Mkuu wa Ujasusi wa Rwanda, Lt. Gen Kayumba Nyanwasa, asema Kagame ni chanzo cha matatizo yote Congo na maziwa makuu

Annunaki

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2021
Posts
2,042
Reaction score
3,674
Aliyewahi kuwa mkuu wa ujasusi Rwanda na Balozi wa Rwanda nchini India, Lt. Gen Kayumba Nyamwasa anasema matatizo yote yanayotokea mashariki ya Congo yanasababishwa na kagame.

Anasema Congo hamna tena tatizo la Banyamulenge ,lilishakwisha zamani na wana haki sawa na wanahudumu hata sasa katika serikali ya Congo.
Anasema kagame amekuwa DRC zaidi ya miaka 30 akiwaua wahutu wa FDRL baada ya Genocide mpaka leo, na kwamba hana kisingizio tena kuhusu FDRL nchini DRC.

Anasema M23 wameibuliwa upya na Rwanda 2021 baada ya Tshikedi kuingia makubaliano na Burundi na Uganda, ndipo Kagame alichukia na kusema kama hajakaribishwa atajikaribisha mwenyewe.

Amekiri Rwanda inaiba madini Congo na kupeleka Rwanda kwa ajili ya kuyauza nje na anasema kila eneo wanaloshika M23 lenye madini, madini huanza kusafirishwa kwenda Rwanda.

Anakiri RDF inatoa sapoti ya 100% kwa M23.

Anasema Rwanda ikiikamata Kivu yote, ataivamia Burundi na huo ndio mpango.

Anakiri ndani ya Rwanda wahutu wamefungwa minyororo na kufuri hawana pa kuongelea na hawana mtetezi.

Anakiri Rwanda ina wakimbizi wengi wahutu na watusi ambao hawakubalina na sera na utawala wa kagame, na kwamba kagame asipowasikiliza kuna hatarii ya kutokea Genocide nyingine Rwanda.

Kumbuka huyu Mtusi kama ilivyo kwa kagame.

Hapa chini nimeweka interview yake yote ya leo wakati akihojiwa akiwa uhamishoni nchini Afrika Kusini.


View: https://x.com/Sentletse/status/1885998079419003033?t=XrJ7G6I2xDOUSU6Sr__OXg&s=19
 
Tafadhari kabla ya kucoment sikiliza interview yake yote kwanza.
 
Porojo zake tu kwa vile alishindwa kumpindua Kagame.
 
Amekiri Rwanda inaiba madini Congo na kupeleka Rwanda kwa ajili ya kuyauza nje na anasema kila eneo wanaloshika M23 lenye madini, madini uanza kusafirishwa haraka kwenda Rwanda.
 
Anakiri Rwanda ina wakimbizi wengi wahutu na watusi ambao hawakubalina na sera na utawala wa kagame, na kwamba kagame asipowasikiliza kuna hatarii ya kutokea Genocide nyingine Rwanda.😭😭😭
 
Na mi nimekiongea Humu, Banyamulenge Wapo Against M23, so kisingizio cha kwamba wao wanasaidia raia wa Congo Mashariki hakina tena mantiki, M23 ni Rwanda 100% hawana legitimacy yoyote ya wao kuwepo Congo.
 
Ana ulinzi wa uhakika?
Au ndiyo baada muda tutasikia R.I.P?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…