Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Marekani Afrika afungua mazoezi ya kijeshi baina ya US na Tanzania

Nadhani wewe ni mdogo kiumri na haujui mazingira yaliyopelekea mazingira magumu ya kiuchumi, skiliza: Kilichoharibu uchumi wa Tanzania ni vita vya kagera. Vita vya kagera vilitokea mwaka 1978 na vikaisha kabisa mwaka 1980! Kabla ya vita hivyo uchumi wa nchi yetu ulikuwa mzuri sana, tulikuwa na viwanda vingi sana. Dola moja ya marekani ilikuwa sawa na sh 8 za Tanzania. Tulikuwa na shilingi yenye nguvu sana. Vitu vingi vilikuwa vinanunuliwa kwa senti yaani pungufu ya shilingi moja. Vile vita vilitugharimu sana. Baada ya vita ikatangazwa miezi 18 ya kufunga mikanda. Lakini pia mwanzoni mwa miaka ya 80 kulitkkea ukame mkubwa sana na kukawa na njaa kali. Hiyo pia ikasababisha mambo kuwa magumu. Kipindi hicho ndio kilikuwa kigumu kwa kukosa bidhaa muhimu na Taifa liliishiwa kabisa pesa za kigeni.
Vinginevyo Tanzania ilikuwa inaheshimika sana duniani na haikuweza kuyumbishwa hata kidogo. Awamu iliyopita ilijitahidi sana kurejesha heshima hiyo.
 
Mwanzoni nilijua Tanzania ni nchi huru kumbe inaongozwa na vibaraka wa mabeberu! Mweeeh!! [emoji52][emoji52][emoji58][emoji58]
 
watu walikuja na Injili ya Yesu ukidhani kweli kumbe walikuwa na jambo lao.
Wewe Pythagoras kadeal na issues za hesabu kule, huenda hapa si mahali pako nadhani!!! Usidhani hata chembe moja kwamba kila ngozi nyeupe unayoiona ni exploiter. That's being too naïve and generalistic and simplistic.

Ni sawa na wale wanasema Wachagga wako hivi ama vile. Najua kuna hujuma kwenye Injili ya Yesu Kristo watu wanafanya hadi sasa tangu enzi hizo za Bible, lakini haina maana kwamba lengo la Ukristo lilikuwa kukutawala wewe.

BTW pasipo Biblia na Ukristo, huenda (nani ajuaye!???), pengine Osama na Obama wangeshaifikisha dunia mwisho wake kitambo tu kabla ya Gharika ya Nuhu!

Mlaumu sana mwalimu wako wa historia kwa kuwa na uelewa finyu na duni ama kuwa biased dhidi ya ukweli wa ujumbe wa mbinguni.
 
Sitaki kuamini kwamba vita hivyo vya miaka miwili ndiyo chanzo cha umaskini wetu hadi sasa kama taifa. Unajua mbaazi ikikoswa maua husingizia jua.

Tatizo la nchi yetu (na pia tatizo linalosibu Bara Afrika) ni kukosa utekelezaji wa mipango kwa sababu haina watu wengi wenye nia (siyo uwezo wala), ya kuitekeleza.

Tanzania ina watu ambao kwa sehemu kubwa wanawaza tu kujitajirisha haraka wao wenyewe kwa gharama ya kuwahatarisha na kuwaangamiza wananchi wengine wote. Hii ni zaidi ya vina vya uwendawazimu!!!
 
..tutajuaje kinachoendelea wakishaingia ndani ya mahema?

..ila mkae mkijua jeshi la marekani linaruhusu ushoga.
Hata kama wanaruhusu, sisi tutashirikiana nao na kuchukuwa yake mazuri pekee. Ushoga tunawaachi wao wenyewe.
 
Lisu alikuwa na kesi gani? Kumbe wewe pimbi sana.
 
Wanakuja kujua udhaifu wa jwtz watachunguza kila kitu na kupandikiza wapelelezi wao humo baadae wakija kuanza chokochoko wanajua pa kupenyea
Una akili za kushikiwa no wonder umeweka hilo picha la dictator mwenzenu kwenye avatar.
 
Ni moja ya aina ya watu wapumbavu sana nchi hii, umeambiwa 2017 walikuwepo. Tangu enzi za nyerere tunapeleka wanajeshi na maafisa usalama kujifunza nje
Dah, kiongozi jamaa naamini sasa kuwa wakishakuwa na chuki na kiongozi aliyopo huwa akili zao zinaenda likizo sijui; maana hata bayana inageuzwa na kuwa ficho. Mi tangu nipo mdogo, nimekuwa nikiuona ushirikiano huu wa kijeshi na mafunzo km haya. Miaka yote, lazima uone au kusikia msaada/mafunzo/ziara kutoka us, German (hawa zaidi ktk wizara ya mambo ya ndani), uingereza na hata China. Sasa sijui kilicho tofauti leo hii ni nini wanafiki hawa?!!!!!! Wanaboa sometimes!!
 
Nyerere hakutaka jwtz iwe na umoja na USA alijua marekani wana Tabia za kuchunguza udhaifu kisha kuleta shida baadae akawakataa kwenye idara za kijeshi lakini alishirikiana nao katika nyanja zingine kabsa
Ni kweli Nyerere aligoma kushirikiana na US kijeshi. Hawa kadri unavyowasogeza jikoni ndivyo unavyozidi kuwa uchi kwao. Ni mabingwa wa kuanzisha uasi.
 
Nyerere hakutaka jwtz iwe na umoja na USA alijua marekani wana Tabia za kuchunguza udhaifu kisha kuleta shida baadae akawakataa kwenye idara za kijeshi lakini alishirikiana nao katika nyanja zingine kabsa

Lkn alikua akipigwa na njaa anaenda kuwaomba wamarekani msaada wa mahindi ya njano.
 
Vipi CDF akafungue mafunzo huko marekani ,syo wao tu kuja huku kwetu ,hapo ndo kutakuwa ushirikiano
Akili za kulishwa, kula na wewe kwa mkono wako, mwisho utalishwa hata visivyo liwa.
 
Ndio naweza kuwa mdogo kiumri lakini historia haidanganyi vita vya kagera tulikurupuka tungeweza kuiepuka kidiplomasia kwa kutumia vyombo vya kimataifa lakini mwalimu alitaka kumrudisha rafiki yake obote madarakani.
Pili ndiyo shilingi yetu ilikuwa na thamani baada ya vita uchumi ukayumba Imf na WB wakaleta mapendekezo tufanye devaluatiation supported by mzee mtei na great economics za BOT again arrogance ya mwalimu akakataa uchumi ukavunjika vipande vipande mashirika ya umma yakapewa wanajeshi wasio na ujuzi wowote.
Unazungumzia ukame hujui kuna nchi hazilimi kabisa lakini ni biggestdonors!!??

Thats history mwalimu alikosea kutowasikiliza wachumi, kibaya zaidi alitumia rasilimali za nchi vibaya kwasaidia ambao wanatucheka na kutukejeli hivi sasa alisahau kuwa ni rais wa tanzania akajivika ubaba wa Africa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…