Wanaomlaumu Mkwassa ukiangalia asilimia kubwa ni wale mashabiki jina, hajawahi hata kusuka mpira wa chandimu, hajui hata kupiga danadana, ni washabiki fuata upepo, huwezi kuifananisha stars iliyopo nafasi ya 135 kidunia na algeria iliyopo nafasi ya 40, nafasi ya 40 kwa nafasi ya 2 afrika ni kichekesho, algeria wanawachezaji zaidi ya 200 wanaocheza soka ulaya, wakati tz tuna samatta na ulimwengu tena hapo kongo:what: ukiangalia sana tatizo sio makocha ni wachezaji na simba na yanga, wachezaji kiu yao kubwa ni kucheza simba au yanga baasi, simba na yanga nazo hazipo tayari kuwaachia wachezaji wakafanye majaribio nje ya nchi na zinafanya usajili wakuleta wachezaji kutoka nje na wanapangwa kikosi cha kwanza, pia, timu itafutiwe mechi za majaribio, kwenye nchi ambazo viwango vinatuzidi mara tatu au nne, Mkwassa wewe ni bonge la kocha, wala usijiuzulu piga kazi.