Mlimba Morogoro jau sana, ikifika saa 9 jioni haujageuka Ifakara ndio nitolee hadi kesho hiyo!

Mlimba Morogoro jau sana, ikifika saa 9 jioni haujageuka Ifakara ndio nitolee hadi kesho hiyo!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Katika harakati za mtu mweusi, nikaenda Ifakara, Morogoro.

Sasa kufika hapo mchongo ukanitaka asubuhi niende Mlimba Morogoro pale Kihansi Hydropower. Nauliza wenyeji wanasema kwa “bus” ni kama masaa 2 hivi. Nikaona sio mbaya.

IMG_0024.png

Nikaamka saa 3 kujiandaa kufika saa 4 nipo stendi. Nikapanda Noah, kutoka hapo saa 5 hivi nafika Mlimba saa 10 jioni.

Njia ni vumbi mwanzo mwisho kuanzia Ifakara kilometa zote 150+, namaliza mishe kurudi naambiwa eti hamna gari hadi kesho.

Nikasema hamna siwezi kulala huku. Nikapanda Bajaji hadi Chita. Kufika pale hamna usafiri tena, nikasubiri ikaja bajaji nyingine inaishia Mngeta, kisha kama zali nikapata Noah inaishia Kisegese.

Hapo ishafika saa 3 usiku, kuna boda ndio akakubali kunipeleka Ifakara kwa 25,000/= aisee.

Wenye magari kule wana ringa sana.
 
Katika harakati za mtu mweusi, nikaenda Ifakara, Morogoro.

Sasa kufika hapo mchongo ukanitaka asubuhi niende Mlimba Morogoro pale Kihansi Hydropower. Nauliza wenyeji wanasema kwa “bus” ni kama masaa 2 hivi. Nikaona sio mbaya.
View attachment 3109716
Nikaamka saa 3 kujiandaa kufika saa 4 nipo stendi. Nikapanda Noah, kutoka hapo saa 5 hivi nafika Mlimba saa 10 jioni.

Njia ni vumbi mwanzo mwisho kuanzia Ifakara kilometa zote 150+, namaliza mishe kurudi naambiwa eti hamna gari hadi kesho.

Nikasema hamna siwezi kulala huku. Nikapanda Bajaji hadi Chita. Kufika pale hamna usafiri tena, nikasubiri ikaja bajaji nyingine inaishia Mngeta, kisha kama zali nikapata Noah inaishia Kisegese.

Hapo ishafika saa 3 usiku, kuna boda ndio akakubali kunipeleka Ifakara kwa 25,000/= aisee.

Wenye magari kule wana ringa sana.
Ngoja nilete Noah yangu huko sitakosa hata Laki moja kwa siku. Sema haimalizi Mwaka inakufa
 
Kule kuna maisha ya kukariri.
Watu wengi husafiri asubuhi na mchana kabla ya saa 9.
Zaidi ya hapo ukiona gari labda ya serikali/kanisa au la wagonjwa.
Kule bado wapo nyuma sana.
Sana man. Saaaana. Mwendo wa vigodoro tu.

Sijui kama watafikishiwa rami. Ifakara to Ruaha sahivi mkeka mmoja amazing sana aisee
 
Sana man. Saaaana. Mwendo wa vigodoro tu.

Sijui kama watafikishiwa rami. Ifakara to Ruaha sahivi mkeka mmoja amazing sana aisee
Nilikuwa huko juzi kati.
Niliona ile lami ya Ruaha kwenda Ifakara ipo poa.
Shida ipo Ifakara kwenda Mlimba.
Ifakara kwenda Malinyi
Ifakara kwenda Mahenge.
Mashimo na vumbi la kufa mtu.
 
Back
Top Bottom