Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

Mkuu wa Majeshi lazima atoke Jeshi la Kujenga Taifa?

Wanaopenda kuonyesha vidole kuwa wenzao ni waongo, kwa kawaida huwa ndio waongo; ungekuwa umeonyesha kiwango kikubwa kwa kupinga hoja yangu bila kuniita mwongo. Hata hivyo nitakupa elimu fupi, na isipokutosha niambie nifafanue zaidi.

Ukisoma sheria ya JKT na sheria ya JWTZ utafahamu kuwa jeshi la kujenga taiofa ni kama jina lake lilivyo; "Kujenga Taifa," wakati jeshi la wanachi ni jeshi la ulinzi wa mipaka ya Tanzania. Kwa hiyo askari wa JKT "hawalazimiki" kupigana vita wakati askari wa JWTZ wanalazimika. Askari wa JKT hawezi kushitakiwa court martial wakati yule wa JWTZ anaweza kushitakiwa huko.

Nadhani wewe kinachokuahadaa ni wale maafisa wanaoendesha JKT ambao ni maafisa wa JWTZ; hakuna afisa wa JKT. Askari wa JKT ni kama vile wale wabunge waliokuwa wamekwenda kupigwa msasa hivi majuzi, na vijana wanaoweza kujiunga na jeshi hilo kwa kujitolea; hawa wanitwa Servicemen," ingawa sina uhakika pia kama kuna "Servicewomen," na kwa muda mrefu namba zao za jeshi zimekuwa zinaanza na SM (Serviceman). Hawa siyo waajiriwa wa serikali ya Tanzania. Askari wa JWTZ ambao kufupi wanajulikana kama wapiganaji, ni waajiriwa wa serikali ya Tanzania, na namba zao kwa muda mrefu zilikuwa zinaanza na MU (mlinzi wa umma.)

Tambua tena kuwa mafunzo yote ya JKT yanaendeshwa na JWTZ; ndiyo maana askari wote wanaoendesha mafunzo ya JKT kuanzia ngazi ya private mpaka Major General ni waajiriwa wa JWTZ. Maafisa wa JWTZ wanaonedesha JKT siyo askari wa JKT. Zamani kidogo wakati bado kuna jeshi la Mgambo, mambo yalikuwa hivyo hivyo; kuwa shughuli zote za kuendesha jeshi hilo zilikuwa chini ya JWTZ ingawa wanamgambo hawakuwa askari wa JWTZ, na wale askari waliokuwa wakiendesha mafunzo ya mgambo hawakuwa askari wa mgambo.

Nadhani mpaka hapo utakuwa umeelewa tofauti baina ya (a) askari wa JKT, (b) askari wa JWTZ, na (c) askari wa JWTZ wanaonedsha JKT.

KIAPO NI KILE KILE,tofauti penye jw unaweka Jkt na pia mafunzo ya vijana Jkt yanaweza tolewa na Volunteer leaders,hawa ni askari wa jkt waliopata course ya instructors. Na kuhusu kushitakiwa ukibainika ulipitia Jkt na upo ndani ya mkataba na Jkt unashtakiwa Kijeshi.
kuhusu vita kuna vigezo vya kumpeleka askari kule mojawapo ni kuwa lazima askari huyo awe amepiga kozi ya Level 1,nje ya hapo haendi, kumbuka kuna privates wa Jeshi hawajapiga hiyo course! na juu ya askari wa jkt kwenda vitani inawezekana kabsa kama atakidhi viwango tajwa hapo juu.
 
Kichuguu MBONA UNAZIDI KUDANGANYA?
ACHA UONGO HII STORY UNGEIACHA KWANI TULISHAIZUNGUMZIA HUMUHUMU JF NA ASKARI WOTE NI SAWA WAMAPIGANA VITA NA WAPO WALIOENDA DARFUR WAKIWEMO POLISI
Vita vya Uganda mpaka Mgambo walikuwepo bega kwa bega na JKT na askari wa akiba (Sisi Raia tuliopitia JKT tukapewa mafunzo hayo) na walikuwa zaidi kwenye Vikosi vya Infantry (Askari wa Miguu) vinavyokuwa mstari wa mbele nyuma ya vifaru na magari ya deraya
Hapo kwenye RED unapodai askari wa JKT halazimiki kupigana Vita ni kichekesho kwani inaonesha wengi wa Raia humu Nchini tukivamiwa na Manduli hasa haya yanayonyemelea nchi yetu kutoka maziwa makuu mtajificha Uvunguni mwa vitanda mama zetu na kina dada wakibakwa. (Raia wote ni Askari na mnatakiwa muende mstari wa mbele mkiongozwa na JKT ya kina Zitto na Halima Mdee)
Kwas kifupi tu JKT ni Askari wa kawaida wa JWTZ na anashtakiwa katika Court Marshal na hakimu wake ni CO wa kikosi na kufungwa Uraiani au kuachishwa Jeshi kilimasera labda kwa kuongeza Mwamunyange navyofahamu ni kweli alitoka TPDF akaenda JKT na wakati wa Utawala wa Mkapa wakati huo Mkuuwa Majeshi alikuwa Waitara na Msaidizi Gau sasa wakastaafu wote ndipo akarudishwa Mwamunyange TPDF kutokana na Rank, alipoingia JK wa awamu ya Nne akamteua kuwa CDF
WAKATI VITA IKIPIGANWA mapigano yote yanawasilishwa kwa Chief of Defence (Mkuu wa Majeshi) naye anayawasilisha kwa Commanding ni Chief ambaye ndiye Kiongozi wa nchi (Rais) Hii thread ipo humu nitakuwasilishia

Huyu jamaa sijui yukoje! Asante kwa kumpa darasa.
 
ipi tofauti ya Kamandi, Brigedi na Kikosi.

Kwa ufupi,Jw wana kamandi ya Jeshi la anga, Ardhini,Majini..
Askari wa Ardhini ndani yake kuna Jkt,Mizinga,komandoo(Comando wapo kamandi zote). Brigedi hapa wamegawanya Vikosi vya jeshi kikanda mfano kunaweza kuwepo na brigedi ya kusini,kaskazini nk.......Wanakuja
Karibu Jkt.
 
Kwa ufupi,Jw wana kamandi ya Jeshi la anga, Ardhini,Majini..
Askari wa Ardhini ndani yake kuna Jkt,Mizinga,komandoo(Comando wapo kamandi zote). Brigedi hapa wamegawanya Vikosi vya jeshi kikanda mfano kunaweza kuwepo na brigedi ya kusini,kaskazini nk.......Wanakuja
Karibu Jkt.

ahsante mkuu
 
Tanzania tuna komand 4, nazo ni komand ya ardhi(infantria), anga (air force) , maji (navy) na jkt. Swala linakuja ni kwamba jkt ni jeshi la vijana huku walimu wao wakiwa ni tpdf. So kinachotokea ili wewe wa tpdf uje kufundisha jkt inabidi uende kozi na hapo unakuwa upo komand ya jkt. Hata viongozi wa jkt wao ni tpdf !. Mkuu wa majeshi ni lazima atoke tpdf/jkt. Cause hauwezi kufananisha mtu aliyepita tpdf na yule aliyepita polisi/mageleza, hizo ni different aspect !. Na hata kwenye system za majeshi ya hapa bongo tpdf ndio masenior wa majeshi yote.
 
Tanzania tuna komand 4, nazo ni komand ya ardhi(infantria), anga (air force) , maji (navy) na jkt. Swala linakuja ni kwamba jkt ni jeshi la vijana huku walimu wao wakiwa ni tpdf. So kinachotokea ili wewe wa tpdf uje kufundisha jkt inabidi uende kozi na hapo unakuwa upo komand ya jkt. Hata viongozi wa jkt wao ni tpdf !. Mkuu wa majeshi ni lazima atoke tpdf/jkt. Cause hauwezi kufananisha mtu aliyepita tpdf na yule aliyepita polisi/mageleza, hizo ni different aspect !. Na hata kwenye system za majeshi ya hapa bongo tpdf ndio masenior wa majeshi yote.

wakuu, nisaidieni kunijuza kuhusu cheo cha Brigedia General, ni sahihi kutamkwa hivo? kwa nini sio Brigedia? nilivo kuwa nafahamu mimi vyeo vya jeshi kuanzia Meja, Lt Kanali, Kanali, Brigedia, Meja General, Lt General na General. Hapa ktk vyeo hivi kuanzia Meja nembo ya ngao ya adamu na eva ipo kote? so please anaye jua naomba anijuze.
 
wakuu, nisaidieni kunijuza kuhusu cheo cha Brigedia General, ni sahihi kutamkwa hivo? kwa nini sio Brigedia? nilivo kuwa nafahamu mimi vyeo vya jeshi kuanzia Meja, Lt Kanali, Kanali, Brigedia, Meja General, Lt General na General. Hapa ktk vyeo hivi kuanzia Meja nembo ya ngao ya adamu na eva ipo kote? so please anaye jua naomba anijuze.

Brigadier na brigadier general ni kitu kile kile ila jina limebadilika kutokana na umoja wa commonwealth

Rank insignia za jwtz zipo hapo chini kwenye hiyo liink

Tanzania Peoples’ Defence Force - Land Forces / Jeshi la Wananchi la Tanzania - JWTZ
 
Back
Top Bottom