Mlango umefungwa hakujawahi kuwepo na safari ya mwezini

Mlango umefungwa hakujawahi kuwepo na safari ya mwezini

Umeshindwa kuweka rejea ya ulichosema ulitaka kutupuga changa la macho ,humu ni Great thinkers ukija njoo kamili kamili
yan we unanitishia 😂 ety greatthinker wanao jua hawaulizi,wamo humu na wajua vitu vingi viko humu forum kuvipata nnje ni ngumu au haiwezekan
 
Unamaanisha nini unaposema kutoka nje ya mfumo wa jua? Kama kiliwesa kupiga picha ya jupiter je ? Jupiter ipo mfumo wa jua lipi?
Mfumo wa jua yaani "Solar system" yaani mjumuiko wa sayari,vumbi la kicosmotiki,magimba,vimondo,mawingu ya kikosmotiki na vinginevyo vyote vinavyolizunguka nyota ya jua.Jupita ni moja ya sayari katika mfumo wa jua pamoja na sayari zingine 8 ikiwemo dunia.Kumbuka nje ya nyota yetu (jua) kuna mabilioni ya nyota nyinginezo pamoja na mifumo yake.
 
Umeokotwa na hao wazungu ukaokoteka na wewe unataka kuokota wengine, hata picha ya wanasayansi kwenda mwezini ni ya kufoji waliweka bendera ya marekani inaonekana inapepea na huko hakuna upepo wa kuipepea bendera. Ndiyo sembuse kufika huko Jupiter
Akili ndogo
 
Haya twambie hali iliyopo mwezini, uchomeke bendera itapepea vipi?
Achana na habari za bendera, Swala ni kwamba kufika mwezini inawezekana au haiwezekani? Kwa hiyo unakataa kwamba haiwezekani kupiga picha Jupita na kwamba chunguzi za anga za mbali ni uongo na haiwezekani?
 
Mfumo wa jua yaani "Solar system" yaani mjumuiko wa sayari,vumbi la kicosmotiki,magimba,vimondo,mawingu ya kikosmotiki na vinginevyo vyote vinavyolizunguka nyota ya jua.Jupita ni moja ya sayari katika mfumo wa jua pamoja na sayari zingine 8 ikiwemo dunia.Kumbuka nje ya nyota yetu (jua) kuna mabilioni ya nyota nyinginezo pamoja na mifumo yake.
Umeelewa lakini swali langu?
 
Achana na habari za bendera, Swala ni kwamba kufika mwezini inawezekana au haiwezekani? Kwa hiyo unakataa kwamba haiwezekani kupiga picha Jupita na kwamba chunguzi za anga za mbali ni uongo na haiwezekani?
Kingine huyo Armstrong alipofanya interview na wanasayansi mbalimbali kuhusiana na safari hiyo, aliulizwa mengi ya msingi kuhusiana na safari yake na alishindwa kuyajibu akaoneoana kubabaika. Na hapo ndiyo ikabainika safari yake ilikuwa ya kupika haikuwa halisi na hata picha hizo zilitengenezwa huko Marekani
 
Mwaka 1969 Neil Armstrong binadamu wa kwanza kuweka mguu wake wa kushoto katika ardhi ya mwezi.Voyager 2 chombo kilochosafiri umbali mrefu zaidi hadi kutoka nje ya mfumo wa jua na kupiga selfie ya solar system baada ya kuwa safarini kwa zaidi ya miaka 40!
Miaka 40...????
 
Quran imeandikwa life iko hapa duniani ila wao wanapinga na kuanza theory za viumbe wa mars cjui Jupiter na zote Ni theory hakuna aliesibitisha uhai Zaid ya hapa earth


Uhai wa sisi viumbe wa duniani ni utakuwa ni hapa hapa duniani, lakini kuna viumbe wengine wanaishi nje ya Galaxy yetu, (exterrestial life) hii ni kwa mujibu wa Qur'an.
 
Hapa huwa nahisi tulipigwa na wamarekani 😀


Tena tulipigwa kitu kizito, mtu atajiuliza; hivi kama walikwenda mwaka 1969 vipi mbona leo ambapo sayansi imeimarika na nyenzo za usafiri zimekuwa bora washindwe kwenda??
 
Miaka 40...????
Ndiyo.Kwa sasa kimeanza kupoteza mawasiliano ila bado kinasafiri kwa mwendokasi ule ule na kitaendelea kusafiri.Ndani imebeba golden disk yenye record za watu wanyama na taarifa mbalimbali kuhusu dunia ili endapo itatokea ikakukatana na viumbe katika safari yake waweze kuitambua dunia na viumbe vyake.
 
Tena tulipigwa kitu kizito, mtu atajiuliza; hivi kama walikwenda mwaka 1969 vipi mbona leo ambapo sayansi imeimarika na nyenzo za usafiri zimekuwa bora washindwe kwenda??
Waende mara ngapi? Hivi unafuatilia vyema habari za anga au unakisia kisia?
 
Tena tulipigwa kitu kizito, mtu atajiuliza; hivi kama walikwenda mwaka 1969 vipi mbona leo ambapo sayansi imeimarika na nyenzo za usafiri zimekuwa bora washindwe kwenda??
Armstrong alipofanya interview na wanasayansi tofauti na akashindwa kujibu maswali mengi aliyoulizwa, ndiyo watu wakashtuka ni uongo
 
Back
Top Bottom