Mkutano wa SADC na EAC waazimia kuondoa vikosi vya kigeni visivyoalikwa katika ardhi ya DRC

Mkutano wa SADC na EAC waazimia kuondoa vikosi vya kigeni visivyoalikwa katika ardhi ya DRC

Wakuu,

Haya ndio maazimio ya mkutano wa SADC na EAC kuhusu mgogoro wa DRC, na moja ya walichoazimia ni Mkutano wa SADC na EAC waazimia kuondoa vikosi vya kigeni visivyoalikwa katika ardhi ya DRC.

Pia soma: Dar: Rais Samia akishiriki Mkutano wa Pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa EAC na SADC Februari 8, 2025

View attachment 3229429View attachment 3229430View attachment 3229431View attachment 3229432View attachment 3229433
View attachment 3229434
Kiswahili kilipaswa kuwepo hapo
 
Yameyarahisisha mno, ni kama wametekeleza wajibu tu wa kuhudhuria,hamna kipya hapo ngoma itaendelea
 
Wakuu,

Haya ndio maazimio ya mkutano wa SADC na EAC kuhusu mgogoro wa DRC, na moja ya walichoazimia ni Mkutano wa SADC na EAC waazimia kuondoa vikosi vya kigeni visivyoalikwa katika ardhi ya DRC.

Pia soma: Dar: Rais Samia akishiriki Mkutano wa Pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa EAC na SADC Februari 8, 2025

View attachment 3229429View attachment 3229430View attachment 3229431View attachment 3229432View attachment 3229433
View attachment 3229434
Maazimio mazuri. Je sasa Kagame akiendeleza hila zake hataki kutoka DRC itakuaje? Kiburi chake kitamponza maana itabidi vita apigwe.
 
Nimeyasoma maazimio....

FDRL nao ni tatizo....mkutano umeamua hao jamaa wawe "neutralized"....

Je serikali ya DRC itaweza?!!

Isipoweza je Rwanda itakubali kuondoa "vikosi vyake" ambavyo navyo VIMEAMRIWA visiendelee kuwepo DRC?!!

Ndani ya siku 5 zijazo imeamriwa CHIEF OF STAFFS wa majeshi ya nchi za SADC-EAC kukutana "kimipango"....

Ndani ya siku 30 zijazo mawaziri wa SADC-EAC wakutane wakiwa na ripoti ya kilichofanyika kutoka sasa.....

My take:
Mpira amerudishiwa Tshisekedi na serikali yake....mzigo alionao si wa kitoto.....

Ushauri:
Serikali ya DRC itulie sana katika kuyaendea maazimio haya kwani kusimama kwao imara ndiko kutakapotoa nafasi ya KUWALAUMU wengine na majeshi yao "yasioalikwa huko DRC".
Ni lazima wapitie katika njia za KISIASA na KIDIPLOMASIA kuondoa "nakama" iliyoko.

#Ndimi Chawa Promax wa Chifu Hangaya!
#Hasta la Victoria URT,amen!
 
nimetafakari sana, naamini imefika mahali tuwaulize wananchi wenyewe wa Goma na Bukavu, wanataka nini, wanataka kinshasa au wanataka wajitegemee? tukipata idadi kubwa ya raia wa eastern congo wanataka kujitawala, basi tisekeli anatakiwa kufyata mkia. kuachia ardhi inauma ila itabidi avumilie maumivu kama alivyovumilia msudani.
 
Vipi kama hivyo vikosi vya kigeni vimealikwa na AFC/M23?
 
Wakuu,

Haya ndio maazimio ya mkutano wa SADC na EAC kuhusu mgogoro wa DRC, na moja ya walichoazimia ni Mkutano wa SADC na EAC waazimia kuondoa vikosi vya kigeni visivyoalikwa katika ardhi ya DRC.

Pia soma: Dar: Rais Samia akishiriki Mkutano wa Pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa EAC na SADC Februari 8, 2025

View attachment 3229429View attachment 3229430View attachment 3229431View attachment 3229432View attachment 3229433
View attachment 3229434
Utekelezaji wa hayo maazimio ndio kipengele.
 
Kiswahili kilipitishwa na AU kama lugha ya mawasiliano, lakini mwisho nimeona DONE kwa lugha zingine pasipo kiswahili tatizo nini?

Pili sijapenda walivyoa mua, wamefunika kombe mwanaharamu apite. Mbona sikuona Muwakilishi wa M23 au ndio Kagame na Museveni?

Mipaka ya Kongo iheshimike, Kivu na Goma ni sehemu ya DRC siyo uwanja wa vita, M23 wakubali kuishi DRC kwa masharti ya DRC siyo masharti yao.

Kuwaacha M23 bila kuwaonya nikama wameogopwa, au taarifa ilipunguza maongezi yaliyokuwepo?

Anyway tusubiri mengine labda hii ilikuwa supu ya kupasha matumbo, tusubili nyama.
 
nimetafakari sana, naamini imefika mahali tuwaulize wananchi wenyewe wa Goma na Bukavu, wanataka nini, wanataka kinshasa au wanataka wajitegemee? tukipata idadi kubwa ya raia wa eastern congo wanataka kujitawala, basi tisekeli anatakiwa kufyata mkia. kuachia ardhi inauma ila itabidi avumilie maumivu kama alivyovumilia msudani.
Tshisekedi kazi anayo.....

Kubwa kabisa ni "kuwaneutalize" FDRL halafu atafute njia za kisiasa na kidiplomasia kudeal na M 23....hakuna namna mpwa!
 
Kiswahili kilipitishwa na AU kama lugha ya mawasiliano, lakini mwisho nimeona DONE kwa lugha zingine pasipo kiswahili tatizo nini?

Pili sijapenda walivyoa mua, wamefunika kombe mwanaharamu apite. Mbona sikuona Muwakilishi wa M23 au ndio Kagame na Museveni?

Mipaka ya Kongo iheshimike, Kivu na Goma ni sehemu ya DRC siyo uwanja wa vita, M23 wakubali kuishi DRC kwa masharti ya DRC siyo masharti yao.

Kuwaacha M23 bila kuwaonya nikama wameogopwa, au taarifa ilipunguza maongezi yaliyokuwepo?

Anyway tusubiri mengine labda hii ilikuwa supu ya kupasha matumbo, tusubili nyama.
Vikao vya wakuu wa SADC-EAC vinahitaje uwakilishi wa WAKONGOMANI M 23?!!!

M 23 wakakae mezani na ndugu yao Tshisekedi......
 
Vikao vya wakuu wa SADC-EAC vinahitaje uwakilishi wa WAKONGOMANI M 23?!!!

M 23 wakakae mezani na ndugu yao Tshisekedi......
Kwani mgogoro unahusu nini au nani na nani?

Mi ninadhani M23 ni wadau wakubwa kwenye huo mkutano, sasa bila kuwasikiliza wao unafikiaje maamuzi ya kusitisha vita, ikiwa wao ndio wanapigana na DRC?
 
Kwani mgogoro unahusu nini au nani na nani?

Mi ninadhani M23 ni wadau wakubwa kwenye huo mkutano, sasa bila kuwasikiliza wao unafikiaje maamuzi ya kusitisha vita, ikiwa wao ndio wanapigana na DRC?
Sawa.....

Uhusiano mbovu wa hao M 23 na serikali ya DRC haujaanza hivi karibuni.....

Kabla ya SADC-EAC kuwaingiza mkutanoni mwao ,je serikali ya DRC ilianza lini kukaa katika meza ya kweli ya usuluhishi* na hao watu ?!!
 
Back
Top Bottom