Pre GE2025 Mkutano wa Tundu Lissu na Waandishi wa Habari Singida Novemba 12, 2024

Pre GE2025 Mkutano wa Tundu Lissu na Waandishi wa Habari Singida Novemba 12, 2024

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000


Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu anatarajiwa kuongea na waandishi wa habari muda wote kuanzia sasa.

Fuatilia updates kadiri zitakavyojitokeza.

  • Wakati anazungumza na waandishi wa habari Tundu Lissu amedokeza kuwa kutokana na yale yanayoendelea kwenye Uchaguzi ni vyema CHADEMA wakarudi nyuma na kujipanga upya

Mimi napenda kuamini tunaimba wimbo mmoja, kama hatuimbi wimbo mmoja basi tutakuwa na hali mbaya sana. Kama hatuwezi kukubaliana kwamba Samia anahitaji kukabiliwa kwa pamoja na kauli moja na sisi wote, kama kuna wanaofikiria wataenda mafichoni kukutana na Samia na kuteta, tutakuwa na hali mbaya sana, mimi naogopa.

  • Aidha Tundu Lissu alisema katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu 2024 kikubwaa CHADEMA watapigania wagombea waliobaki tu lakini huu kifupi umekwisha kwani udanganyifu umekuwa mkubwa.

  • Aidha alisema kuwa CHADEMA kwa sasa kijikite zaidi katika kugombea Katiba mpya, Tume uhuru, Demokrasia, na Haki.

  • Pia alidokeza kuwa wagombea wengi wa CHADEMA waliwekewa mapingamizi hata kabla ya majina yao kubandikwa
Singida tulisimamisha wagombea takriban 1225, wamepigwa mpaka tuliobaki nao nafikiri hawafiki 500 zaidi ya nusu wameondolewa pamoja na kwamba kanuni zinasema mapingamizi yataamuliwa ndani ya siku mbili tokea mapingamizi hayo yapokelewe.
Mapingamizi yalitakiwa yapokelewe tarehe 9 na tarehe 10 Novemba. Mapingamizi mengi yameletwa tarehe 8, kwa mujibu wa kanuni, tarehe 8 ilikuwa siku ya kuteua wagombea tu.



1731396908394.png
 
Taifa Linaongea na Dunia nzima (EU World Bank IMF Trump Mabalozi) wanasikiliza

Huko nje Tunaitwa majina ya ajabu ajabu kwa sababu ya Mambo ya kikkuda kama haya Mijitu mizima ustaraabu SIFURI

Unaharibu Uchaguzi kwa sababu za uchawa utazani hizo fedha za kuendeshea uchaguzi mnazitoa kwenye Familia zenu
 
Inamaana CHADEMA tu ndiyo wenye makosa na kuenguliwa. Mbona CCM hawaenguliwi?
 

Attachments

  • b3a34e7e631270a9e73fdd13db687369.mp4
    3.6 MB
  • watermark-51a3cc01acd06eefe8d1d23a20c76918_0.jpeg
    watermark-51a3cc01acd06eefe8d1d23a20c76918_0.jpeg
    516.2 KB · Views: 3
Awaambie dunia kuwa Mozambique na Tanzania kuna uhuni na uhaini wapigwe vikwazo hawa viongozi wanaoharibu uchaguzi?!! Magnistky law iwahusu
 
halafu kwa nn anavaa vaa madude dude hivyo. sio sawa madude dude mikononi hayo mambo ya vijana
 
Shida ya Lissu ni inconsistency leo ataongea mambo ya maana, kesho anaanza utunzi wake..

Mkutano wa leo kajenga hoja za msingi na kujibu hoja kama kiongozi wa taifa na kutoa elimu ya juu ya siasa na sheria. Utaashangaa kama CDM hawatafuata mtazamo wake kama msimamo wa chama.
 
Wale vilaza pale chadema wakiongozwa na Mzee Mbowe,Lema na Mdude unadhani wanao uwezo wa kuelewa alichoongea MSOMI Lissu?
Shida ya Lissu ni inconsistency leo ataongea mambo ya maana, kesho anaanza utunzi wake..

Mkutano wa leo kajenga hoja za msingi na kujibu hoja kama kiongozi wa taifa na kutoa elimu ya juu ya siasa na sheria. Utaashangaa kama CDM hawatafuata mtazamo wake kama msimamo wa chama.
,
 
Wale vilaza pale chadema wakiongozwa na Mzee Mbowe,Lema na Mdude unadhani wanao uwezo wa kuelewa alichoongea MSOMI Lissu?

,
Siasa za Tanzania ni shida. Chukulia yote aliyoongea kwa muktadha wa kutoa elimu kwanini habari za ‘nusu mkate’ ni changa la macho kwa siasa za Tanzania,

Mapungufu ya sheria iliyounda tume huru ya uchaguzi Tanzania, na kutokuwepo na nia ya dhati at implementation level TAMISEMI bado inasimamia.

Ameongea mengi ambayo yana make sense kwanini chama kinahitaji ‘strategic retreat’ hadi kuhitimisha huu uchaguzi jamaa washafanya yao maana hata rufaa hawataki (kwa kuweka mazingira magumu ya wakata rufaa).

Sasa kwa siasa za Tanzania watu wataweka vi-clip vyao vya dakika mbili na kujengea hoja; wakati mwenzao kaongea mengi sana na yenye kuelimisha kupata inside story.
 
Back
Top Bottom