Mkwara wa Rais Magufuli, Maalim Seif anyimwa posho ya matibabu!

Mkwara wa Rais Magufuli, Maalim Seif anyimwa posho ya matibabu!

Kwa vile tumekubali watawala wavunje sheria hata kunyima stahiki za viongozi waliopita,basi ujue kama Taifa tunakazi kubwa ya kuvuka daraja.Na kitu kimoja kikubwa kinaitwa sheria ya dhahabu inasema'USICHOPENDA KUTENDEWA USIMTENDEE MWENZAKO" maana kuna siku utakuja tendwa usijue sababu.Na ukumbuke kila siku MKUKI MTAMU KWA NGURUWE NA KWA BINADAMU MCHUNGU.Leo furahia anachotendewa Maalim Seif kesho yako huwezi ijua.

Nakumbuka Rais Chiluba alipoingia madarakani alimtendea mambo kama haya Mzee Kaunda lakini naye alipo achia madaraka yakamkuta makubwa zaidi na ndio yalichangia hata kuondoka duniani mapema. Tujifunze kuacha sheria iongoze mambo yetu na hakuna atakayemlaumu mtu na sio kiburi na hisia kutuongoza.
 
Hata ningekuwa mimi nisinge sain kitu chochote cha mtu aliyekataa mkono wangu kumsalimia na hata mkono wa shen ni halali kukataa kusain kama yeye alivyoukataa.
 
Mbeya tunajiendesha serikali haijawahi kuweka mipango mikubwa yeyote ya maendeleo lakini tupo na tunaishi na maisha wetu wachapa kazi namba one nchi hii tunalisha nchi


ni kweli mkuu, Mbeya tupo kama yatima kwa serikali hii, zaidi ya uwanja wa Songwe hawana lingine la kujivunia Mbeya, miradi yote wanaikimbizia Mwanza.....bora tuendelee kula viazi na wali mkavu lakini kuwakomesha kwa kuwapa wapinzani jiji
 
Je ni kweli Dk Shein kamnyima Maalim hiyo posho ya matibabu....???Kama ni kweli basi Dr. SHEIN kampa Maalim kick kubwa saana na huenda ikaathiri saana hali ya ZNZ.Ningependa saana maeleano,na wafikirie vizazi vijavyo.Kwa umri wa Maalim na Dr Shein,kunyemelewa na maradhi ya utu uzima ni rahisi .Kamwe hakutakuwa na maendeleo ZNZ kama hawatafikiria vizazi vijavyo.
 
ya nzanzibar ingekuwa busara sana wazanzibar wenyewe kwanza wakae na atafutwe mtu mwingine ambaye sio zao la haya yaliyopo walau aje ambaye hana upande aje asaidie sio ubabe ubabe hautakuwa msaada kamwe
 
Back
Top Bottom