Mliofiwa na wazazi (mama), mliwezaje kuvuka kipindi hiki?

Mliofiwa na wazazi (mama), mliwezaje kuvuka kipindi hiki?

Kwanza pole sana Mkuu, na nikwambie kitu hakuna namaanisha hakuna kitu unaweza ambiwa au hata watu wakucomfort vp kikaweza japo kupunguza maumivu ya kuondokewa na mama hakipo. Mimi nina miaka mitatu mama yangu amefariki ila kila nikiingia chumbani kwake najikuta machozi yanadondoka yenyewe nikiwa hata bar nikisikia nyimbo yoyote inayomhusu mama mimi ni kilio siwezi kujizuia kwenye hili hata kidogo. Ni Mungu mwenyewe ndio akawe mfariji wako ila Mama anauma aisee acha kabisa.
 
Mkuu pole sana.

Haielezeki na haivumiliki ila unatakiwa kuukubali ukweli kwamba hayupo tena.

Mimi alifia mikononi mwangu halafu ndio nilikua nimeanza kupanda mlima wa mafanikio angalau nianze kulipa fadhila zake ila ikashindikana.

Kinachoniumiza zaidi ni kwamba ali sacrifice maisha yake kwa mafanikio yangu ya ya watoto wake wengine kwa maana kwamba nilitafta hela nimpeleke India akakataa kwamba hata kama akienda akapata nafuu bado atakufa so nisiharibu hela, akakataa kabisa.

Akasema kama nina hela ya kumtibu, basi niitumie kusaidia ndugu zangu wengine (nina ndugu zangu wengine mambo yao hayakua sawa) akaniambia niwasaidie hao ila sio yeye.

Nikapambana nae Muhimbili lakini ikawa hivyo so akafariki mikononi.

Kwa sacrifice aliyofanya, ikabidi na mimi niamue jambo moja, nikaamua ku sacrifice kila kitu changu kwa miaka 4 kuwabust hao jamaa, yaani sikufanya maendeleo yangu binafsi yoyote kwa miaka 4 angalau wakae level. Kwa miaka 4 mapato yangu yote nimeffanya hivyo.

Anyway, nimetoka kumuota usiku huu halafu naamka nakutana na hii mada, mada kama hizi hua sipendi kuzisoma maana naishia kulia tu.

Mama yangu endelea kupumzika kwa amani, najua sacrifice yako kwenye maisha yangu haina mfano na sitakaa kuja kuilipa hata robo. Namini one day tutaonana tena.
Machozi yamenitoka mnoo, ama kweli hakuna upendo mkuu Duniani kama wa mama, Mungu aendelee kuwapa pumziko la milele zetu wote waliotangulia mbele ya haki.
Mungu aendelee kuwapa afya njema na baraka zitokazo kwake mama zetu walio hai maana hatuna chochote Cha kuwalipa ili kufidia Yale waliyowahi kututendea na maumivu mazito waliyokwisha kupitia kwaajili yetu

Sent from my CPH2239 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu zangu wapendwa habari za muda mrefu tena.
Ninajitahidi kuzoea hali ya kutokuwa na mama ila bado siamin kama ndo mazima.... Inauma lkn hakuna namna.
Mama tulimzika na matanga tayri.

Kuna kauli nilizokutana nazo kwa kipindi hiki nazikumbuka sana naomba niweke hapa.

Dadammoja ambaye yeye ni Yatima na amekuwa vizuri mikononi mwa ndugu wengine na sasa yupo JWTZ alinipigia simu na kuniambia: SHUKURU WEWE MZAZI AMEKUKUZA HADI HAPO ILA WENGINE WANAPOTEZA WAZAZI MAPEMA ZAIDI.
hii kauli iliniingia kichwani.

Binamu yangu mmoja aliniambia.
Nimekuja msibani sio kwa ajili ya baba yenu(kwake ni mjomba) wala ninyi (sisi sasa) ila ni sababu za mama yenu (marehemu) the way alivyoishi na sisi....ana heshima kubwa. Kuna vitu alitengeneza ambavyo vina msaada mkubwa kwetu na sisi tuendeleze.
Pia SWALA MSIBA LISAHAU MAPEMA MAANA KUNA MAISHA BAADA YA MSIBA.

Wa tatu ni broo mmoja ambye hata simjui.
Mama yako yupo sehemu salama zaidi ya hapa duniani hakuna haja ya kusikitika.

Hizi ni chache zinazo run kichwani muda wote ila ni nyingi sana ninazo kumbuka .
Nathamini kila mchango wa mwana JF kwan nimepitia kila comment na zimenifariji sana sana.
Pole Sana,

Huwa nawazaga leo nipo ma mama na najisemea ndiyo kila kitu kwangu,vipi siku naambiwa mama yako hatunae tena,yaani ni fumbo,

Mama ananiambiaga yaani nawaza nikifa sijui nitakuacha ktk hali gani mwanangu,yaani nakuwazia wewe kuliko hata wadogo zako,
 
ni kweli inaumiza ila ninachokiona kwako ni kama unajiendekeza unalazimisha uchungu. Huenda wewe ni mnyak. Likipita piga moyo konde ruhusu maisha mengine yasonge Mkuu kila mtu maewahi kufiwa na mtu wake wa karibu. Ila kuendelea kuandika andika kila saa huku ni utoto na kutafuta faraja ya lazima na kutafuta Huruma

Pole sana Yesu akutie Nguvu na Roho ya uchungu ikutoke
Mmmmmmh anajiendekeza?

Haujui tu,yakupasa[emoji40]
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
ni kweli inaumiza ila ninachokiona kwako ni kama unajiendekeza unalazimisha uchungu. Huenda wewe ni mnyak. Likipita piga moyo konde ruhusu maisha mengine yasonge Mkuu kila mtu maewahi kufiwa na mtu wake wa karibu. Ila kuendelea kuandika andika kila saa huku ni utoto na kutafuta faraja ya lazima na kutafuta Huruma

Pole sana Yesu akutie Nguvu na Roho ya uchungu ikutoke
Kudeka muhimu kaka.
Katika kuandika huku nimegundua mengi sana
 
Wandugu habari, mama alikuwa mgonjwa na akaanza matibabu ila akiwa hospital akafariki. Hapa naenda msibani, ila siwezi kuvumilia kulia mara kwa mara licha ya kujikaza.

Kwa mliopata hii changamoto, mliwezaje kumove on? Nikifikiria ameenda bado mdogo hata 50 hajafika, ni mengi nawaza yananiumiza ila sometimes inabidi nifanye ujinga tuu ili kupoteza mawazo.
Tushapoa maumivu ila sometimes unagombana na mtu anamtukana mama yako aliekufa tena saa nyingine mkeo Kabisa anamtukana mama yako.Mke Wangu ana wazazi wake wote wawili lkn tukigombana anawatukana wazazi Wangu waliokufa bila woga
 
Mkuu kifo hakizoeleki na ngumu Sana mtu wa karibu yako akakutoka na utachukuwa mda Sana kumsahau na hata ukimsahau Kuna siku unaweza ukaanza kulia mwenyewe
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Tushapoa maumivu ila sometimes unagombana na mtu anamtukana mama yako aliekufa tena saa nyingine mkeo Kabisa anamtukana mama yako.Mke Wangu ana wazazi wake wote wawili lkn tukigombana anawatukana wazazi Wangu waliokufa bila woga
Mh na bado ni mkeo?
 
Mimi nimefiwa na baba yangu miaka kama miwili imepita[emoji24][emoji24] na bado akili yangu haija kubali kwamba ameniacha!
Huwa nalia kila ninapo mkumbuka na kwenye ndoto zangu huwa ninamuona ni mzima kabisa tuna endelea na maisha mazuri tulio kuwa nayo!
Yaani we acha tu ni uchungu wa hali ya juu [emoji30]
Namwomba Mwenye Enzi Mungu anipe nguvu na amani moyoni mwangu!
Nami nakuombea na wewe amani ya Mwenye Enzi Mungu iwe nawe milele walahi!
 
Kwanza nikupe Pole Sana mimi nimepita changamoto hiyo alianza Baba, baada ya mwaka akafuata mama kisha dogo aiee niliishi Jehanamu nikiwa dunian lkn Neema ya Mungu ilinipitisha salama.

Mwombe tu Mungu akusaidie ni maumivu Sana.

Pole sana!
 
Maumivu ya kufiwa na mama hayaelezeki....kuna muda unafika unatamani mamaako awe hai umueleze matatizo akusikilize akubembeleze lakini wapi....mimi wangu alifariki 2004 lakini maumivu yake hadi leo hayaelezeki

Mtumeee!
Kwa kweli Mwenye Enzi Mungu akusaidie!
 
Back
Top Bottom