Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

Duh Magufuri angefanya kama Museveni Jf hapa pangechimbika kwa post
 
Tatizo reliability ya information zinazozunguka kwenye mitandao yetu ya kijamii iko chini sana. The veracity of your conclusion about anything depends on the veracity of the basis for your conclusion! Garbage in garbage out. It's that simple!
 
Kwani ukuu wa wilaya unahitaji mapambano? acha ushabiki
 
Mkuu inabidi urudi darasani hujui nini maana ya conflict of interest. Mkuu wa wilaya ni mwakilishi wa rais wilayani. Unapozungumzia conflict of interest always Ina involves two parties. Sasa hiyo conflict of interest ni Kati ya Nani na nani
 
hata akiwa wa kumzaa amchague tu mbona inchi za wenzetu yanafanyika kwa nn isiwe TANZANIA ?
 
Hivi ukiwa Raisi halafu ukawa na watoto wa kuwazaa kumi, halafu watoto wamesoma kwelikweli na ni wazalendo haswa, na wachapa kazi makini, Je ukiwateua Zile nafasi Kumi za Ubunge kisha Ukawapa Uwaziri Litakuwa ni Tatizo?

Je Ukifanya hivi, Makatibu wa Kuu wa wizara wanazoziongoza wataweza kweli kuwakatalia "Watoto wa Raisi" iwapo wataanza kufanya madudu?
 
Ccm ni ile ile hata aje nani kwa mfumo wa ccm ulivyo nikazi bure
Si kweli!
Maraisi wa 5 wa Tanzania kutoka ccm wako tofauti sana!
Uwezo na utashi wa raisi unashinda ilani za vyama na hata agenda kuu ya ccm!
Magufuli na serikali yake hawafanani kabisa na kikwete na serikali yake!
Kama unataka kuwajaji viongozi wa nchi, just deal nao personally, hakuna mfumo unaowasimamia, Ila upo wanaoutengeneza!
 
Mkuu inabidi urudi darasani hujui nini maana ya conflict of interest. Mkuu wa wilaya ni mwakilishi wa rais wilayani. Unapozungumzia conflict of interest always Ina involves two parties. Sasa hiyo conflict of interest ni Kati ya Nani na nani

Sio lazima iwe btn two individuals!

Inaweza ikatokea pale pia mtu anapoweza kuangalia personal benefit kwa decision anazofanya sababu ya nafasi yake ya kimamlaka!

Kwa standard ya JPM kama huyo kweli ni binti yake atakuwa anakosea big time! Itafanya watu warudi na kuchambua teuzi zake zote!

Ni hivi kama Mimi nikiwa kiongozi mwenye mamlaka sehemu, naweza kulipa fadhila kwa kutoa nafasi za uongozi, naweza kusaidia watu wakiwemo watu wa karibu kama wanafamilia, rafiki etc! Inakuwa conflict of interest kwa kuwa sitoi equal chances kwa wengine na decisions zako zitakuwa biased when it comes to kuchagua candidates wenye sifa sawa au hata aliyemzidi kidogo huyo wa kwako!

Ila sio big deal kwa kuwa hapana kiongozi ktk taifa hili ambaye hajawahi kupokea mtoto wa rafiki yake, workmate, mchungaji/padri/sheikh wake, jirani etc! Suala hili ni tatizo la kimaadili linalomtatiza kila mwaafrika, nadhani si shida ya taifa letu pekee!
 
Kweli kabisa zaidi ukizingatia viongozi wa Afrika. Museven si alimchagua mkewake pia. Sishangai sana viongozi wa Afrika kuteua watu wao wa karibu. "Sadaka huanzia nyumbani"
 
Isitoshe sio baba yake wa kumzaa shida iko wapi hapo?. Tatizo tunalolikataa wananchi ni kubeba mtu asiyebebeka...huyo dada anayo elimu nzuri tu...
Declear interest man
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…