Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

Una umri gani? ....................... Tatizo lako hukuwahi kupitia JKT, daah miaka sita hiki kitu kinakusumbua ?! una kazi ya kufanya?
sie vijana wa sasa man JKT tunaisikia tu kwa waliopitia bahati mbaya tumekuta mafunzo yalishafungwa ila tulipenda sana yangeendelea kuwepo!
 
Una umri gani? ....................... Tatizo lako hukuwahi kupitia JKT, daah miaka sita hiki kitu kinakusumbua ?! una kazi ya kufanya?

umri si tatizo na kuto kujua ni kwamba sisi vijana wa sasa hatujapitia JKT nadhani itakuwa poa ukiendelea kunijuza kwa ninyi wenzetu mliopitia JKT sisi wengine tumepiga shule kipindi cha kikwete na mkapa
 
hapo penye bold nimepapenda. kweye gwaride huwa wankusudia kutoa kiapo cha utii na hesjhima zao kwa amiri jeshi mkuu ambaye ndiye commanda in chief wa majeshi yote, hapo ndipo majeshi yote yanapohusika kila jeshi kivyake. ni katika kuonyesha uniformity ndio maana wanafanya mazoezi kwa pamoja laini wakati wa kumatch, kla jeshi linatengeneza gadi zake, hawachanganyiki kuonyesha kuwa ni majeshi tofauti. enzi za mwalimu aliwahi kuwa na ADC kutoka polisi . kwa hiyo kwa suala la nani awe AD linaweza kutoka katika majeshi mengine, ila nadhani wanaona kama ujiko fulani hivi kumchukua toka JWTZ

Kwenye gwaride mkuu wa nchi huwa anasindikizwa na CDF pekee bila IGP au magereza. Hii ina maana mkuu wa majeshi ana dhamana kubwa zaidi.
 
wakuu kumekuwa na muendelezo wa kuchaguliwa wakuu wa majeshi kutoka jkt kwa miaka mfurulizo.je ni kanuni za majeshi yetu au ni matakwa ya marais wetu.naomba kujuzwa
 
mhh haya ngoja tusubiri wenye data waje kutuelimisha kuhusu hili
 
wakuu kumekuwa na muendelezo wa kuchaguliwa wakuu wa majeshi kutoka jkt kwa miaka mfurulizo.je ni kanuni za majeshi yetu au ni matakwa ya marais wetu.naomba kujuzwa


Mkuu wa majeshi mwingine ni nani? Hata hivyo kama Mwamunyange alieteuliwa na Mkapa kuwa mkuu wa JKT akitokea JW na huko alikua director of millitary intelligence, pia kwa uelewa waangu JKT na JW ni walewale in fact JKT branch ya JW so sioni tatizo mkuu wa majeshi akitoka huko.

Wapo wajuzi watatueleza vizuri zaidi
 
Hakuna tofauti kubwa kati ya JW na JKT labda majukumu tu.Inapotokea vita wote wanavaa sare zinazofanana(mavazi ya mapambano), Gari zao namba ni hizo hizo(JW, MT),vyeo vinafanana n.k.
JKT ni moja kati ya kamandi zilizo chini ya JWTZ.Majukumu yake ni malezi kwa vijana,ulinzi wa taifa na uzalishaji mali. Kamandi nyingine ni Kamandi ya Nchi Kavu, Kamandi ya Anga na Kamandi ya Wanamaji.
Wasiwasi unaotokea kuwa kwa nini Wakuu wa Majeshi(hapa ni pamoja na Wanadhimu) wanatoka JKT si wa msingi sana kwani wote ni wanajeshi( Kuanzia mwaka 1975).Ni sawa na pale ambapo kule Marekani 'Chairman of Joint Chiefs' alipotoka katika jeshi la 'Marines'. Kila mtu alishangaa kuwa 'Chairman of Joint Chiefs' 'has never been a Marine'. Hii ni kwa sababu 'Marines' ni kitengo kidogo.
Wakuu wa majeshi huteuliwa kutokana na vigezo mbalimbali kama uzoefu,uadilifu,weledi n.k
Mkuu wa majeshi aliye na historia ya JKT ni Jenerali Davis Mwamunyange.Wanadhimu wakuu wenye historia na JKT ni Luteni Jenerali Samuel Ndomba na Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo.
 
kwani kwenye "majeshi ya ulinzi na usalama" ambao mkuu wao ni CDF, jeshi letu la polisi, magereza, zimamoto na mgambo hayahusiki au yenyewe sio majeshi na hayahusiki na ulinzi wala usalama?
 
Mkuu wa majeshi mwingine ni nani? Hata hivyo kama Mwamunyange alieteuliwa na Mkapa kuwa mkuu wa JKT akitokea JW na huko alikua director of millitary intelligence, pia kwa uelewa waangu JKT na JW ni walewale in fact JKT branch ya JW so sioni tatizo mkuu wa majeshi akitoka huko.

Wapo wajuzi watatueleza vizuri zaidi
Kweli mkuu.
Tanzania tunatatizo kubwa la uelewa kwa vijana wetu, wengine hawajui hata chanzo cha JKT na uhusiano wake na JWTZ.
 
Mkuu wa majeshi mwingine ni nani? Hata hivyo kama Mwamunyange alieteuliwa na Mkapa kuwa mkuu wa JKT akitokea JW na huko alikua director of millitary intelligence, pia kwa uelewa waangu JKT na JW ni walewale in fact JKT branch ya JW so sioni tatizo mkuu wa majeshi akitoka huko.

Wapo wajuzi watatueleza vizuri zaidi
Mkuu hapo kwenye red siamini kama ni kweli. Hata mfumo wa mafunzo kwa vyombo hivi ni tofauti. Hata hivyo, nashukuru kwa kunijulisha kuwa kabla ya ukuu wa JKT Mwamunyange allikuwa JW. Hii kitu nilikuwa siijui.
 
Mkuu hapo kwenye red siamini kama ni kweli. Hata mfumo wa mafunzo kwa vyombo hivi ni tofauti. Hata hivyo, nashukuru kwa kunijulisha kuwa kabla ya ukuu wa JKT Mwamunyange allikuwa JW. Hii kitu nilikuwa siijui.

Yupo sahihi,maelezo mazuri yametolewa hapo juu na mkuu mungo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hapo kwenye red siamini kama ni kweli. Hata mfumo wa mafunzo kwa vyombo hivi ni tofauti. Hata hivyo, nashukuru kwa kunijulisha kuwa kabla ya ukuu wa JKT Mwamunyange allikuwa JW. Hii kitu nilikuwa siijui.

Kwanini huamini sasa, JKT na JW ni kitu kile kile, mtu anaweza kuhamishiwa either side wakati wowote.
 
kuweka rekodi sawa, mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama lazima atoke JW kwa kuwa ndio senior na tunaposema majeshi tunazungumzia jeshi la anga, jeshi la maji, jeshi la nchi kavu, na jeshi la kujenga taifa. Wakati wa magwaride yote ya kitaifa hayo majeshi ndio hutangulia mbele ikiongozwa na jeshi la nchi kavu, polisi na wenzake hufunga tela. anapokuja raisi wa nchi nyingine gwaride linahusu JW peke yao na siku rais anaagwa gwaride linahusu JW peke yao, gwaride la muungano au la uhuru huongozwa na kamanda toka JW mind you kwamba hata hizo guard zina wakuu wao ambao wanachukua amri kutoka kwa mkuu wa parade ambaye anakuwa na cheo cha luteni kanali . Raisi huingia na mkuu wa majeshi uwanjani kwa kuwa naye ni raisi asiyeonekana akitaka kumwondoa rais madarakini hufanikiwa kwakuwa silaha zote kuu zipo chini yake kupitia anga, ardhi na maji. polisi hawezi kuwa ADC wa rais hata siku moja utaratibu lazima atoke JW na awe senior officer yaani anzie cheo cha major na asizidi cheo cha kanali.
 
Kweli mkuu.
Tanzania tunatatizo kubwa la uelewa kwa vijana wetu, wengine hawajui hata chanzo cha JKT na uhusiano wake na JWTZ.

Nina uhakika sana kuwa huwa una michango mizuri kama utaamua kuitoa.
Ila kinachofifisha ni style yako ya uchangiaji imekaa kushambulia zaidi na kuji defend zaidi hata pale ambapo hapana ulazima....hautoi fair ground.
Siku utakapolitambua hili naamini wengi watafaidika sana michango yako....I'm sory but I have to tell this.
 
kuweka rekodi sawa, mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama lazima atoke JW kwa kuwa ndio senior na tunaposema majeshi tunazungumzia jeshi la anga, jeshi la maji, jeshi la nchi kavu, na jeshi la kujenga taifa. Wakati wa magwaride yote ya kitaifa hayo majeshi ndio hutangulia mbele ikiongozwa na jeshi la nchi kavu, polisi na wenzake hufunga tela. anapokuja raisi wa nchi nyingine gwaride linahusu JW peke yao na siku rais anaagwa gwaride linahusu JW peke yao, gwaride la muungano au la uhuru huongozwa na kamanda toka JW mind you kwamba hata hizo guard zina wakuu wao ambao wanachukua amri kutoka kwa mkuu wa parade ambaye anakuwa na cheo cha luteni kanali . Raisi huingia na mkuu wa majeshi uwanjani kwa kuwa naye ni raisi asiyeonekana akitaka kumwondoa rais madarakini hufanikiwa kwakuwa silaha zote kuu zipo chini yake kupitia anga, ardhi na maji. polisi hawezi kuwa ADC wa rais hata siku moja utaratibu lazima atoke JW na awe senior officer yaani anzie cheo cha major na asizidi cheo cha kanali.

Umeongea kila kitu pwenti tupu ila hapo kwenye bbold tu umeteleza ndugu yangu. Rais Nyerere alikua na maADC kutoka Polisi zaidi ya mara mbili. Wa mwisho alikwenda Msumbiji nadhani kusaidia kutrain Jeshi lao jipya la Polisi. Ni zamani kidogo na kuna sababu ambazo zilifanya wakabadilisha huu utaratibu ila sio hizo ulizoandika. Kuna mada tuliongea haya mambo na mkuu JokaKuu nadhani atanisaidia hapa.
 
Last edited by a moderator:
Kwa kuongezea Mkuu wa Majeshi, IGP, Mkuu wa Magereza Hawa wote lazima wawe TISS ....

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Nina uhakika sana kuwa huwa una michango mizuri kama utaamua kuitoa.
Ila kinachofifisha ni style yako ya uchangiaji imekaa kushambulia zaidi na kuji defend zaidi hata pale ambapo hapana ulazima....hautoi fair ground.
Siku utakapolitambua hili naamini wengi watafaidika sana michango yako....I'm sory but I have to tell this.
Mkuu, nilikuwa sabatical, kama umegonga bull vile!
 
KMKM nalo ni jeshi?! Mbona wamechoka sana. Huku Zanzibar wanalinda hospitali tu
 
Back
Top Bottom