi na kupewa hiyo nafasi? Tume ilihitaji mtu kama Prof Assad,

Ukiona mtu yoyote ni mteule wa Magufuli, ujue moja kwa moja anafuata atakacho na sio sheria zitakavyo. Na ukienda kinyume tu cha matamanio yake, hata kama unasimamia sheria lazima akuondoe.
 
Kwani mgombea wa chama changu ametoa tuhuma gani? Mkurugenzi asituonee
 
Ukiona mtu yoyote ni mteule wa Magufuli, ujue moja kwa moja anafuata atakacho na sio sheria zitakavyo. Na ukienda kinyume tu cha matamanio yake, hata kama unasimamia sheria lazima akuondoe.
Mkuu nchi hii inaendeshwa KIDIKTETA sana we acha tu!
 
Mbona mkurugenzi kama sio kazi yake hii??
 

Asimfundishe mgombea cha kusema kwenye kampeni wala asianze kupigia kampeni CCM. Abakie na huo ukada wake kila mtanzania anayejitambua anajuwa kwamba tume inapendelea CCM tangu mwanzo kabisa
 
Asiwafundishe watanzania nini wanahitaji
 
TUME ya uchaguzi haina mamlaka ya kisheria ya kumuita mgombea katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa, Mkurugenzi wa Uchaguzi anapozungumza mamlaka ya kisheria inapaswa amalize kwa kutaja kifungu kamili na jina la sheria husika inayompa yeye au TUME mamlaka hayo.

Kamati ya Maadili ya Kitaifa, TUME ina uwezo wa kwasilisha malalamiko tu mbele ya kamati na sio kumuita mgombea, hii ni kwa mujibu wa aya ya 5.4 ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na madiwani ya mwaka 2020.



Kwa mujibu wa aya 5.2.2 ya Maadili ya Uchaguzi 2020, Kamati ya Kitaifa inaundwa na watu wengi ikiwa na mjumbe wa kutoka TUME ya uchaguzi ambaye ndiye mwenyekiti wa Kamati, sasa bwana Mahera amejitokeza katika vyombo vya habari kama Mkurugenzi wa Uchaguzi na sio mwenyekiti wa kamati ya Maadili ya Kitaifa (kama ni mjumbe huko), ambayo inafanya jambo zima kuwa batili. TUME ina idara ya Sheria, ni aibu kufanya madudu ilhali watu wanalipwa mshahara na wanashindwa kushauri ipasavyo, huku ni kuchezea kodi zetu

 
Mimi kimsingi sikubalian na matamshi ya mkurugenz wa NEC kwasababu tayari ameonyesha dalili ya upendeleo fulani kwenye uchaguzi huu,kwani yeye amekuwa mgombea tayari? Na ni wa chama gan? Amejuaje kuwa kuna mgombea atapeleka madin nje ya nchi? Ni vizuri wazee wa chi hii wakaa pamoja na huyu mtu wakamkemea kwa matamshi yake haya wala haya afya kwa mustakabali wa uchaguzi huu.tayari ana personal interest kwa chama chake.naomba tusifike huko tafadhalini kabisa tuwe huru na haki kwa vyama vyote.
 
halafu kuna mtu anaamini hii ni tume huru ?
Tume huru inafanya kampeni za ccm hadharani?
Ndio maana tunasema kila siku hakuna tume huru ya uchaguzi Tz, hii tuliyo nayo ni Nec-ccm kama zilivyo; uvccm au uwt
 
Kazungumza kama nani, mpiga ramli, mfanya research (watanzania wanataka nini?), mwanachama wa chama fulani, mpiga kampeni, mpiga debe au msimamizi wa uchaguzi ?, Na amefanya uchunguzi kwamba kuna watu watauza madini nje ?, na kwa sasa hayo madini hatuyauzi tunayala au tunayatumia wenyewe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…