Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa unaofanyika kwa siku mbili kuanzia leo Jumamosi, Julai 11, 2020 jijini Dodoma, Wajumbe 1,846 wanatarajiwa kushiriki. Mkutano huo unongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli.
AJENDA:
1. Kufungua Mkutano
2. Marekebisho ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977, Toleo la 2017
3. Taarifa za Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020 za SMZ, SMT na CCM
4. Uteuzi wa Mgombea wa CCM wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
5. Kufunga Mkutano.
View attachment 1503538
UPDATES;
Mkutano Mkuu wa CCM unafanyika leo tarehe 11 Julai 2020 ukiwa na lengo kuu la kumpitisha mgombea wa Urais wa JMT.
Mkutano umehudhuriwa na wanachama 1,822 huku wanachama waliokosekana wakiwa 23 sawa na 1% hivyo uko sahihi kikatiba na ajenda zinaweza kujadiliwa.
View attachment 1503539