Mkuu wa mkoa wa Kivu kasikazini auliwa na M23

Mkuu wa mkoa wa Kivu kasikazini auliwa na M23

Mzimu wa M23 ni hatari sana kwa mustakabali wa mashariki ya DRC.
Mzaha mzaha hao jamaa kuna siku wataichukua Goma na kutangaza Taifa linguine katikati ya DRC na Rwanda.

DRC wana resourcea nyingi sana kuanzia Katanga province, kuja huku mashariki mpaka maeneo ya Kisangani yote, wangekaa chini mataifa yote ya Africa na kuangalia uwezekano wa kuigawa hiyo nchi maana imeonekana hata kiutawala imewashinda.
Unaigawaje nchi ya watu?
DRC ni mali ya wakongo, vita iishe na ardhi ibakie kwa wakongomani.
Hiyo vita inaweza kuisha ndani ya mwezi mmoja tu ikiwa nchi za Africa kwa umoja wake zikiamua iishe. Tatizo wakuu wa nchi za Afrika wamejaa unafiki.
 
Unaigawaje nchi ya watu?
DRC ni mali ya wakongo, vita iishe na ardhi ibakie kwa wakongomani.
Hiyo vita inaweza kuisha ndani ya mwezi mmoja tu ikiwa nchi za Africa kwa umoja wake zikiamua iishe. Tatizo wakuu wa nchi za Afrika wamejaa unafiki.

Nchi za Africa hazina uwezo.
DRC ilishatekwa kama Africa yote ilivyotekwa, Kwa sasa ni mali ya walioiteka.
Dunia hii haihitaji huruma ya watu wengine ili usurvive, it's survival of the fittest.

Africa yenyewe yote imetekwa Iko chini ya maharamia, maharamia ndio player wa game all over.

Africa tuna njaa, hatuna nguvu, hatuna akili aka wanasesere.
 
Maj Gen anakufaje kizembe hivyo? Tatizo la Africa vyeo vingi jeshini haviendani na uwezo wa muhsika

Ambush Mzee, ukipigwa ambush unakuwa offguard, Rossevart/Truman waliamulu Gen McCarthy akimbilie Australia haraka baada ya kichaa cha Japs kupanda waliogopa angeweza kutekwa au kuuwawa Pacific.

Majeshi mengi ya Africa hayana resource na technolojia ya kutosha kuweza kusurvive front line.
 
tuseme amechomeshwa na double agent uwanja wa vita....wamelengaje gari yake tu
Mkuu, mambo ya jeshi waachie wenyewe. Kikubwa ameshakaa pembeni, hapo lazima watu wapoteze morali kidogo, na ukizingatia waliobaki wamezingilwa, imani tu ni kwamba kwa kuwa si rahisi M23 kupigana na MONUSCO, basi wanatumia mwamvuli huo. Hivyo kila mtu haelewi hili wala lile
 
Mkuu, mambo ya jeshi waachie wenyewe. Kikubwa ameshakaa pembeni, hapo lazima watu wapoteze morali kidogo, na ukizingatia waliobaki wamezingilwa, imani tu ni kwamba kwa kuwa si rahisi M23 kupigana na MONUSCO, basi wanatumia mwamvuli huo. Hivyo kila mtu haelewi hili wala lile
wajeshi wa Drcongo mzigo kwelikweli
 
Major General Peter NKUBA CHIRIMWAMI, mkuu wa jeshi na mkuu wa mkoa wa Kivu Kasikazini, jana tarehe 23 Januari 2025, majira ya saa moja na dakika 44 usiku,alipokuwa amewatembelea wanajeshi wake kuwaunga mkono katika vita na kundi la waasi la M23, alimiminiwa risasi na kufariki hapo hapo.

Baada ya waasi hao kukalia mji mdogo wa SAKE, MONUSCO na SAMIDRC waliamua kuwafuata mjini humo kuwafukuza. Kama ilivyo vitani, hairuhusiwi kufyatulia risasi wanajeshi wa umoja wa mataifa.

Hivyo, baada ya kuwa na taarifa kwamba makundi hayo yatakuja, walijigawa(M23), na kuacha barabara nyeupe. Lakini waliitahadhalisha MONUSCO kwamba ikiachia risasi, na yenyewe itashughulikiwa.

SAMIRDC ambayo imeundwa na Afrika Kusini,Tanzania na Malawi, M23 ilisema yenyewe lazima wazichape. Basi katika uwepo wake kiongozi huyo, huku maeneo yaliyozingira barabara hiyo itokayo Goma kwenda SAKE, ndipo risasi zikaanza kulindima.

Baada ya kifo cha kiongozi huyo, maiti yake haikukamatwa, maana wenzake walimuchukua na kuondoka nae.

Pamoja na hayo, nchi za ugaibuni zimewaomba raia wake waishio mjini Goma kuhakikisha wanaondoka humo, na kwamba msaada wa haraka unaweza tolewa kwa waliopo Kinshasa tu. Siku ya jana,wengi wao walipaki mizigo wakielekea nchini Rwanda.
Mpaka sasa, mapigano yanaendelea.
Ni hatari kubwa sana.

Drc igawanwe tu,
Wachapane, wateke maeneo,wajitangazie Uhuru, it's time congo iwe nchi mbili, Vita iishe, ilitokea Ethiopia na Eritrea, Sudan, na South Sudan,
Hata ikigawanywa na tatizo la msingi linaendelea kubaki kama lilivyo, basi Vita hiyo haitamalizika Bali itaendelea
 
Mimi naona kama waasi watakosa support ya silaha, magari na fedha
Vita itaisha mapema tuu
Hahahahahaha nimeipenda hiyo ndugu. Unadhani M23 kiuharisia ni waasi wenye nguvu ya kulivaa taifa hivi hivi? Hapa inasemekana M23 ina msaada wa Rwanda, Uganda na Kenya. Burundi ilikuwa upande wa DRC, imeshanyoosha mikono na kuondoka. Ripoti ya Umoja wa mataifa, mpaka sasa inasema machimbo ya madini karibia yote yameshakuwa mali ya M23, wachimbaji wanafanya kazi kwa kasi ya ajabu, baada ya kulipwa vizuri. Je, unadhani madini yakiuzwa hawapati pesa? Kuhusu siraha, asikudanganye mtu, hakuna vita visivyo na wafadhili. Wauzaji wa siraha ni wengi, wanachokitaka ni pesa tu. Wamepora siraha nyingi sana, wasaliti jeshini hawakosi. Na ukisikia kwa makini sif za M23,ina snippers na ma Commando wa kutumia tu mikono yao, visu na shoka. Je, hawa watu unadhani ni wa mchezo? Taarifa za chini chini zilizopo, japo kama kweli nchi moja wapo inayohusishwa kama kweli inahusika, kinachosubiliwa ni neno anzeni tu. Maana giza lililopo Goma,inasemekana limetengeneza mazingira ya watu kuingia. Na cha ajabu, kundi la wazalendo, nguo wameshavua na hawataki tena kujihusisha na vita, bado kukabidhi siraha tu.
 
Hahahahahaha nimeipenda hiyo ndugu. Unadhani M23 kiuharisia ni waasi wenye nguvu ya kulivaa taifa hivi hivi? Hapa inasemekana M23 ina msaada wa Rwanda, Uganda na Kenya. Burundi ilikuwa upande wa DRC, imeshanyoosha mikono na kuondoka. Ripoti ya Umoja wa mataifa, mpaka sasa inasema machimbo ya madini karibia yote yameshakuwa mali ya M23, wachimbaji wanafanya kazi kwa kasi ya ajabu, baada ya kulipwa vizuri. Je, unadhani madini yakiuzwa hawapati pesa? Kuhusu siraha, asikudanganye mtu, hakuna vita visivyo na wafadhili. Wauzaji wa siraha ni wengi, wanachokitaka ni pesa tu. Wamepora siraha nyingi sana, wasaliti jeshini hawakosi. Na ukisikia kwa makini sif za M23,ina snippers na ma Commando wa kutumia tu mikono yao, visu na shoka. Je, hawa watu unadhani ni wa mchezo? Taarifa za chini chini zilizopo, japo kama kweli nchi moja wapo inayohusishwa kama kweli inahusika, kinachosubiliwa ni neno anzeni tu. Maana giza lililopo Goma,inasemekana limetengeneza mazingira ya watu kuingia. Na cha ajabu, kundi la wazalendo, nguo wameshavua na hawataki tena kujihusisha na vita, bado kukabidhi siraha tu.
Sasa inaonesha hii vita imetengenezwa na watu wa East Africa wenyewe.
Unajua kupigana kwenye vita miaka yote hiyo inahitajika gharama kubwa sana? Alaf maskini mwingine anafadhuli😀
Kwahyo wapewe uhuru wajitangaze kua nchi au sio
 
Sasa inaonesha hii vita imetengenezwa na watu wa East Africa wenyewe.
Unajua kupigana kwenye vita miaka yote hiyo inahitajika gharama kubwa sana? Alaf maskini mwingine anafadhuli😀
Kwahyo wapewe uhuru wajitangaze kua nchi au sio
Kosa kubwa alilofanya DRC, ni kukingia kifua FDLR. Baada ya badhi wao kuhusika na mauaji, walipewa hifadhi, badae wakaanza kufadhiliwa. Eneo lenyewe limekaa kama vile halina mwenyewe, wakaanza kulitawala. Kilichofuata, ni kundi hili kuanza kuwanyanyasa watutsi wa Congo. Hapo ndipo mambo yalianza kuvurugika na kuleta utata. Af ujue, mali ya Congo ilishakuwa mali ya umma. Hivyo hata hao UN ni majizi tu. Bora viongozi waige mfumo wa Burkina Faso, vinginevyo, baada ya Congo, mi naona dalili za nchi nyingine kukumbwa na ghasia ya ukabila tena.
 
Major General Peter NKUBA CHIRIMWAMI, mkuu wa jeshi na mkuu wa mkoa wa Kivu Kasikazini, jana tarehe 23 Januari 2025, majira ya saa moja na dakika 44 usiku,alipokuwa amewatembelea wanajeshi wake kuwaunga mkono katika vita na kundi la waasi la M23, alimiminiwa risasi na kufariki hapo hapo.

Baada ya waasi hao kukalia mji mdogo wa SAKE, MONUSCO na SAMIDRC waliamua kuwafuata mjini humo kuwafukuza. Kama ilivyo vitani, hairuhusiwi kufyatulia risasi wanajeshi wa umoja wa mataifa.

Hivyo, baada ya kuwa na taarifa kwamba makundi hayo yatakuja, walijigawa(M23), na kuacha barabara nyeupe. Lakini waliitahadhalisha MONUSCO kwamba ikiachia risasi, na yenyewe itashughulikiwa.

SAMIRDC ambayo imeundwa na Afrika Kusini,Tanzania na Malawi, M23 ilisema yenyewe lazima wazichape. Basi katika uwepo wake kiongozi huyo, huku maeneo yaliyozingira barabara hiyo itokayo Goma kwenda SAKE, ndipo risasi zikaanza kulindima.

Baada ya kifo cha kiongozi huyo, maiti yake haikukamatwa, maana wenzake walimuchukua na kuondoka nae.

Pamoja na hayo, nchi za ugaibuni zimewaomba raia wake waishio mjini Goma kuhakikisha wanaondoka humo, na kwamba msaada wa haraka unaweza tolewa kwa waliopo Kinshasa tu. Siku ya jana,wengi wao walipaki mizigo wakielekea nchini Rwanda.
Mpaka sasa, mapigano yanaendelea.
dah mtu mkubwa hivyo anauawa vipi?
 
Kiini haswa cha huo mgogoro ni Interahamwe waliokimbilia DRC na kuanza kuua Wanyamlenge, na sasa wanajiita FLDR.

FLDR wanapigana bega kwa bega na Majeshi ya Serikali ya DRC.

Hata hayati Baba wa taifa aliwahi kuongelea huu mgogoro.

Tuache chuki dhidi ya jamii ya Kitutsi.
 
Back
Top Bottom