Mliofanikisha kujenga nyumba, Tupeane uzoefu hapa

Mliofanikisha kujenga nyumba, Tupeane uzoefu hapa

bado najenga, nikimaliza nitasimulia. Nilianza hivi, kuanzia January mwaka 2018 hadi 2019 Desemba nilikuwa naweka akiba nikafikisha sh milioni 5, milioni 5 hiyo nilinunua kiwanja.

mwaka 2020 niliweka akiba ikafika milioni 2, nilimwaga mawe trip 19 saiti hapa ilinigharimu kama sh mil 1.3.

nikabakiwa na sh 700,000, nikawaza niweke Tofali hii hela? Au niendelee kuitunza kama akiba? kabla sijaamua cha kufanya, siku moja nimeenda site nilimtembelea jirani yangu kwenye kiwanja changu, yeye alikuwa anainua boma, nikamuuliza swali amepata wapi ujasiri wa kujenga nyumba kwa ramani yenye ukubwa ule? ( ilikuwa na vyumba vinne viwili self, jiko, sebule, dinning, study room, stoo n.k) akaniambia tofali ameweka watu wanafyatua ananunua tofali moja la udongo ambalo halijachomwa sh 100 anamlipa mpanga tanuri sh 50,000. mchoma tanuri sh 70,000 kwa njia hiyo imemuwezesha kufika hapo alipo. na Mimi "nikakopi nikaenda kupesti"

sikutunza hela tena kama akiba badala yake nikawa nagharamia uandaaji wa tofali, mwaka ule nikawa nimesogeza matofali ya kutosha ilinigharimu kama milioni 2.5, nikawa ninamawe, na Matofali site.

Kuanzia January 2021 hadi Mei nilifanikiwa kuweka akiba ya sh milioni 2, nilimtafuta fundi nikampa ramani akanijengea msingi kwa milion 1, fedha nyingine nilinunulia vifaa mbalimbali vya ujenzi kama saruji n.k. nikapatana naye tena fundi huyo kujenga boma kwa sh mil.1.2, kwa makubaliano yakumlipa kwa awamu. Kwa sasa nafunga linta/beam, nasogea taratibu huo ndio uzoefu wangu kwa kifupi
 
Hapa umenifungua, MAWE, then MCHANGA, then TOFALI, thanks
.....hela ya fundi, ramani, na mwisho kabisa usisahau kununua gunia la mahindi kwa ajili ya unga, gunia la dagaa (kauzu) na deba kadhaa za maharage!! Kwa ajili ya kuanza maisha mapya ya kujibana!!

Maana ujenzi siyo wa mchezo mchezo kama wewe siyo mpiga dili, hunq mshahara mkubwa, au huna biashara ya kukuletea faida kubwa! Na ndiyo kipindi hiki, ndipo utakuta unanuniwa kweli kweli na wale wenzetu wa Beijing!
 
Bila shaka ulijikita kwenye ujenzi wa jumba, sio nyumba!
Nmejenga nyumba 3 kwa Miaka 3 mfululizo

December2017 -march 2018
nyumba ya kwanza IKAKAMILIKA

November 2018 - may 2019
Nyumba ya pili IKAKAMILIKA

December 2019- June 2020
Nyumba ya 3 IKAKAMILIKA.

Mwaka 2021,
Mambo yameyumba NMEFULIA na SINA HAMU KABISA Tena na ujenzi
 
.....hela ya fundi, ramani, na mwisho kabisa usisahau kununua gunia la mahindi kwa ajili ya unga, gunia la dagaa (kauzu) na deba kadhaa za maharage!! Kwa ajili ya kuanza maisha mapya ya kujibana!!

Maana ujenzi siyo wa mchezo mchezo kama wewe siyo mpiga dili, hunq mshahara mkubwa, au huna biashara ya kukuletea faida kubwa! Na ndiyo kipindi hiki, ndipo utakuta unanuniwa kweli kweli na wale wenzetu wa Beijing!
Mkuu, nikijenga bila Ramani kuna tatizo?
 
Nmejenga nyumba 3 kwa Miaka 3 mfululizo

December2017 -march 2018
nyumba ya kwanza IKAKAMILIKA

November 2018 - may 2019
Nyumba ya pili IKAKAMILIKA

December 2019- June 2020
Nyumba ya 3 IKAKAMILIKA.

Mwaka 2021,
Mambo yameyumba NMEFULIA na SINA HAMU KABISA Tena na ujenzi
kwanza kabisa HONGERA SANA, nyumba tatu sio mchezo mkuu, mimi ndo kwanza naangaikia kamoja haka na kananitoa jasho sana!
 
Ela ya ujenz inayotoka kdg kidg huwez yasikia maumivu,

Nunua material kidg kidg,
Ukifika hatua flan unaita mafundi wanatia kambi saiti moja kwa moja mpaka unamaliza
 
Kwanza usifanye ujenzi uwe Kama ni adhabu alaf jichange ukipata hela anza kununua material piga msingi na utulie kdogo nunua tofal tafuta hela ya fundi alaf Anza kunyanyua boma taratbu, ukimaliza tulia jichange mfuko unenepe alaf nunua mbao na bat upaue kwa Mara moja
Baada ya hapo tulia isahau nyumb kdog hata miez 4 weka frame za madirishan na mlango.

Ukishazuia watu wasiweze kuingia ndan hapo unaanza kupiga finishing taratbu unaweza kuweka frame za milango na kumwaga jamvi chini na badae unapiga draft juu na kupiga plasta ndani[emoji109][emoji109] hapo unaweza hata kuzba dirisha na gunia na ukahamia ili kusave na hela ya Kodi ukawa unamalizia ujenzi ukiwa ndani.

Cha msingi usikubali ujenzi uwe adhabu , maana ukifanya Kama adhabu utajinyima hata kula na utakua na madeni mengi mtaani kitu ambacho itakua ni tatzo na utapoteza amani, ww tafta hela weka na akiba kdogo inayobaki tupia yote kwenye ujenzi.
 
Kama kiwanja hakina hati, unajenga tu. Ila kama umeshepewa hati miliki, basi ni vyema ukaenda tu ofisi za Ardhi Wilaya ili ukapate muongozo.
sikuwahi kulijua hili mkuu, kiwanja kimepimwa, nishakifanyia michakato yote ya hati miliki, nasubir anytime nitapewa
 
Kwanza usifanye ujenzi uwe Kama ni adhabu alaf jichange ukipata hela anza kununua material piga msingi na utulie kdogo nunua tofal tafuta hela ya fundi alaf Anza kunyanyua boma taratbu, ukimaliza tulia jichange mfuko unenepe alaf nunua mbao na bat upaue kwa Mara moja
Baada ya hapo tulia isahau nyumb kdog hata miez 4 weka frame za madirishan na mlango.

Ukishazuia watu wasiweze kuingia ndan hapo unaanza kupiga finishing taratbu unaweza kuweka frame za milango na kumwaga jamvi chini na badae unapiga draft juu na kupiga plasta ndani[emoji109][emoji109] hapo unaweza hata kuzba dirisha na gunia na ukahamia ili kusave na hela ya Kodi ukawa unamalizia ujenzi ukiwa ndani.

Cha msingi usikubali ujenzi uwe adhabu , maana ukifanya Kama adhabu utajinyima hata kula na utakua na madeni mengi mtaani kitu ambacho itakua ni tatzo na utapoteza amani, ww tafta hela weka na akiba kdogo inayobaki tupia yote kwenye ujenzi.
Mkuu, pamoja na ushauri wa wana JF wengine, ushauri wako naufanyia kazi maana sio siri najitesa sana!
pamoja sana mkuu 👍
 
Hongera kwa kuamua kuanza ujenzi.

Ni jambo la kishujaa .
Unajengea wapi?.

Ila asikuambie mtu, ujenzi wa nyumba ni balaa, ila ukienda mdogo mdogo na kujipa miaka 3 - 4 , nyumba inaisha.

Kila la kheri
 
Kwanza usifanye ujenzi uwe Kama ni adhabu alaf jichange ukipata hela anza kununua material piga msingi na utulie kdogo nunua tofal tafuta hela ya fundi alaf Anza kunyanyua boma taratbu, ukimaliza tulia jichange mfuko unenepe alaf nunua mbao na bat upaue kwa Mara moja
Baada ya hapo tulia isahau nyumb kdog hata miez 4 weka frame za madirishan na mlango.

Ukishazuia watu wasiweze kuingia ndan hapo unaanza kupiga finishing taratbu unaweza kuweka frame za milango na kumwaga jamvi chini na badae unapiga draft juu na kupiga plasta ndani[emoji109][emoji109] hapo unaweza hata kuzba dirisha na gunia na ukahamia ili kusave na hela ya Kodi ukawa unamalizia ujenzi ukiwa ndani.

Cha msingi usikubali ujenzi uwe adhabu , maana ukifanya Kama adhabu utajinyima hata kula na utakua na madeni mengi mtaani kitu ambacho itakua ni tatzo na utapoteza amani, ww tafta hela weka na akiba kdogo inayobaki tupia yote kwenye ujenzi.
umeongeA point ya msingi Sana,

Binafs niliwahi kua na malengo ya kila mwaka niwe nimenunua kiwanja kipya na nimesimamisha nyumba moja ya biashara.

Aisee,
Ayo malengo yamenitesa mno,

maana Kuna MDA unasimamisha program nyingine ili mradi TU ile nadhiri na malengo yako yatimie.

Huu mwaka na mwakani
Napumzika kabisa kujijenga Kwanza kiuchumi.
 
Hongera kwa kuamua kuanza ujenzi.

Ni jambo la kishujaa .
Unajengea wapi?.

Ila asikuambie mtu, ujenzi wa nyumba ni balaa, ila ukienda mdogo mdogo na kujipa miaka 3 - 4 , nyumba inaisha.

Kila la kheri
Shukrani Mkuu, Asante kwa kunitia moyo!
 
umeongeA point ya msingi Sana,

Binafs niliwahi kua na malengo ya kila mwaka niwe nimenunua kiwanja kipya na nimesimamisha nyumba moja ya biashara.

Aisee,
Ayo malengo yamenitesa mno,

maana Kuna MDA unasimamisha program nyingine ili mradi TU ile nadhiri na malengo yako yatimie.

Huu mwaka na mwakani
Napumzika kabisa kujijenga Kwanza kiuchumi.
mkuu asante kwa kutoa experience yako, kuna kitu najifunza hapa.
 
Back
Top Bottom