Mkuyu ni Mti gani?

Gordian Anduru

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2021
Posts
369
Reaction score
747
Hapa ni makumbusho ya Taifa, kuna mti mkubwa sana mimi naufahamu kama BODHI TREE, ni mti ambao BUDDHA alipatia UFUNUO akajitambua, hata hivyo wafanyakazi pale makumbusho wameandika kwamba ule mti unaitwa MKUYU.

Mkuyu ni mti aliokwea ZAKAYO ili amuone YESU. Binafsi sifahamu mkuyu ukoje ila ninacho fahamu ni kwamba mti aliokaa BUDDHA na mti aliokwea ZAKAYO ni miti miwili tofauti.

Kisayansi mti aliopanda zakayo unaitwa Ficus sycamorus na ule wa BUDDHA unaitwa ficus religiosa mti aliokwea zakayo


 
Mkuyu una ua la ndani kwa ndani ndani ya tunda ..ambalo huota kama kipele...wasps jike ni mdudu pekee ambaye hutobowa hilo tundaupele na kuweka mayai yake humondani ...mayai hujiangua na watoto huweza kuchavusha tunda hilo lenye maua ndani kwa ndani....

Cc botanists na waikolojia
 
Tafuta kitu kinaitwa Baniani kwa Hindu kwenye engo ya Botany Indian
 
Mkuu hizo mvi kwenye kidevu na kichwani, ni zile za kupaka rangi, au ni za ukweli kama hizi za kwangu?

Halafu mbona unaonekana kama Mkuda fulani vile!! Au ni macho yangu?
 
Na wewe umekuwa sehemu ya mkuyu?
 
Tatizo unatafuta dawa ya miti shamba kijanja janja............huo wa juu ndo unaonekana kama mkuyu ingawaje nitahitaji kusogea karibu kuulinganisha na mikuyu ninayojua, huu uliopiga nao picha hapa siyo mkuyu hata kwa kuufananisha.....
 
We ni mtaalum wa mimea..?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…