Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Ulinzi, Usalama wa Vyombo vya Majini na Utunzaji wa Mazingira ya Bahari (DMSE) Mhandisi Japhet L.Loisimaye kilichotokea Jana Jumapili, tarehe 10 Mei, 2020 jioni jijini Dar es salaam.
Shirika linatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa marafiki na watu wote walioguswa na msiba huu. Taarifa ya mazishi itatolewa kwa wafanyakazi wa Shirika mara baada ya kujulishwa na familia.
Bwana ametoa,Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
Imetolewa na Mkurugenzi Mkuu,
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania.