Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Gidhim,Tumati,Endamilay,Qamtananat,Geterer,Hyderer!Dongobesh
100k *300 days unapata milioni 30 sawa sawa na noah ngapi??Ngoja nilete Noah yangu huko sitakosa hata Laki moja kwa siku. Sema haimalizi Mwaka inakufa
Huku pesa ipo kwenye:Mbali na kilimo kuna fursa gani mitaa hiyo mkuu?
Me wananiambia eti sahivi wamechonga barabara msimu wa mvua usipime.Nilikuwa huko juzi kati.
Niliona ile lami ya Ruaha kwenda Ifakara ipo poa.
Shida ipo Ifakara kwenda Mlimba.
Ifakara kwenda Malinyi
Ifakara kwenda Mahenge.
Mashimo na vumbi la kufa mtu.
Dar is the epitome of public TransportTanzania nzima jau, ukiachilia Dar sidhani kama kuna mkoa mitaa yake inafikika kirahisi na muda wowote kama Dar
Nilienda Matombo juzijuzi kikazi. Shida sana kule. Vumbi mwanzo mwisho.Morogoro yote jau mkuu. Kutoka wilaya Moja kwenda nyingine kunakuwaga na gari Moja ukiikosa mpaka kesho Tena😂
Katika harakati za mtu mweusi, nikaenda Ifakara, Morogoro.
Sasa kufika hapo mchongo ukanitaka asubuhi niende Mlimba Morogoro pale Kihansi Hydropower. Nauliza wenyeji wanasema kwa “bus” ni kama masaa 2 hivi. Nikaona sio mbaya.
View attachment 3109716
Nikaamka saa 3 kujiandaa kufika saa 4 nipo stendi. Nikapanda Noah, kutoka hapo saa 5 hivi nafika Mlimba saa 10 jioni.
Njia ni vumbi mwanzo mwisho kuanzia Ifakara kilometa zote 150+, namaliza mishe kurudi naambiwa eti hamna gari hadi kesho.
Nikasema hamna siwezi kulala huku. Nikapanda Bajaji hadi Chita. Kufika pale hamna usafiri tena, nikasubiri ikaja bajaji nyingine inaishia Mngeta, kisha kama zali nikapata Noah inaishia Kisegese.
Hapo ishafika saa 3 usiku, kuna boda ndio akakubali kunipeleka Ifakara kwa 25,000/= aisee.
Wenye magari kule wana ringa sana.
Hizi ni hesabu za online.....kwenye real world ya Mlimba hakuna kitu hicho.100k *300 days unapata milioni 30 sawa sawa na noah ngapi??
Ukivizia kipisi (treni)cha makambako to mkamba unapiga baoWatu wanaishi nalo yaani inapita Fuso inatimua vumbi watu ata kusema wazibe pua hamna.
Lack of government support.....ukubwa sio issue.Ndio maana watu wa Morogoro bado wanalia sana na barabara,
Barabara zote zipo Morogoro mjini tu ndanindani hamna kitu
Halafu mkoa nao mi mkubwa sana, masaa manne mtu unasafiri ndani ya mkoa mmoja tu. Huu mkoa unatakiwa ugawanywe, watu wa ifakara na Mlimba wako mbali mno na Morogoro mjini, wako karibu na Njombe kuliko Morogoro mjini
Issue nayoona hapa ni WatejaKunakua hamna usafiri sababu ya mlima au usiku hamna wateja??
DahAbiria wapo sema mazoea tu man. Washazoea jioni abiria wa kubahatisha.