TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 25,225
- 25,488
BEBERUUUUUUUUS Unafiki ni kitu kibaya sana.
Kisa katiba mpya au.? 😂😀😂😂Subiri uchumi usimamishwe, mpaka utaita maji mma
Nadhani wewe ni mdogo kiumri na haujui mazingira yaliyopelekea mazingira magumu ya kiuchumi, skiliza: Kilichoharibu uchumi wa Tanzania ni vita vya kagera. Vita vya kagera vilitokea mwaka 1978 na vikaisha kabisa mwaka 1980! Kabla ya vita hivyo uchumi wa nchi yetu ulikuwa mzuri sana, tulikuwa na viwanda vingi sana. Dola moja ya marekani ilikuwa sawa na sh 8 za Tanzania. Tulikuwa na shilingi yenye nguvu sana. Vitu vingi vilikuwa vinanunuliwa kwa senti yaani pungufu ya shilingi moja. Vile vita vilitugharimu sana. Baada ya vita ikatangazwa miezi 18 ya kufunga mikanda. Lakini pia mwanzoni mwa miaka ya 80 kulitkkea ukame mkubwa sana na kukawa na njaa kali. Hiyo pia ikasababisha mambo kuwa magumu. Kipindi hicho ndio kilikuwa kigumu kwa kukosa bidhaa muhimu na Taifa liliishiwa kabisa pesa za kigeni.Huo msimamo ndo ulisababisha
Bidhaa kupungua nchini
Sukari kuadimika
Watu kupanga foleni kununua sukari, sabuni na dawa ya meno
Mafuta kuadimika
Na uchumi kudidimia kabisa
Mpaka nchi ilipomshinda nyerere akaona ajiuzulu.
Kama ndo hiyo misimamo unaizungumzia tuambie ilitufikisha wapi !?
Wewe Pythagoras kadeal na issues za hesabu kule, huenda hapa si mahali pako nadhani!!! Usidhani hata chembe moja kwamba kila ngozi nyeupe unayoiona ni exploiter. That's being too naïve and generalistic and simplistic.watu walikuja na Injili ya Yesu ukidhani kweli kumbe walikuwa na jambo lao.
Sitaki kuamini kwamba vita hivyo vya miaka miwili ndiyo chanzo cha umaskini wetu hadi sasa kama taifa. Unajua mbaazi ikikoswa maua husingizia jua.Nadhani wewe ni mdogo kiumri na haujui mazingira yaliyopelekea mazingira magumu ya kiuchumi, skiliza: Kilichoharibu uchumi wa Tanzania ni vita vya kagera. Vita vya kagera vilitokea mwaka 1978 na vikaisha kabisa mwaka 1980! Kabla ya vita hivyo uchumi wa nchi yetu ulikuwa mzuri sana, tulikuwa na viwanda vingi sana. Dola moja ya marekani ilikuwa sawa na sh 8 za Tanzania. Tulikuwa na shilingi yenye nguvu sana. Vitu vingi vilikuwa vinanunuliwa kwa senti yaani pungufu ya shilingi moja. Vile vita vilitugharimu sana. Baada ya vita ikatangazwa miezi 18 ya kufunga mikanda. Lakini pia mwanzoni mwa miaka ya 80 kulitkkea ukame mkubwa sana na kukawa na njaa kali. Hiyo pia ikasababisha mambo kuwa magumu. Kipindi hicho ndio kilikuwa kigumu kwa kukosa bidhaa muhimu na Taifa liliishiwa kabisa pesa za kigeni.
Vinginevyo Tanzania ilikuwa inaheshimika sana duniani na haikuweza kuyumbishwa hata kidogo. Awamu iliyopita ilijitahidi sana kurejesha heshima hiyo.
Kwani umeambiwa wanaenda kufundisha ushoga?..jeshi la marekani linaruhusu ushoga halafu sisi tuko kimbelembele kushirikiana nao kimafunzo.
Hata kama wanaruhusu, sisi tutashirikiana nao na kuchukuwa yake mazuri pekee. Ushoga tunawaachi wao wenyewe...tutajuaje kinachoendelea wakishaingia ndani ya mahema?
..ila mkae mkijua jeshi la marekani linaruhusu ushoga.
Lisu alikuwa na kesi gani? Kumbe wewe pimbi sana...wewe labda umri wako ni mdogo.
..kwa taarifa yako Tanzania iliwahi kutimua maofisa wa ubalozi wa Marekani hapa nchini.
..Tanzania pia ilishawahi kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na kuufunga ubalozi wa Ujerumani Magharibi.
..Sasa hivi tumekuwa watu wa kupiga domo tu na kudanganya-danganya wananchi kwa propaganda lakini hatuna msimamo wowote.
..Mwaka jana Tundu Lissu alisindikizwa na balozi wa Ujerumani mpaka uwanja wa ndege alipotokomea.
..Lissu ana kesi na alikuwa akihitajika mahakamani, lakini serikali na polisi wakaacha aondoshwe nchini na balozi wa Ujerumani.
..Jambo hilo lisingeweza kutokea wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere kwani wakati ule serikali na viongozi wetu walikuwa na misimamo na kamwe hawakuruhusu mabeberu watupande kichwani.
Una akili za kushikiwa no wonder umeweka hilo picha la dictator mwenzenu kwenye avatar.Wanakuja kujua udhaifu wa jwtz watachunguza kila kitu na kupandikiza wapelelezi wao humo baadae wakija kuanza chokochoko wanajua pa kupenyea
Dah, kiongozi jamaa naamini sasa kuwa wakishakuwa na chuki na kiongozi aliyopo huwa akili zao zinaenda likizo sijui; maana hata bayana inageuzwa na kuwa ficho. Mi tangu nipo mdogo, nimekuwa nikiuona ushirikiano huu wa kijeshi na mafunzo km haya. Miaka yote, lazima uone au kusikia msaada/mafunzo/ziara kutoka us, German (hawa zaidi ktk wizara ya mambo ya ndani), uingereza na hata China. Sasa sijui kilicho tofauti leo hii ni nini wanafiki hawa?!!!!!! Wanaboa sometimes!!Ni moja ya aina ya watu wapumbavu sana nchi hii, umeambiwa 2017 walikuwepo. Tangu enzi za nyerere tunapeleka wanajeshi na maafisa usalama kujifunza nje
Ni kweli Nyerere aligoma kushirikiana na US kijeshi. Hawa kadri unavyowasogeza jikoni ndivyo unavyozidi kuwa uchi kwao. Ni mabingwa wa kuanzisha uasi.Nyerere hakutaka jwtz iwe na umoja na USA alijua marekani wana Tabia za kuchunguza udhaifu kisha kuleta shida baadae akawakataa kwenye idara za kijeshi lakini alishirikiana nao katika nyanja zingine kabsa
Nyerere hakutaka jwtz iwe na umoja na USA alijua marekani wana Tabia za kuchunguza udhaifu kisha kuleta shida baadae akawakataa kwenye idara za kijeshi lakini alishirikiana nao katika nyanja zingine kabsa
Akili za kulishwa, kula na wewe kwa mkono wako, mwisho utalishwa hata visivyo liwa.
Ndio naweza kuwa mdogo kiumri lakini historia haidanganyi vita vya kagera tulikurupuka tungeweza kuiepuka kidiplomasia kwa kutumia vyombo vya kimataifa lakini mwalimu alitaka kumrudisha rafiki yake obote madarakani.Nadhani wewe ni mdogo kiumri na haujui mazingira yaliyopelekea mazingira magumu ya kiuchumi, skiliza: Kilichoharibu uchumi wa Tanzania ni vita vya kagera. Vita vya kagera vilitokea mwaka 1978 na vikaisha kabisa mwaka 1980! Kabla ya vita hivyo uchumi wa nchi yetu ulikuwa mzuri sana, tulikuwa na viwanda vingi sana. Dola moja ya marekani ilikuwa sawa na sh 8 za Tanzania. Tulikuwa na shilingi yenye nguvu sana. Vitu vingi vilikuwa vinanunuliwa kwa senti yaani pungufu ya shilingi moja. Vile vita vilitugharimu sana. Baada ya vita ikatangazwa miezi 18 ya kufunga mikanda. Lakini pia mwanzoni mwa miaka ya 80 kulitkkea ukame mkubwa sana na kukawa na njaa kali. Hiyo pia ikasababisha mambo kuwa magumu. Kipindi hicho ndio kilikuwa kigumu kwa kukosa bidhaa muhimu na Taifa liliishiwa kabisa pesa za kigeni.
Vinginevyo Tanzania ilikuwa inaheshimika sana duniani na haikuweza kuyumbishwa hata kidogo. Awamu iliyopita ilijitahidi sana kurejesha heshima hiyo.
nimecheka sana🤣🤣🤣Kwani wanatoa mafunzo ya ushoga?