Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh Chalamila astuka , Atengua zuio la kufunga Bar kuzuia Corona

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426


Hapo Jana Mh Chalamila aliweka utaratibu wa wanywaji wa Mbeya , kwa kutoa muda wa hadi saa 3 usiku wawe wamepukutika kwenye mabar , kwa hoja kwamba baada ya muda huo wengi wanakuwa wamelewa kiasi cha kukiuka kinachoitwa Social Distancing ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona .

Lakini katika hali ya kushangaza leo hii amefuta amri hiyo , na kwamba wanywaji waendelee kupiga kilaji mpaka watakapotosheka , ili mradi wachukue tahadhari .

#Tuendelee kunawa mikono kwa maji Tiririka ili kuzuia maambukizi ya virusi vya corona
Your browser is not able to display this video.
 
Hili ndiyo tatizo la kuacha kumuomba Mungu,unabaki kumsifia mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunataka mapato "Naomba mukakorekiti revenyu. Nataka kodi" Kwa sauti ya mwenye hashtag yake kule 254
Hashtag ya mukaidi. Ila wakenya buana, sjui ni kiswahili kulod kwa muda mrefu ama waliamua tu kumchafua
 
Kifupi na kitaalamu yanaitwa Maagizo toka JUU.
 
Watakapopatikana wagonjwa kwenye bar ndio akili itawarudi na Bar zitajifunga zenyewe bila kujua
Kwa sasa endeleeni kukusanya kodi
Siombei hilo ila ndio ukweli


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…