Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

hebu taja sifa za kuwa mkuu wa wilaya tuzijue

Acha kukurupuka - you need to pay attention, Mr JF - Expert Member. Kwenye post yangu huoni kama nime-highlight mambo matatu? Kama huwezi kusoma mistari miwili utaweza kusoma mikataba ya ulaghai kweli au nyie ndiyo mnaotutia hasara nchi hii?
 
Ni kawaida kwa mtawala, kama wewe ni mfugaji kachunge. Kama mseven kajaza ndugu zake, mpaka mke wake. Unashangaa,!.
 
Kwahio kama amemlea na anazo sifa za kuteuliwa basi aachwe?

Ufipa nani kawalogaaaa...
Mtoto wa mjomba wa Rais, shemeji wa Rais, mdogo wa Rais, mtoto wa Rais, mke wa Rais, n.k' kuteuliwa na Rais kwenye nafasi za uongozi wa kisiasa upo Afrika tu, ndiyo demokrasia ambayo tumeamua kuifuata. Demokrasia hii ya pekee ya Afrika, inayoshabikiwa na Afrika ndiyo inayolifanya bara la Afrika liwe la pekee lenye maendeleo ya pekee Duniani. Ujijnga mkubwa haupo kwa viongozi wanaoyafanya hayo bali kwa wananchi wa Afrika. Umaskini wetu mkubwa wa kichwani ndiyo chanzo kikuu cha haya yote. Mungu ibariki Afrika ambayo uliipa kila kitu lakini ukaruhusu umaskini wa vichwa vya waafrika.
 
Msambichaka mie natamani kulia.
Kweli matatizo tunayo sisi wenyewe
 
Mara baada ya uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliofanyika na kutangzwa leo, jamii imeanza kuwachambua na kujuwa historia zao na ushiriki wao katika kumasaidia kazi Mh Rais.

Wananchi wamekuwa na shauku ya kumfahamu na kuelewa historia ya Mkuu wao mpya wa Wilaya Mh. Happy es Senenda William. Kabla ya kuwa DC wa Kisarawe tunaambiwa dada huyu alikuwa Manager wa HR wa TANROADS Mkoa wa Tanga, ni mdada mdogo mwenye elimu ya Masters. Mwaka 2010 aligombea ubunge viti maalumu kupitia mkoa wa Geita lakini hakufanikiwa, mwaka 2015 alipumzika ili kuzunguka na baba kumtafutia kura

Habari zinazidi kupenyeza kuwa Mh.Happyness William ni mtoto wa kulelewa na Rais JPM, amesomeshwa na Rais na amekuwa akiishi na JPM kwa maisha yake mpaka alipopata kazi. Kifupi Mh.Happyness ni "mtoto" wa JPM na kwa sasa ni DC wa Kisarawe

Ama hakika huu ni msimu wa vijana...Vijana mjiibidishe ili muonekane na mpate Wilaya au Mkoa.

Safi sana, cha msingi afanye kazi kwa bidii na bidii inaweza kumpereka juu zaidi.
 
Usigeuze JF kuwa chungu cha majungu! Ongelea uwezo wake, sio uhusiano wake...ungejisikiaje kama ungekuwa wewe unaomba kazi sehemu afu unanyimwa simply because wewe una undugu na rais...tuletee CV na track record ya performance sio mijungu
Tusishabikie tusichokijua. Hapa suala siyo uwezo wa mteuliwa bali ni kukiuka misingi ya uadilifu. Hii siyo kazi ya uwalimu, udaktari au uhasibu, ni nafasi ya uongozi wa kisiasa. Hapa kuna mgongano wa kimaslahi. Meneji wa kampuni ya umma akimpa tenda kwenye kampuni anayoiongoza mwanae, anakuwa ametenda kosa. Siyo kwa sababu mwanae hana uwezo wa kutekeleza tenda bali tunakuwa hatuna uhakika kama tenda amepewa kwa sababu ya uwezo (ambao anao) au kwa sababu ya mahusiano ya kifamilia.

Wenye uwezo na masters siyo huyo tu. Kwa nini hao wote hawakupewa? Kwa hiyo hizi teuzi haziangalii uwezo na elimu pekee yake bali ni pamoja na vigezo vingine, huenda vya upendeleo vikawa ni miongoni.

Kama ni kweli yaliyoandikwa, nijuavyo mimi ni kwamba, kiongozi mwadilifu kabisa kabisa, kamwe asingeweza kufanya hivyo. Ndiyo maana Viongozi waliowahi kuwa na uadilifu wa hali ya juu kama Mwalimu hawakuawahi, hata mara moja kuwapa uongozi wanafamilia kwenye nafasi za uteuzi zinazofanywa na Rais, hakuwahi kufanya hata siku moja. Na haya mataifa yenye demokrasia, huwezi kuona kitu kama hicho hata siku moja. Haya yanatokea Afrika, na bahati mbaya sana watu wanatetea vitu vinavyokiuka misingi ya utawala bora.
 
Mara baada ya uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliofanyika na kutangzwa leo, jamii imeanza kuwachambua na kujuwa historia zao na ushiriki wao katika kumasaidia kazi Mh Rais.

Wananchi wamekuwa na shauku ya kumfahamu na kuelewa historia ya Mkuu wao mpya wa Wilaya Mh. Happy es Senenda William. Kabla ya kuwa DC wa Kisarawe tunaambiwa dada huyu alikuwa Manager wa HR wa TANROADS Mkoa wa Tanga, ni mdada mdogo mwenye elimu ya Masters. Mwaka 2010 aligombea ubunge viti maalumu kupitia mkoa wa Geita lakini hakufanikiwa, mwaka 2015 alipumzika ili kuzunguka na baba kumtafutia kura

Habari zinazidi kupenyeza kuwa Mh.Happyness William ni mtoto wa kulelewa na Rais JPM, amesomeshwa na Rais na amekuwa akiishi na JPM kwa maisha yake mpaka alipopata kazi. Kifupi Mh.Happyness ni "mtoto" wa JPM na kwa sasa ni DC wa Kisarawe

Ama hakika huu ni msimu wa vijana...Vijana mjiibidishe ili muonekane na mpate Wilaya au Mkoa.

Aisee hata majungu naona huyajui. Hivi mtu kama anao uwezo na ni ndugu wa kiongozi ina maana hasipiwe nafasi? Tafakari kwanza unapoamua kuleta hoja. Umeandika mwenyewe sifa zake na anaonesha ni mpiganaji na anafaa kushika nafasi hiyo. Sometimes tuache majungu tusonge Mbele. Hakuna tatizo lolote kwa huyo mkuu wa wilaya kupewa nafasi.

Ushauri, tafuta sifa, fanya kazi kwa bidii utafanikiwa na kushika nafasi za juu. Nchi ya Tanzania bado inaangalia merits Zaidi, waweza kuibuka toka kokote ukifanya bidii. Mfano ni wa huyo unayemlalamikia kuchagua, angalia History yake na sasa ni nani. Chapa kazi tafuta elimu, maarifa kwa bidii
 
Tusishabikie tusichokijua. Hapa suala siyo uwezo wa mteuliwa bali ni kukiuka misingi ya uadilifu. Hii siyo kazi ya uwalimu, udaktari au uhasibu, ni nafasi ya uongozi wa kisiasa. Hapa kuna mgongano wa kimaslahi. Meneji wa kampuni ya umma akimpa tenda kwenye kampuni anayoiongoza mwanae, anakuwa ametenda kosa. Siyo kwa sababu mwanae hana uwezo wa kutekeleza tenda bali tunakuwa hatuna uhakika kama tenda amepewa kwa sababu ya uwezo (ambao anao) au kwa sababu ya mahusiano ya kifamilia.

Wenye uwezo na masters siyo huyo tu. Kwa nini hao wote hawakupewa? Kwa hiyo hizi teuzi haziangalii uwezo na elimu pekee yake bali ni pamoja na vigezo vingine, huenda vya upendeleo vikawa ni miongoni.

Kama ni kweli yaliyoandikwa, nijuavyo mimi ni kwamba, kiongozi mwadilifu kabisa kabisa, kamwe asingeweza kufanya hivyo. Ndiyo maana Viongozi waliowahi kuwa na uadilifu wa hali ya juu kama Mwalimu hawakuawahi, hata mara moja kuwapa uongozi wanafamilia kwenye nafasi za uteuzi zinazofanywa na Rais, hakuwahi kufanya hata siku moja. Na haya mataifa yenye demokrasia, huwezi kuona kitu kama hicho hata siku moja. Haya yanatokea Afrika, na bahati mbaya sana watu wanatetea vitu vinavyokiuka misingi ya utawala bora.

Tuanze na wewe, utupe CV yako na sifa za kufaa kuachwa
 
Kama sifa anazo haijalishi hata angekuwa mtt wa kuzaliwa na mh.
 
Hapa kila MTU mahali ulipo wewe vuta ndugu yako weka ukiulizwa sema tatizo ni mfumo!
 
Kwa nchi zetu hizi za Kiafrika nikiwa rais mtoto mmoja nampa wizara ya ulinzi, mwingine ukuu wa majeshi, mwingine ukuu wa kunilinda, maisha yenyewe yapo wapi?
 
Akiwa mtoto wa JPM kama ana sifa ndiyo asiteuliwe. Mmeambiwa "Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali".
Sifa zilizotajwa hapa ni kuwa na masters,jee hiyo ni sifa ya kuwa mkuu wa wilaya? Pia sifa nyingine ni kugombea ubunge viti maakumu, jee hiyo nayo ni sifa ya kufaa kuwa mkuu wa wilaya? Au hiyo ya kuwa HR Tanroad, tujiukize aneingia Tanroad mwaka gani na kaingiaje maana tunajua Tanroad iko chini ya wizara gani na wizara hiyo ilikuwa chini ya nani.
Kuna makosa makubwa yanafanyika kwa kufanya U DC kama kazi ya kutokea wakati kazi hiyo ni muhimu sana hasa kwa maeneo ya vijijini na inahitaji mtu mwenye busara nyingi kwani ina madaraka makubwa hata ya kunweka mtu korokoroni.
Binafsi sipingi kupewa uDC huyo kijana lakini kama anamahusiano na mteuzi basi lazima awe na sifa na uzoefu wa ziada usio na shaka vinginevyo hiyo ni dosari kubwa kwa mteuzi.
Wachangiaji wengi wanaonyesha kubisha kwa ushabiki tuu na kutoa mifano ya Museveni na Marais watangulizi, hayo ni makosa kosa kulilinganisha na kosa
 
Back
Top Bottom