Mkuu wa Mkoa Simiyu atenguliwa, Kenan Kihongosi achukua nafasi hiyo

Mkuu wa Mkoa Simiyu atenguliwa, Kenan Kihongosi achukua nafasi hiyo

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
uteuzi.jpg

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Viongozi kama ifuatavyo:
1. Amemteua Bw. Kenan Laban Kihongosi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Kabla ya uteuzi, Bw. Kihongosi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba. Bw. Kihongosi anachukua nafasi ya Dkt. Yahaya Ismail Nawanda ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

2. Amemteua Bw. Elias Daniel Mwandobo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba. Kabla uteuzi, Bw. Mwandobo alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais Ikulu.

3. Amemteua Bw. Christopher Magala kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu. Bw. Magala anachukua nafasi ya Dkt. Stephen Isaac Mwakajumilo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

4. Amemteua Bw. George Hillary Herbet kuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani. Kabla ya uteuzi, Bw. Herbet alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani.

Uapisho wa Mkuu wa Mkoa na Msajili wa Mahakama ya Rufani utafayika kwa tarehe itakayopangwa baadaye.

====

Pias soma: MCL: Mkuu wa Mkoa adaiwa kumlawiti mwanafunzi
 
Itakuwa baada ya uchunguzi dhidi yake kukamilika juu ya tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Ukimya uliokuwepo kwa hizi siku mbili itakuwa ndio walikuwa wakiendelea kufanya uchunguzi wao, now wamejiridhisha kweli ametenda sasa kesi iende mahakamani, wasimlinde mhalifu kama walivyomlinda Gekul.
 
Back
Top Bottom