Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

ADC (aide de camp) imeibuka kwenye mjadala; huyu ni nani hasa? Google inaniambia ni msaidizi wa karibu zaidi na rais, je huyu ndie mlinzi wa rais kwa setting za Tanzania? Ahsanteni

tragedy of the commons
 
Tatizo vijana wa siku hizi hamkupitia JKT kujulishwa mambo haya. JKT ni sehemu ya Jeshi na kama wewe ni Luteni USU au major au Major Jenelali ujui wewe ni JWTZ hata lensi corporal ni mwanajeshi wa Tanzania sema tu ni uhamisho kwenda JKT lakini mafunzo yote ya Kijeshi ni ya JWTZ. Kwa hiyo CDF au mkuu wa Majeshi tuseme Mwamnyange ni mkuu wa Majeshi yote ya ulinzi na usalama CDF (Chief of Defence Forces na ndiyo maana wakati wa sherehe utaona ndiye pekee anaandamana na Amiri Jeshi Mkuu au Rais na wala si mkuu wa Polisi au Magereza au Uhamiaji au sijui nani wote wako chini yake
 
Kwanza wenye katiba hakuna sehemu inayosema mkuu wa majeshi ya ulinzi ni mkuu wa majeshi yote.

Pili, Mwamunyange ni CDF (Chief of DEFENCE forces), kiswahili chake sahihi ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (Defence). Na sio mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama.

Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ni Rais peke yake.

JKT ni sehemu ya JWTZ. Na mara nyingi wanamwitwa Mkuu wa MAjeshi badala ya Mkuu Wa Jeshi, kwa sababu MAjeshi yanamaanisha (JWTZ na JKT).

JWTZ ni jeshi la ulinzi. Polisi ni jeshi la Usalama.

Kwenye sherehe za muungano, CDF anaambatana na Rais, kwa sababu ni mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Nchi. JWTZ ndio lina mamlaka ya kuilinda Tanzania kama nchi.

Polisi wana mamlaka ya kulinda raia huru na usalama wa ndani.

Magereza wana mamlaka ya kulinda magereza na raia wafungwa.
 
nijuavyo mimi ni kwamba amri jeshi mkuu ni mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama katika mantiki ya utawala kama lilivyo jina lake amri(command) kazi yake kubwa ni kuamrisha sababu ndio kazi yake ila linapokuja swala la mkuu wa majeshi mantiki yake ni kwamba yeye anakuwa mkuu wa majeshi yote ya usalama na ulinzi katika maswala yote yanayohusu utendaji kwaiyo amri jeshi mkuu(raisi) yeye utoa amri kwa mkuu wa majeshi nae mkuu wa majeshi uibadili ile amri nakuiweka katika utendaji vile vile tunapozungumzia majeshi nayo pia yapo kwa status au ni seme grades..... mfano mgambo si sawa na polisi,kwa lugha rahisi mkuu wa majeshi analindwa na jwtz ni kwasababu,IGP nae analindwa na polisi pia ni kwasababu kwaiyo kivyeo uanza mkuu wa majeshi, majenerali wa jeshi akiwemo mnadhimu mkuu wa jeshi..........(nimekisahau cheo kinachofwata hapo) alafu IGP alafu wanafwata makamishina wote nakuendelea
 
Nimekuwa nikisumbuliwa muda mrefu na swali hili Hivi huyu mkuu wa majeshi ya ulizi tanzania Aden Mwamunyange si alikuwa JKT?

Ssa swali langu ni kwamba ilikuwaje achaguliwe kuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania na kwanini siku moja mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania asitoke jeshi la polisi au magereza?

Na tunaposema mkuu wa majeshi tunamaana kwamba ni mkuu wa majeshi yote yaani mgambo,magereza,polisi,JKT,JWTZ,TAKUKURU n,k.pia kuna tofauti gani kati ya Amirijeshi mkuu na mkuu wa majeshi?

Yaani mambo haya yananichanganya sana hasa hilo la mkuu wa majeshi ina maana rais anashauriwa kuteua mtu yeyote yule? Au ni lazima atoke JWTZ na JKT? Au hata jeshi la polisi, magereza, uhamiaji, KMKM nayo yana uwezo wa kutoa mkuu wa majeshi?

Na ukiangalia ndani ya gari la uhuru utakuta kuna Rais na mkuu wa majeshi tu yaani watu 2 tu kwanini asiongezeke IGP, Mkuu wa magereza,usalama wa taifa n,k!jamani naomba majibu kwa mada hii kwa yeyote anayefahamu maana maswali hayo najiuliza huu mwaka wa 6 sasa bado sijapata jibu labda hapa jamvini mnaweza kunisaidia swali hili!


JKT ni wing ya JWTZ; maafisa wote wa JKT (NCOs na COs) ni maafisa wa JWTZ. Tofauti iliyopo ni kuwa askariwa JKT ni askari-raia wanaosimamiwa na JWTZ, wakati askari wa JWTZ ni askari walioapishwa.
 
pole kaka kwa kujiuliza muda mrefu hivyo. nadhani ni makosa kumuita mkuu wa majeshi, cheo hicho ni cha rais na neno amiri jeshi mkuu, lina maana ya "mkuu wa jeshi mkuu" kwani neno amiri lina maana ya mkuu. cheo cha mwamunyange kinapaswa kuwa mkuu wa JWTZ na sio mkuu wa majeshi kwani JWTZ ni jeshi moja. ila kutokana na majukumu ya kulinda mipaka ya nchi na kuhakikisha uhuru wa jamhuri, ndio maana unamuona mkuu wa JWTZ akiambatana na rais kwenye sherehe za uhuru na hata za muungano.

kwa kumalizia, mkuu wa JWTZ lazima atoke JWTZ na rais humteua baada ya kushauriana na makamanda waandamizi wa JWTZ. kwa hiyo JKT ni sehemu ya JWTZ ni kama idara tu ya JWTZ. sio mwamunyange pekee bali hata shimbo alikuwa mkuu wa JKT kabla hajawa mnadhimu mkuu wa JWTZ. so ichukulie JKT kama idara mojawap ya JWTZ to make life easier. thanx kwa kunisoma

Hapana Mkuu, Davic Mwamunyange ni Mkuu wa Majeshi ya Tanzania. Kila Kila Jeshi hapa nchini lipo chini ya Mwamunyange, ila na yeye Mkuu wa Majeshi bado yupo chini ya Amiri Jeshi Mkuu.
 
JKT ni wing ya JWTZ; maafisa wote wa JKT (NCOs na COs) ni maafisa wa JWTZ. Tofauti iliyopo ni kuwa askariwa JKT ni askari-raia wanaosimamiwa na JWTZ, wakati askari wa JWTZ ni askari walioapishwa.

Hapa Kaka umenijuza kitu.
 
nashukuru sana nimekupata kaka kwa hiyo hakuna uhusiano wowote kati ya jeshi la polisi na JWTZ maana kipindi cha sherehe mbalimbali huwa naona wanacheza Rigwaride pamoja na kutoa heshima kwa pamoja
Judith amebugi man!

Mkuu wa majeshi kwa kimombo ni "Chief of Defence Forces(CDF)". Huyu ndiye mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama na pia ndiye Mwenyekiti katika vikao vya viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama(yaani majeshi(askari wa miguu, anga na majini), polisi, magereza na usalama wa Taifa)!

Amiri Jeshi Mkuu kwa kimombo ni "Commander-in-Chief". Huyu ni mkuu wa nchi au serikali ambaye kwa desturi siyo lazima awe amepitia mafunzo yo yote ya kijeshi bali ameingia madarakani kidemokrasia (kwa kupigiwa kura na wananchi) au kwa mabavu ya nguvu za jeshi! Katika masuala ya kijeshi amiri jeshi mkuu ndiye mwenye mamlaka ya kuamrisha jeshi au nchi kuingia vitani! Aidha yeye ndiye hupandisha vyeo wanajeshi na maaskari wote kwa ujumla!
 
Hivi mkuu wa majeshi wa Tanzania ni nani? maana sijasikia akiamrisha kitu?
 
Ndugu yangu nami napenda nikupe ufahamu kuhusu majeshi yetu ya ulinzi na usalama.JWTZ inajukumu la kulinda mipaka yetu yote,Jeshi la Polisi lina jukumu la kulinda watu na mali zao,Jeshi la Magereza linajukumu la kuwarekebisha tabia wale wahalifuwote wanaotumikia vifungo vyao Jela. Tunapozungumzia Mkuu wa Majeshi hapa kwetu Tanzania yaani kwa Kiengereza "Chief of Defence Forces" tunazyungumzia Mkuu wa Majeshi yote ya Ulinzi na usalama na ukitaka kuona tofauti hata ya vyeo vyao angalia Cheo cha Jenerali Mwamunyange hakifanani na yoyote hata wale walio Wakuu wa Polisi ama Magereza ila Cheo cha Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi kinafanana kwa kila namna na cha Mkuu wa Polisi hii ina maana kuwa Mkuu wa Majeshi yeye anakuwa Mkuu wa Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama Nchini. Nafasi ya Amiri Jeshi Mkuu nayo ni moja na ni Raisi wa Nchi ndiyo mwenye mamlaka ya kuwa na nafasi hiyo aambayo kwa Kiingereza inaitwa "Comender in Chief of Armied Forces"
 
Kwa kuongezea Mkuu wa Majeshi, IGP, Mkuu wa Magereza Hawa wote lazima wawe TISS ....

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Mkuu kuna vyeo ukifika jeshini unakuwa automatic TISS, masalani ili uwe Brigadier General lazima uende kozi ya ubrigedia na ndani hiyo kozi wanajifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na mfumo mzima wa usalama wa nchi. Na kwa taarifa wakuu wengi wa TISS wanatoka jeshini, refers to Maj. Gen Imrani Kombe, Col. Abson na wakuu wengi wa TISS mikoani na baadhi ya vitendo ni ma major wa jeshi. Kwa kifipi asilimia kubwa ya TISS ni wanajeshi hivyo jeshi ndo senior la majeshi yetu yote ya ulinzi na usalama.
 
JKT ni wing ya JWTZ; maafisa wote wa JKT (NCOs na COs) ni maafisa wa JWTZ. Tofauti iliyopo ni kuwa askariwa JKT ni askari-raia wanaosimamiwa na JWTZ, wakati askari wa JWTZ ni askari walioapishwa.

Acha uongo, kama hujui usipotoshe jamii, kumbuka huku jamvini huenda hata Mwamnyange akawa member so usipende kupotosha. JKT na JW wana kiapo sawa, tofauti yao tena hapa nasisitiza ni ndogo mno tena ni kimajukumu tu. linapokuja suala la core activities wote wako sawa kimajukumu.
 
Acha uongo, kama hujui usipotoshe jamii, kumbuka huku jamvini huenda hata Mwamnyange akawa member so usipende kupotosha. JKT na JW wana kiapo sawa, tofauti yao tena hapa nasisitiza ni ndogo mno tena ni kimajukumu tu. linapokuja suala la core activities wote wako sawa kimajukumu.

Wanaopenda kuonyesha vidole kuwa wenzao ni waongo, kwa kawaida huwa ndio waongo; ungekuwa umeonyesha kiwango kikubwa kwa kupinga hoja yangu bila kuniita mwongo. Hata hivyo nitakupa elimu fupi, na isipokutosha niambie nifafanue zaidi.

Ukisoma sheria ya JKT na sheria ya JWTZ utafahamu kuwa jeshi la kujenga taiofa ni kama jina lake lilivyo; "Kujenga Taifa," wakati jeshi la wanachi ni jeshi la ulinzi wa mipaka ya Tanzania. Kwa hiyo askari wa JKT "hawalazimiki" kupigana vita wakati askari wa JWTZ wanalazimika. Askari wa JKT hawezi kushitakiwa court martial wakati yule wa JWTZ anaweza kushitakiwa huko.

Nadhani wewe kinachokuahadaa ni wale maafisa wanaoendesha JKT ambao ni maafisa wa JWTZ; hakuna afisa wa JKT. Askari wa JKT ni kama vile wale wabunge waliokuwa wamekwenda kupigwa msasa hivi majuzi, na vijana wanaoweza kujiunga na jeshi hilo kwa kujitolea; hawa wanitwa Servicemen," ingawa sina uhakika pia kama kuna "Servicewomen," na kwa muda mrefu namba zao za jeshi zimekuwa zinaanza na SM (Serviceman). Hawa siyo waajiriwa wa serikali ya Tanzania. Askari wa JWTZ ambao kufupi wanajulikana kama wapiganaji, ni waajiriwa wa serikali ya Tanzania, na namba zao kwa muda mrefu zilikuwa zinaanza na MU (mlinzi wa umma.)

Tambua tena kuwa mafunzo yote ya JKT yanaendeshwa na JWTZ; ndiyo maana askari wote wanaoendesha mafunzo ya JKT kuanzia ngazi ya private mpaka Major General ni waajiriwa wa JWTZ. Maafisa wa JWTZ wanaonedesha JKT siyo askari wa JKT. Zamani kidogo wakati bado kuna jeshi la Mgambo, mambo yalikuwa hivyo hivyo; kuwa shughuli zote za kuendesha jeshi hilo zilikuwa chini ya JWTZ ingawa wanamgambo hawakuwa askari wa JWTZ, na wale askari waliokuwa wakiendesha mafunzo ya mgambo hawakuwa askari wa mgambo.

Nadhani mpaka hapo utakuwa umeelewa tofauti baina ya (a) askari wa JKT, (b) askari wa JWTZ, na (c) askari wa JWTZ wanaonedsha JKT.
 
Nimekuwa nikisumbuliwa muda mrefu na swali hili Hivi huyu mkuu wa majeshi ya ulizi tanzania Aden Mwamunyange si alikuwa JKT?

Ssa swali langu ni kwamba ilikuwaje achaguliwe kuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania na kwanini siku moja mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania asitoke jeshi la polisi au magereza?

Na tunaposema mkuu wa majeshi tunamaana kwamba ni mkuu wa majeshi yote yaani mgambo,magereza,polisi,JKT,JWTZ,TAKUKURU n,k.pia kuna tofauti gani kati ya Amirijeshi mkuu na mkuu wa majeshi?

Yaani mambo haya yananichanganya sana hasa hilo la mkuu wa majeshi ina maana rais anashauriwa kuteua mtu yeyote yule? Au ni lazima atoke JWTZ na JKT? Au hata jeshi la polisi, magereza, uhamiaji, KMKM nayo yana uwezo wa kutoa mkuu wa majeshi?

Na ukiangalia ndani ya gari la uhuru utakuta kuna Rais na mkuu wa majeshi tu yaani watu 2 tu kwanini asiongezeke IGP, Mkuu wa magereza,usalama wa taifa n,k!jamani naomba majibu kwa mada hii kwa yeyote anayefahamu maana maswali hayo najiuliza huu mwaka wa 6 sasa bado sijapata jibu labda hapa jamvini mnaweza kunisaidia swali hili!
Kilimasera;
Mkuu wa majeshi ni kifupi tu lakini neno sahihi kabisa ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama. Jeshi la Ulinzi na Usalama ndilo linalohusika na usalama wa mipaka ya nchi, aidha ndani au hata nje ya mipaka ikibidi. Haya majeshi mengine yaliyopo kama mgambo, polisi, magereza nk yanahusika zaidi na ulinzi wa raia na mali zao ndani ya nchi yao, ambayo nayo pia kwa hali hiyo yako covered na Jeshi la Ulinzi na Usalama. Yanatakiwa yalindwe na Jeshi hilo pia ili yaweze kufanya kazi zake ndani ya nchi kama inavyopaswa. Hata hivyo, inapotokea kwamba kuna korogesheni ambayo ni external, majeshi haya (yaani polisi, magerea, mgambo, n.k. ) huwa yana tabia ya kumegeka na kubadili sura na kuwa kiungo kimojawapo na muhimu cha Jeshi la ulinzi na Usalama. Pia inabidi uchukue angalizo (take note) kwamba kama wewe sasa hivi ni raia lakini uliwahi kupitia JKT, be sure kwamba ni mwajiriwa mzuri sana wa Jeshi la Ulinzi na Usalama ambaye hulipwi mshahara kwa muda huu kwa sababu huwafanyii kazi yoyote ila kama siku ikibidi mshahara wako utakuwepo na maneno utakayoyasikia masikioni mwako ni MSTARI WA MBELE basi na hautakuwa hata na nafasi ya kuuliza maswali!
 
Wanaopenda kuonyesha vidole kuwa wenzao ni waongo, kwa kawaida huwa ndio waongo; ungekuwa umeonyesha kiwango kikubwa kwa kupinga hoja yangu bila kuniita mwongo. Hata hivyo nitakupa elimu fupi, na isipokutosha niambie nifafanue zaidi.

Ukisoma sheria ya JKT na sheria ya JWTZ utafahamu kuwa jeshi la kujenga taiofa ni kama jina lake lilivyo; "Kujenga Taifa," wakati jeshi la wanachi ni jeshi la ulinzi wa mipaka ya Tanzania. Kwa hiyo askari wa JKT "hawalazimiki" kupigana vita wakati askari wa JWTZ wanalazimika. Askari wa JKT hawezi kushitakiwa court martial wakati yule wa JWTZ anaweza kushitakiwa huko.

Nadhani wewe kinachokuahadaa ni wale maafisa wanaoendesha JKT ambao ni maafisa wa JWTZ; hakuna afisa wa JKT. Askari wa JKT ni kama vile wale wabunge waliokuwa wamekwenda kupigwa msasa hivi majuzi, na vijana wanaoweza kujiunga na jeshi hilo kwa kujitolea; hawa wanitwa Servicemen," ingawa sina uhakika pia kama kuna "Servicewomen," na kwa muda mrefu namba zao za jeshi zimekuwa zinaanza na SM (Serviceman). Hawa siyo waajiriwa wa serikali ya Tanzania. Askari wa JWTZ ambao kufupi wanajulikana kama wapiganaji, ni waajiriwa wa serikali ya Tanzania, na namba zao kwa muda mrefu zilikuwa zinaanza na MU (mlinzi wa umma.)

Tambua tena kuwa mafunzo yote ya JKT yanaendeshwa na JWTZ; ndiyo maana askari wote wanaoendesha mafunzo ya JKT kuanzia ngazi ya private mpaka Major General ni waajiriwa wa JWTZ. Maafisa wa JWTZ wanaonedesha JKT siyo askari wa JKT. Zamani kidogo wakati bado kuna jeshi la Mgambo, mambo yalikuwa hivyo hivyo; kuwa shughuli zote za kuendesha jeshi hilo zilikuwa chini ya JWTZ ingawa wanamgambo hawakuwa askari wa JWTZ, na wale askari waliokuwa wakiendesha mafunzo ya mgambo hawakuwa askari wa mgambo.
Nadhani mpaka hapo utakuwa umeelewa tofauti baina ya (a) askari wa JKT, (b) askari wa JWTZ, na (c) askari wa JWTZ wanaonedsha JKT.
Kichuguu MBONA UNAZIDI KUDANGANYA?
ACHA UONGO HII STORY UNGEIACHA KWANI TULISHAIZUNGUMZIA HUMUHUMU JF NA ASKARI WOTE NI SAWA WAMAPIGANA VITA NA WAPO WALIOENDA DARFUR WAKIWEMO POLISI
Vita vya Uganda mpaka Mgambo walikuwepo bega kwa bega na JKT na askari wa akiba (Sisi Raia tuliopitia JKT tukapewa mafunzo hayo) na walikuwa zaidi kwenye Vikosi vya Infantry (Askari wa Miguu) vinavyokuwa mstari wa mbele nyuma ya vifaru na magari ya deraya
Hapo kwenye RED unapodai askari wa JKT halazimiki kupigana Vita ni kichekesho kwani inaonesha wengi wa Raia humu Nchini tukivamiwa na Manduli hasa haya yanayonyemelea nchi yetu kutoka maziwa makuu mtajificha Uvunguni mwa vitanda mama zetu na kina dada wakibakwa. (Raia wote ni Askari na mnatakiwa muende mstari wa mbele mkiongozwa na JKT ya kina Zitto na Halima Mdee)
Kwas kifupi tu JKT ni Askari wa kawaida wa JWTZ na anashtakiwa katika Court Marshal na hakimu wake ni CO wa kikosi na kufungwa Uraiani au kuachishwa Jeshi kilimasera labda kwa kuongeza Mwamunyange navyofahamu ni kweli alitoka TPDF akaenda JKT na wakati wa Utawala wa Mkapa wakati huo Mkuuwa Majeshi alikuwa Waitara na Msaidizi Gau sasa wakastaafu wote ndipo akarudishwa Mwamunyange TPDF kutokana na Rank, alipoingia JK wa awamu ya Nne akamteua kuwa CDF
WAKATI VITA IKIPIGANWA mapigano yote yanawasilishwa kwa Chief of Defence (Mkuu wa Majeshi) naye anayawasilisha kwa Commanding ni Chief ambaye ndiye Kiongozi wa nchi (Rais) Hii thread ipo humu nitakuwasilishia
 
Kichuguu MBONA UNAZIDI KUDANGANYA?
ACHA UONGO HII STORY UNGEIACHA KWANI TULISHAIZUNGUMZIA HUMUHUMU JF NA ASKARI WOTE NI SAWA WAMAPIGANA VITA NA WAPO WALIOENDA DARFUR WAKIWEMO POLISI
Vita vya Uganda mpaka Mgambo walikuwepo bega kwa bega na JKT na askari wa akiba (Sisi Raia tuliopitia JKT tukapewa mafunzo hayo) na walikuwa zaidi kwenye Vikosi vya Infantry (Askari wa Miguu) vinavyokuwa mstari wa mbele nyuma ya vifaru na magari ya deraya
Hapo kwenye RED unapodai askari wa JKT halazimiki kupigana Vita ni kichekesho kwani inaonesha wengi wa Raia humu Nchini tukivamiwa na Manduli hasa haya yanayonyemelea nchi yetu kutoka maziwa makuu mtajificha Uvunguni mwa vitanda mama zetu na kina dada wakibakwa. (Raia wote ni Askari na mnatakiwa muende mstari wa mbele mkiongozwa na JKT ya kina Zitto na Halima Mdee)
Kwas kifupi tu JKT ni Askari wa kawaida wa JWTZ na anashtakiwa katika Court Marshal na hakimu wake ni CO wa kikosi na kufungwa Uraiani au kuachishwa Jeshi kilimasera labda kwa kuongeza Mwamunyange navyofahamu ni kweli alitoka TPDF akaenda JKT na wakati wa Utawala wa Mkapa wakati huo Mkuuwa Majeshi alikuwa Waitara na Msaidizi Gau sasa wakastaafu wote ndipo akarudishwa Mwamunyange TPDF kutokana na Rank, alipoingia JK wa awamu ya Nne akamteua kuwa CDF
WAKATI VITA IKIPIGANWA mapigano yote yanawasilishwa kwa Chief of Defence (Mkuu wa Majeshi) naye anayawasilisha kwa Commanding ni Chief ambaye ndiye Kiongozi wa nchi (Rais) Hii thread ipo humu nitakuwasilishia

Nafikiri wewe hujui tofauti baina ya maafisa wa JWTZ wanaoendesha JKT na askari wa JKT ambao siku hizi ni volunteer tu; zamani kulikuwa na askari wa JKT kwa mujibu wa sheria, ingawa nilisoma tena siku za hivi karibuni kuwa kulikuwa na plani ya kurudisha ule utaratibu wa mujibu wa sheria. Ukijua tofauti hzio ndipo utagundua kwa nini nyota za maafisa wa JKT zina maandishi ya JWTZ na wala siyo JKT. Vile vile uniform za maafisa wote wa wanaonedsha JKT zina nembo ya JWTZ wala siyo ya JWTZ. Askari wa JKT anapomaliza mafunzo yake huko JKT hupewa cheti chenye na nembo ya JKT siyo ya JWTZ.

Ingawa sisi Tanzania tumezwea kufanya mambo bila kuangalia sheria, basi kwa taarifa yako ni kuwa kisheria askari wa JKT (yaani wale volunteer siyo wale wa JWTZ wanaondesha JKT) wanaweza kabisa wakakataa kwenda vitani na kisheria wasishitakiwe popote, kwa sababu hawana mkataba wa namna hiyo. Juzi juzi wabunge walipokuwa kwenye makambi ya JKT wasingeweza kupelekwa vitani kwa nguvu. Yale mashitaka yanayoendeshwa kwenye kambini za JKT chini ya CO kutunza nidhamu ya kambi siyo court martial hiyo!.

Unaweza kueleza ni kwa nini iwapo JKT ni jeshi kama JWTZ kwa nini maafisa wake wasitumie nembo yao kama vile ilivyo majeshi mengine ya polisi na magereza, badala yake wanatumia nembo ya JWTZ na kuiacha ile ya JKT.

Kuhusu polisi na magereza kwenda vitani, hiyo ni sehemu ya majukumu yao wakati wakitakiwa kufanya hivyo na amiri jeshi mkuu.
 
Nimekuwa nikisumbuliwa muda mrefu na swali hili Hivi huyu mkuu wa majeshi ya ulizi tanzania Aden Mwamunyange si alikuwa JKT?

Ssa swali langu ni kwamba ilikuwaje achaguliwe kuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania na kwanini siku moja mkuu wa majeshi ya ulinzi tanzania asitoke jeshi la polisi au magereza?

Na tunaposema mkuu wa majeshi tunamaana kwamba ni mkuu wa majeshi yote yaani mgambo,magereza,polisi,JKT,JWTZ,TAKUKURU n,k.pia kuna tofauti gani kati ya Amirijeshi mkuu na mkuu wa majeshi?

Yaani mambo haya yananichanganya sana hasa hilo la mkuu wa majeshi ina maana rais anashauriwa kuteua mtu yeyote yule? Au ni lazima atoke JWTZ na JKT? Au hata jeshi la polisi, magereza, uhamiaji, KMKM nayo yana uwezo wa kutoa mkuu wa majeshi?

Na ukiangalia ndani ya gari la uhuru utakuta kuna Rais na mkuu wa majeshi tu yaani watu 2 tu kwanini asiongezeke IGP, Mkuu wa magereza,usalama wa taifa n,k!jamani naomba majibu kwa mada hii kwa yeyote anayefahamu maana maswali hayo najiuliza huu mwaka wa 6 sasa bado sijapata jibu labda hapa jamvini mnaweza kunisaidia swali hili!

ni Davis Mwamunyange! Huyo Aden Mwamunyange ni yupi?
 
Ukijua tofauti hzio ndipo utagundua kwa nini nyota za maafisa wa JKT zina maandishi ya JWTZ na wala siyo JKT. Vile vile uniform za maafisa wote wa wanaonedsha JKT zina nembo ya JWTZ wala siyo ya JWTZ. Askari wa JKT anapomaliza mafunzo yake huko JKT hupewa cheti chenye na nembo ya JKT siyo ya JWTZ.
Unaweza kueleza ni kwa nini iwapo JKT ni jeshi kama JWTZ kwa nini maafisa wake wasitumie nembo yao kama vile ilivyo majeshi mengine ya polisi na magereza, badala yake wanatumia nembo ya JWTZ na kuiacha ile ya JKT.
Kuhusu polisi na magereza kwenda vitani, hiyo ni sehemu ya majukumu yao wakati wakitakiwa kufanya hivyo na amiri jeshi mkuu.
samahani Kichuguu labda nimetoka nje au tuko sawa lakini kwa ninavyojua JWTZ (TPDF) ndilo hubeba JKT (National Service)
JWTZ chini ya Davis Mwamunyange ;

images
lina
Air Force -Jeshi la Anga
Land Force (Infanttry) Jeshi la Ardhini
na Navy Jeshi la Majini
Baada ya hapo ndipo kuna JKT
Vikosi vyote vipo chini JWTZ na mafunzo yao hutolewa
katika Vyuo vya Kijeshi na walimu wa JWTZ
Kama ni NCO's Koplo mpaka Staff mafunzo yanaweza tolewa kwenye makambi yoyote hata ya JKT
ila CO's
(Luteni Usu hadi Captan) zaidi ni Monduli walikokuwa J.K na Kinana km walimu wa Siasa
zaidi ya hapo Kanali nk wanaenda Israel China nk

JKT ni kwa mujibu wa sheria ndio maana wanaenda kuchukua uzoefu Raia wa Tanzania (ni bora iwe kwa wote km Israel au Marekani kwa wasomi)

Kuhusu Coury Marshal ni kweli kabisa huwa ni kwa ngazi za juu. Ila Mkuu wa kikosi chochote (CO) ana ruksa ya kuamua Kesi au kukufunga chini ya siku 90 Brigedia wa Brigeni yeye zaidi anahusika na Kesi za Nidhamu

Force namba za JKT zilanza na alphabeti A naona zimeshamaliza Z
JWTZ wanatumia MT kwa wanaume na wanawake ni MTM

MAGEREZA, POLISI, UHAMIAJI, TAKUKURU Vikosi hivi vipo chini ya Wizara ya mambo ya ndani na vingine ikulu lakini tunasema wakati wa dharura vitahusika na na JWTZ km JKT

kwa hiyo JKT ni Jeshi lililo chini ya JWTZ lililopo kwa mujibu wa Sheria
 
Last edited by a moderator:
Mwamunyange ni mkuu wa Majeshi Tanzania,ikiwa na maana majeshi yotee ktk Taifa hili, na ni kwanini wengi wao hutoka JKT (Hili swali liliwahi ulizwa kwa Kanali Mkisi alipokuwa akitoa aelimu ya uraia Jeshini), Alisema hii ni sehemu ya kuangalia utendaji kazi wa Msoja,Jkt ni mtoto wa Jw hivyo CDF na baadhi ya masoja waandamizi (Brigediaz) kabla kuchaguliwa huletwa Jkt kupima ufanisi wao,ikumbukwe kuwa Infatria wengi ndiyo huchukua Madaraka ya juu ya Jeshi na JKT NI command ya Jw ktk infantry. Pia hata Masoja waliopo Jkt ni wanapiga kazi ya kutosha ongeza na ile ya kumtafutia mkubwa CHOCHOTE (SUMA JKT) rejea kwa Shimbo na Mradi wa Trekta MWENGE,WANAJESHI WA TZ UMOJA WA TAIFA
 
Back
Top Bottom