Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

dito.jpg


Mkuu wa Mkoa wa zamani, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri (58),akiingia mahakamani jana.


Dito amlalamikia Kikwete

Na Tausi Ally

Mkuu wa Mkoa wa zamani, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri (58), amelalamikia ziara za viongozi wa serikali kwenda kutoa rambirambi kwenye familia ya dereva wa daladala, marehemu Hassan Mbonde, anayedaiwa kuuawa naye kuwa ni sawa na kumuhukumu kabla ya mahakama kutoa hukumu yake.

Ingawa hakufika mwenyewe kuhani msiba huo, Rais Jakaya Kikwete alimtuma Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, ambaye pamoja na kutoa salamu maalum za rais kwa wafiwa, pia alitoa ubani wa Sh500,000 kwa familia ya marehemu.

Kupitia kwa wakili Nimrod Mkono, aliyejiunga na jopo la mawakili wanaomtetea, Ditopile aliiomba mahakama iwapige marufuku viongozi hao wa serikali kwenda kutoa rambirambi kiserikali kwenye familia hiyo.

Pia aliitaka mahakama kuvizuia vyombo vya habari kuandika na kutangaza habari za mteja wao nje ya mahakama kwa madai kuwa hali hiyo inaleta hisia mbaya katika jamii na inamtia wasiwasi kuwa hatatendewa haki.

Nimrod alitoa ombi hilo jana mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Michael Luguru, akidai kuwa mambo hayo yanajenga picha kuwa mteja wake tayari ana hatia kabla ya mahakama kumaliza kazi yake.Aliieleza mahakama kuwa endapo viongozi wa serikali wanataka kwenda kutoa rambirambi kwa familia ya marehemu, basi waende kwa siri na siyo hadharani kama wanavyofanya sasa.

Alihoji kuwa inakuwaje Makamu wa Rais anakwenda kutoa rambi rambi kwa wafiwa kwa niaba ya Rais pamoja na viongozi wengine kwa niaba ya serikali wakiwa na magari ya vimulimuli na hawafanyi hivyo kwa kwenda kumtembelea mteja wake kwa staili hiyo hiyo ya magari ya vimulimuli.Alidai kuwa wapo watu wengi waliouawa kwa kupigwa risasi lakini hakuna viongozi wa serikali wanaokwenda kutoa pole kwa familia zao kwa kutumia magari na vimulimuli vya serikali.

Hata hivyo, baada ya wakili huyo wa Ditopile kutoa malalamiko yake, Mwendesha Mashtaka, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Charles Kenyela, alisimama na kuieleza mahakama kuwa Katiba ya Tanzania inatambua kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria na kwamba mahakama haifanyi kazi zake kwa kusikiliza mambo yanayofanyika mitaani au ya kisiasa, hivyo matukio hayo hayawezi kuingilia au kuishawishi iegemee upande mmoja.

Aliendelea kueleza kuwa mahakama haiwezi kuzuia viongozi wa serikali kwenda kusalimia ndugu au jamaa zao kwa kuwa nao ni binadamu wenye ndugu na marafiki na hakuna sheria inayozuia kujuliana hali na kwamba vyombo vya habari navyo vina uhuru wa kuripoti kila kinachotokea.Kwa upande wake, Hakimu Luguru alisema mahakama hiyo haina uwezo wa kutoa amri hiyo kama ilivyoombwa kwa kuwa kesi ya mauaji inasikilizwa na Mahakama Kuu.

Alisema kama anaona vyombo vya habari vinaripoti kinyume na matukio yanayojiri, basi awe huru kuchukua hatua za kisheria.Tangu tukio hilo viongozi mbalimbali wamekuwa wakienda nyumbani kwa marehemu kuhani msiba huo, akiwemo, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo aliyekwenda kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete na kutoa ubani wa Sh500,000.

Luhanjo pia alitoa ahadi kuwa Rais Kikwete akitoka safarini angekwenda mwenyewe kuhani msiba huo.Viongozi wengine waliokwenda kuhani msiba huo, ni Makamu wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein ambaye pia aliahidi kuwatuma wasaidizi wake kupeleka ubani.

Wengine ni Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Londa, ambaye alitoa viroba 10 vya mchele na mafuta ya kula kwa kwa ajili ya kufanikisha kisomo cha hitma ya kumuombea marehemu iliyoandaliwa na kiongozi huyo Jumamosi iliyopita.Vile vile Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro, Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa, Meya wa Manispaa ya Ilala, Abuu Jumaa nao wamekwishafika kuhani msiba huo.

Kiongozi aliyefika kwenye msiba huo wakati wa mazishi na kutoa ubani wake wa Sh100,000 alikuwa ni Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema.Mahakamani jana, watu wengi zaidi walijitokeza katika kushuhudia jinsi kesi hiyo inavyoendeshwa kuliko waliojitokeza wakati Ditopile alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Novemba 6.

Ditopile anadaiwa kuwa Novemba 4, majira ya saa 1:00 usiku katika eneo la njia panda ya Bagamoyo na Kawe wilayani Kinondoni, jijini Dar es Salaam, alimuua Hassan Mbonde.Mshtakiwa huyo anatetewa na mawakili maarufu watano wa jijini Dar es Salaam, ambao pamoja na Mkono ni Dk Ringo Tenga, Losan Mbwambo, Cuthbert Tenga na Samwel Mapande.
 
Written by Irene Mark
Tuesday, 21 November 2006

MWANASHERIA maarufu wa kimataifa, Nimrod Mkono, amechukua jukumu la kuwa kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile - Mzuzuri, anayekabiliwa na mashitaka ya mauaji.

Mkono, ambaye ni Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), sasa anaungana na mawakili wengine wanne. Mawakili hao ni Dk. Ringo Tenga, Cuthbert Tenga, Rosan Mbwambo, na Samuel Mapande.

Get it there:

http://jambotanzania.net/v2/content/view/894/2/
 
Wanataka kupindisha ushaidi..
Ili ionekane kulikuwa na mawakili maarufu...
Mimi wala sielewi..

Ila jamaa ataachiwa huru au itageuka manslaughter.. Kama hauamini watch out!!
 
I noticed this before... Kuna ?!? Ama kweli lisemwalo lipo...! Watu hapa walisema issue hii itapindishwa tu. Angalia Nimrod nae kishaona deal heavy hili.

Au ndo kumlia fedha? Sipati picha
 
Sasa hawa watagawanaje hizo fees? Au DITO anatoa dau kubwa sana?
 
Maswali mengi najiuliza sipati jibu! Inshallah yangu mie macho na nataka kuona nini watanzania watafanya. Cha kuleta matumaini ni kesi kuendeshwa mapema kabla watu hatujaletewa dhahma nyingine. Lakini hiki kisiwe kigezo cha watanzania kusahau machungu ya RDC (Richmond). Tumetangaziwa mgawo wa umeme hadi saa 4 usiku!
 
Naiona Dream team ya kibongo na kama tulivyosema....maskini Mbonde ndio imetoka hiyooo!...
 
There's no way Dito can afford Mkono,the guy charges in excess of 400 dollars an hr! Mawazo yangu mimi ni kuwa lazima kuna 'mfadhili' au 'wafadhili' kwenye hili.Maana kwanza kumuona Mkono mahakamani kwenye kesi ya mauaji(achilia mbali ya Kisutu) ni sawa na kuona kifaru Mikumi!
 
Ofcourse at the moment Dito can't afford Mkono but the friends have seen that if Dito has gone with water there is no way for him to protect them.

They will do everything possible to set him free. Just ask yourself how come the gun went missing? That is a crucial evidence in Law, these guys are just buying time and they know down the line 10years no one will care anymore.
 
Wasituletee ujinga OJ Simpson hapa, hata kama the gun went missing TUTAFUKUA MAITI, ku-prove kuwa aina ya bunduki na risasi iliyoua, ilikuwa ya Dito na ilikuwa triggered na Dito (the impact ya risasi) + mashahidi. hata angeshuka MALAIKA LEO HII leave alone Mkono, hatishiki mtu hapa, walalahoi tutapambana/tutapiga kelele mpaka mwisho wa dunia.

Tena nimeshaanza kuona dalili za hii topic kufungiwa, tuweke back-up za hii mada.
 
Hivi Mkono amewahi kusimamia kesi gani maarufu ya kukumbukwa. Najua kuwa ni tajiri sana kutokana na kuwa corprate lawyer wa makumpuni mengi tena makubwa makubwa lakini sijawahi kumsikia katika criminal case kubwa yoyote ile.
 
ndio sheria

na kwa jinsi mapolisi wetu walivyo wajinga basi sitoshangaa Mkono kushinda hii kesi

si unajua jinsi gani polisi wanavyogopa wanasheria?
 
WALIACHIWA KWA PRESSURE KUTOKA UK

MKONO HAJAFANYA KESI YOYOTE YA KUWEZA KUWA TESTED KISHERIA. HIVI SASA WANATAKA KUTISHA KWANZA MAANA ILE KESI YA WAINGEREZA PROSECUTOR NDIO ALIIFUTA. ( KESI NYINGI ILIZOFANYA UKICHUNGUZA ZITAKUWA HIVYO HIVYO) MAANA MAGAZETI WAKIANZA KUKUSIFIASIFIA NDIO UNAKUWA LIMBUKENI. KAMA MKONO WA SERIKALI UTAACHIA MAHAKAMA IFANYE KAZI YAKE BASI HAKUNA CHA MKONO WALA NANI?

____________________________
DUA LA KUKU HALIMPATI MWEWE
 
question... inakuwaje a sitting MP anakuwa Wakili mahakamani!!!? hivi wajuzi wa nchi nyingine hayo yanawezekana, kwa mfano Waziri Mkuu mwanasheria anaweza kufanya kazi ya Uwakili akiwa bado Waziri Mkuu? Vipi Waziri mwingine ambaye ni mwanasheria anaweza kufanya kazi ya uwakili akiwa bado Waziri? na vipi Mbunge (Mtunga sheria) anawezaje kufanya kazi ya uwakili wakati yeye ni Mbunge?
 
Mzee Mwanakijiji,
Hili swali zito sana! na sidhani kama lina jibu maanake ipo siku jaji atakuja simama kama wakili na Speka wa Bunge kusimama kama mbunge!!.....
 
MKJJ

Swali zuri lakini turudi kule ambako wengi humu ndani twapenda kufuata referece ni KATIBA ...halafu kuna suala zima la balance of power ambako kwetu hilo ni HARAM lakini having said that najua kuwa BLAIR ni lawyer halikadhalika CLINTON naye alikuwa ni lawyer sasa itabidid tuangalie hilo
 
Heshima mbele wazee, nilikuwa nilikuwa pembeni kidogo, lakini juzi nilikuwepo mahakamani kujionea mwenyewe,

kuingia kwa mbunge Mkono kwenye hii kesi, kuna maana moja tu, kwamba kuna "mkono mzito" nyuma unaojaribu kumsaidia Blaza Dito, kwa sababu huyu jamaa hana shida ya hela, kwa hiyo anafanya bure, WHY?

Anyway, ninapenda kuwahakikishia wanachi wapenda haki, kuwa hii kesi haina fix, wala takrima, hii kesi ni Home Run, hata aje wakili Shapiro toka US, hawezi saidia kitu, tena kuingia kwa Mkono ndio sasa kumewaamsha majaji kuwa kuna kamchezo kanataka kuchezwa, na wao sasa wameanza kujipanga, nasikia wameapa kuwa kwenye hii kesi ndipo hao wanaotaka kucheza mchezo watajifunza adabu, Mkono anazo hela lakini hawezi kuibadili sheria kwenye hili, halafu yeye sio mtandao,

tunaendelea kuifuatilia kwa makni hii kesi!
 
Back
Top Bottom