Mkuu wa mkoa wa Kivu kasikazini auliwa na M23

Mkuu wa mkoa wa Kivu kasikazini auliwa na M23

Twin_Kids

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2016
Posts
3,692
Reaction score
5,647
Major General Peter NKUBA CHIRIMWAMI, mkuu wa jeshi na mkuu wa mkoa wa Kivu Kasikazini, jana tarehe 23 Januari 2025, majira ya saa moja na dakika 44 usiku,alipokuwa amewatembelea wanajeshi wake kuwaunga mkono katika vita na kundi la waasi la M23, alimiminiwa risasi na kufariki hapo hapo.

Baada ya waasi hao kukalia mji mdogo wa SAKE, MONUSCO na SAMIDRC waliamua kuwafuata mjini humo kuwafukuza. Kama ilivyo vitani, hairuhusiwi kufyatulia risasi wanajeshi wa umoja wa mataifa.

Hivyo, baada ya kuwa na taarifa kwamba makundi hayo yatakuja, walijigawa(M23), na kuacha barabara nyeupe. Lakini waliitahadhalisha MONUSCO kwamba ikiachia risasi, na yenyewe itashughulikiwa.

SAMIRDC ambayo imeundwa na Afrika Kusini,Tanzania na Malawi, M23 ilisema yenyewe lazima wazichape. Basi katika uwepo wake kiongozi huyo, huku maeneo yaliyozingira barabara hiyo itokayo Goma kwenda SAKE, ndipo risasi zikaanza kulindima.

Baada ya kifo cha kiongozi huyo, maiti yake haikukamatwa, maana wenzake walimuchukua na kuondoka nae.

Pamoja na hayo, nchi za ugaibuni zimewaomba raia wake waishio mjini Goma kuhakikisha wanaondoka humo, na kwamba msaada wa haraka unaweza tolewa kwa waliopo Kinshasa tu. Siku ya jana,wengi wao walipaki mizigo wakielekea nchini Rwanda.
Mpaka sasa, mapigano yanaendelea.
 
Unajua muundo wa jeshi husika unatofautiana,

Labda nikuulize vita ya Urusi na Ukrainia wamekufa generals wangap?

Huyo Gen wa Congo kuna mawili tu .
Huwez kufananisha vita vya Ukraine vs Russia na vya Congo, huko unaweza ukawa uko zako vikindu mbagala mtu Yuko Kibaigwa Dodoma na anakutungua vizuri kabisa.
 
Major General Peter NKUBA CHIRIMWAMI, mkuu wa jeshi na mkuu wa mkoa wa Kivu Kasikazini, jana tarehe 23 Januari 2025, majira ya saa moja na dakika 44 usiku,alipokuwa amewatembelea wanajeshi wake kuwaunga mkono katika vita na kundi la waasi la M23, alimiminiwa risasi na kufariki hapo hapo.

Baada ya waasi hao kukalia mji mdogo wa SAKE, MONUSCO na SAMIDRC waliamua kuwafuata mjini humo kuwafukuza. Kama ilivyo vitani, hairuhusiwi kufyatulia risasi wanajeshi wa umoja wa mataifa.

Hivyo, baada ya kuwa na taarifa kwamba makundi hayo yatakuja, walijigawa(M23), na kuacha barabara nyeupe. Lakini waliitahadhalisha MONUSCO kwamba ikiachia risasi, na yenyewe itashughulikiwa.

SAMIRDC ambayo imeundwa na Afrika Kusini,Tanzania na Malawi, M23 ilisema yenyewe lazima wazichape. Basi katika uwepo wake kiongozi huyo, huku maeneo yaliyozingira barabara hiyo itokayo Goma kwenda SAKE, ndipo risasi zikaanza kulindima.

Baada ya kifo cha kiongozi huyo, maiti yake haikukamatwa, maana wenzake walimuchukua na kuondoka nae.

Pamoja na hayo, nchi za ugaibuni zimewaomba raia wake waishio mjini Goma kuhakikisha wanaondoka humo, na kwamba msaada wa haraka unaweza tolewa kwa waliopo Kinshasa tu. Siku ya jana,wengi wao walipaki mizigo wakielekea nchini Rwanda.
Mpaka sasa, mapigano yanaendelea.
Rwanda ikemewe vikali na jumuiya ya kimataifa iache kuharibu amani ya Drc.
 
Major General Peter NKUBA CHIRIMWAMI, mkuu wa jeshi na mkuu wa mkoa wa Kivu Kasikazini, jana tarehe 23 Januari 2025, majira ya saa moja na dakika 44 usiku,alipokuwa amewatembelea wanajeshi wake kuwaunga mkono katika vita na kundi la waasi la M23, alimiminiwa risasi na kufariki hapo hapo.

Baada ya waasi hao kukalia mji mdogo wa SAKE, MONUSCO na SAMIDRC waliamua kuwafuata mjini humo kuwafukuza. Kama ilivyo vitani, hairuhusiwi kufyatulia risasi wanajeshi wa umoja wa mataifa.

Hivyo, baada ya kuwa na taarifa kwamba makundi hayo yatakuja, walijigawa(M23), na kuacha barabara nyeupe. Lakini waliitahadhalisha MONUSCO kwamba ikiachia risasi, na yenyewe itashughulikiwa.

SAMIRDC ambayo imeundwa na Afrika Kusini,Tanzania na Malawi, M23 ilisema yenyewe lazima wazichape. Basi katika uwepo wake kiongozi huyo, huku maeneo yaliyozingira barabara hiyo itokayo Goma kwenda SAKE, ndipo risasi zikaanza kulindima.

Baada ya kifo cha kiongozi huyo, maiti yake haikukamatwa, maana wenzake walimuchukua na kuondoka nae.

Pamoja na hayo, nchi za ugaibuni zimewaomba raia wake waishio mjini Goma kuhakikisha wanaondoka humo, na kwamba msaada wa haraka unaweza tolewa kwa waliopo Kinshasa tu. Siku ya jana,wengi wao walipaki mizigo wakielekea nchini Rwanda.
Mpaka sasa, mapigano yanaendelea.
Wachapane, wateke maeneo,wajitangazie Uhuru, it's time congo iwe nchi mbili, Vita iishe, ilitokea Ethiopia na Eritrea, Sudan, na South Sudan,
 
Mara kadhaa rwanda inakana kuhusika ktk mzozo wa eastern congo
Kukubali au kukataa ni ngumu mzee. Mashariki mwa DRC kabla ya mipaka ya wakoloni, na kipande cha Uganda, kulikuwa Rwanda. Mpaka leo, wakazi wa maeneo hayo bado wanaongea kinyarwanda pure kabisa. Na wana ndugu nchini Rwanda. Mganda au Mkongo anaeongea kinyarwanda, huwezi mtofautisha na mnyarwanda wa Rwanda. Kwa hiyo, hata mnyarwanda akiwepo, si rahisi kumtofautisha na wakazi hao wa nchi hizo. Na hiki kimekuwa kitendawili kwa yeyote. Haya nayaongea kama mimi. Serikali ya Rwanda ihusike isihusike, haijulikani. Ila sasa, ukiangalia kinachoendelea pale, hakina tofauti na Russia vs Ukraine. Mataifa mbalimbali yapo, japo kwa inovyoonekana, kuna muasi furani anatembeza kichapo hadi watu wanarukwa na akili.. Hakika nae anapoteza, ila si kwa kiasi kikubwa. Mkongo, Mrundi, wanalia
 
Mzimu wa M23 ni hatari sana kwa mustakabali wa mashariki ya DRC.
Mzaha mzaha hao jamaa kuna siku wataichukua Goma na kutangaza Taifa linguine katikati ya DRC na Rwanda.

DRC wana resourcea nyingi sana kuanzia Katanga province, kuja huku mashariki mpaka maeneo ya Kisangani yote, wangekaa chini mataifa yote ya Africa na kuangalia uwezekano wa kuigawa hiyo nchi maana imeonekana hata kiutawala imewashinda.
 
Mzimu wa M23 ni hatari sana kwa mustakabali wa mashariki ya DRC.
Mzaha mzaha hao jamaa kuna siku wataichukua Goma na kutangaza Taifa linguine katikati ya DRC na Rwanda.

DRC wana resourcea nyingi sana kuanzia Katanga province, kuja huku mashariki mpaka maeneo ya Kisangani yote, wangekaa chini mataifa yote ya Africa na kuangalia uwezekano wa kuigawa hiyo nchi maana imeonekana hata kiutawala imewashinda.
Dawa hapa mwenye nayo ni mtoto mdogo Traore, lakini anahusika na ya kwake kwanza. Hii vita ni kama ile movie ya No retreat no surrender. Ukija kuangalia kila upande una support. Sasa hivi DRC inasema M23 inapewa support na UGANDA, KENYA na RWANDA. Burundi nae majuzi alisema isiwe tabu kuona jirani yake anapewa msaada(japo taarifa za chini ya carpet zinasema aliyetamka maneno hayo nae huenda akawa tayari yupo sebure moja a Generali Chilimwami wakishea kinywaji) bado hazijahakikiwa. Unadhani hapo kuna FDLR karibu na Rwanda tena? Litabaki zoezi la kuifuata ilipokimbilia. Watu wanajichukulia yvao bhana
 
Nimefurahi sana kusikia hili jambo.
Congo wameilaani wenyewe kwa mikono yao walipomwaga damu za wenzao, na juzi wameendelea kuilaani kwa kuwaua wale watoto waovu bila kujali kuwa uovu ule wa panya road ulisababishwa na uongozi mbovu.
Huu ni mwanzo tu , DRC itaharibika zaidi
 
hivi kuna trend huko tiktok za wale kundi la kuluna nn kilitokea had wakawa executed vile? inauma had trump akasema anataka raia wawili wamarekani malanga na mwenzie warudishwe marekani haraka na videos zinaonesja wamerudishwa whats going on??
 
Back
Top Bottom