MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Sumbawanga - Kala nako basi ni moja tu.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😂😂😂Hahaha DahKuna sehem inaitwa IMALAMPAKA ipo Tabora.. huko ukienda unahisi haurudi tena.. nilipanda aina zote za Usafiri, Boda, Bus, mpaka Punda kasoro treni, Meli na ndege.
ArushaTanzania nzima jau, ukiachilia Dar sidhani kama kuna mkoa mitaa yake inafikika kirahisi na muda wowote kama Dar
🤣🤣🤣🤣 aiseeeKuna sehem inaitwa IMALAMPAKA ipo Tabora.. huko ukienda unahisi haurudi tena.. nilipanda aina zote za Usafiri, Boda, Bus, mpaka Punda kasoro treni, Meli na ndege.
Siku likitokea la kutokea huko kwa wakwe zangu siendi.Katika harakati za mtu mweusi, nikaenda Ifakara, Morogoro.
Sasa kufika hapo mchongo ukanitaka asubuhi niende Mlimba Morogoro pale Kihansi Hydropower. Nauliza wenyeji wanasema kwa “bus” ni kama masaa 2 hivi. Nikaona sio mbaya.
View attachment 3109716
Nikaamka saa 3 kujiandaa kufika saa 4 nipo stendi. Nikapanda Noah, kutoka hapo saa 5 hivi nafika Mlimba saa 10 jioni.
Njia ni vumbi mwanzo mwisho kuanzia Ifakara kilometa zote 150+, namaliza mishe kurudi naambiwa eti hamna gari hadi kesho.
Nikasema hamna siwezi kulala huku. Nikapanda Bajaji hadi Chita. Kufika pale hamna usafiri tena, nikasubiri ikaja bajaji nyingine inaishia Mngeta, kisha kama zali nikapata Noah inaishia Kisegese.
Hapo ishafika saa 3 usiku, kuna boda ndio akakubali kunipeleka Ifakara kwa 25,000/= aisee.
Wenye magari kule wana ringa sana.
Ukubwa ni ishuLack of government support.....ukubwa sio issue.
Sijawahi kufika hii mikoa miwili.Arusha
Mwanza
Vibaka ni wengi jioniKunakua hamna usafiri sababu ya mlima au usiku hamna wateja??
Itakuwa abiria wachache sana, kumepoozaMorogoro kote kilosa ukipeleka gari unavuna pesa,usafiri wa kule ni noah tu watu wenye mabus dar wapeleke morogoro haswa barabara ya kilombero lpaka ifakara,kuna pesa sana
Kumbe Ifakara napo bado sanaKule kuna maisha ya kukariri.
Watu wengi husafiri asubuhi na mchana kabla ya saa 9.
Zaidi ya hapo ukiona gari labda ya serikali/kanisa au la wagonjwa.
Kule bado wapo nyuma sana.
Hata Dar kuna maeneo ikifika usiku usafiri shidaTanzania nzima jau, ukiachilia Dar sidhani kama kuna mkoa mitaa yake inafikika kirahisi na muda wowote kama Dar
Abiria watakua wengi wakiona usafiri upoKumsubiri abiria mmoja kama yeye?
Wilaya ya Sikonge hiyo mzeeKuna sehem inaitwa IMALAMPAKA ipo Tabora.. huko ukienda unahisi haurudi tena.. nilipanda aina zote za Usafiri, Boda, Bus, mpaka Punda kasoro treni, Meli na ndege.
Kuna basi moja la saa 7 kama sikosei inaitwa SARDINI / SADINI hilo likienda leo linarud kesho alfajiri..Wilaya ya Sikonge hiyo mzee
Ahahahaha napajua vizuri.
OkNilienda Matombo juzijuzi kikazi. Shida sana kule. Vumbi mwanzo mwisho.