Mkurugenzi waTume ya uchaguzi hawezi kutusemea watanzania, eti Watanzania hawamtaki mtu atakayeuza madini yetu nje...... alikutana wapi na hao Watanzania?
Mkurugenzi mwenyewe ndio huyu?Lissu ajikite kwenye sera sio vibweka
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!
Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao
Ameyasema hayo alipokuwa anazungumza kumuandikia barua Tundu Lissu ili kutoa maelezo dhidi ya tuhuma za uongo anazotuhumiwa kuzitoa
Amesema Tundu Lissu amekuwa akitangaza matusi, tuhuma na kudanganya wafanyakazi badala ya kutangaza sera
==
YALIYOZUNGUMZWA KWENYE VIDEO YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC
Kwa mamlaka ya kisheria Tume iliyonayo, tayari imemuandikia Barua Mh. Tundu Lissu ya kumuita katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa ili aje kutoa maelezo na ushahidi wa kile alichokisema katika mkutano wake huko Musoma.
Kwa mara nyengine tena Tume inawasihi Wagombea wa Vyama vyote kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani ya nchi yetu, katika kipindi cha kampeni kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni, ratiba za kampeni na kuepuka matusi, sababu unatumia muda mwingi kutangaza matusi badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kutangaza tuhuma badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kuwadanganya Watanzania na wafanyakazi badala ya kutangaza sera.
Watanzania sasa hivi wanataka Afya iliyoimarika, Watanzania sasa hivi wanataka barabara nzuri, Watanzania sasa hivi wanataka miradi ya umeme, Watanzania sasa hivi wanataka elimu bora, Watanzania hawataki bra bra. Watanzania sasa hivi wanataka viongozi ambao watalinda madini yao, sio viongozi watakaokuja kuchukua madini yao na kupeleka kwa wageni nje.
Huyu mkurugenzi mkuu wa NEC anaitisha vyombo vya habari na kusema eti watanzania wanataka mtu atakayelinda madini yao, atakayewajengea vituo vya afya, atakayewajengea mabarabara, atakayewaletea umeme. Kwani haya yanaihusu NEC?
Mkurugenzi wa NEC anaposema kuwa watanzania hawataki mtu atakayetorosha madini nje, kwani inaihusu nini NEC?
Kweli nimeamini hawa NEC siyo wa kuwachekea hata kidogo. Hata hii engua ya wagombea wa upinzani inafanywa kimkakati na inaonekana wazi wazi.
Magufuli amevuruga mifumo mingi huru ya maamuzi. Hii nchi inakoelekea siko hata kidogo.
View attachment 1583150
Mungu wangu sio kwa kujisahau huku ...hii evidence mambo yakienda vibaya itamuweka pabaya mno...
Bila kutaraji kajionesha rangi zake halisi
kama kweli unmasikio basi yatakuwa hayafanyi kazi yaani lissu anavyotukana wewe husikii?Kwani huyo mkurugenzi anagombea urais kupitia chama gani? Watanzania tuna masikio, hayo matusi ya Lissu anasikia peke yake tu?
Wameshapoteana.Hayo anayoyaongea ndiyo kazi ya Tume? Mbona anaiweka Tume kwenye nafasi ya hatari sana? Yaani Tume inawalazimisha wagombea kitu cha kuongea? Watanzania wanajua wanachotaka kusikia na kila Chama kina ya kwake ya kujinadi kwa wananchi na Wananchi ndiyo wataamua.
Kwani madini yetu huwa yanauzwa wapi? Tume inahusika vipi na utekelezwaji wa Ilani za vyama? Mbona haijaongea kitu kuhusu aliyejisifu kuwanyima wananchi maendeleo kwa kutomchagua na kuahidi kuendelea kuwanyima kama hawatomchagua?
Mpaka hapo Tume imeshapoteza uhalali wake wa kusimamia uchaguzi huu na naiona kwamba kuwa ndiyo chanzo cha vurugu nchini.
Tunaposema Lissu ni hatari ndio muelewe. Mkurugenzi wa uchaguzi kachanganyikiwa na kuanza kunadi sera kama kichaa. Sasa kama kibaraka hofu yake ni dhahiri namna hii ‘bosi’ wake ana hali gani?
Hii sio aibu, ni fedheha!
amna mtu anayetishwa na icc yenu hiyoAngejua huu ni ushahidi tosha ICC
Hii ni dalili ya wazi kuwa ndani ya kambi ya CCM na watawala wameshapanic sana, Magu keshalegea kulegea sana, Bashiru anawatisha tu wanaCCM, PolePole anavurumisha matusi, Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ameingia kupiga kampeni!!
Lissu kamatia hapo hapo, endelea kupiga spana tu.
Unajua kuwa hujielewi au hujui pia?Yani mnatetea mtu anaetaka kuweka rehani ardhi yetu? Unajidai upo deep kumbe umejaza manyoya tu kichwani. Mkiona hamuwezi kuisapoti CCM bora mkae kimya kuliko kutetea uovu.
Ataiweza hiyo kazi ?Naona kapania kupambana na Lissu.
Mkurugenz anatuletea mambo ya kisengeHahaha mkurugenzi kasikia wapi watanzania wakitaka hayo?!
4..tundu lissuICC list
1. Bashiru
2. Polepole
3. Mahera
4. ...
Mkurugenzi kanichekesha na kunihuzunisha sana, Watanzania wapi waliyomwambia hayo?Hahaha mkurugenzi kasikia wapi watanzania wakitaka hayo?!
aliyeanza usenge ni tundu lissuMkurugenz anatuletea mambo ya kisenge
Huyo kada anajua madini tunayachimba na kuyala hapa hapaHivi madini yetu yanauzwa wapi? Si yanauzwa huko nje, huyu mkurugenzi ajiangalie sana.
"Eti" ndiye refa huyoHuyu mgombea wa chama gani jaman?mbona amechelewa kuanza kampeni