Mlioishi Ulaya na Amerika, eti huko wazungu wanakula kuku wa kienyeji au wa kisasa?

Mlioishi Ulaya na Amerika, eti huko wazungu wanakula kuku wa kienyeji au wa kisasa?

Vyakula vyote vinavyoliwa duniani kwa 99% ni natural, duniani bado haijafikia kuanza kula vyakula artificial.
Hadi makuku mataahira yanayokua kwa wiki 2 tu? Ndiyomaana Vijana siku hizi wanaota manyonyo, kuku mataahira ni sumu tupu, pia ni tasteless kabisa sababu ya midawa, kuwa makini usijizolee kansa zinazoepukika.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Una nashangaa neno wanalishwa madawa , how? Yaani kuku alishwe dawa tu bila chakula?
Kuku wa huko hata kama ni kienyeji ila ni improved kienyeji ambaye anafugwa free range na kupewa chakula Cha ziada kuku bei yake unakuta ni shilling elfu 60 , maana broiler tu mwenye kilo mbili Kwa bei ya kule ni kuanzia 20 - 30 elfu
Lakini unakuta kule bar maid kwa mwezi anakunja 4M,mlinzi 6M,dereva 10M
 
Nachojua mzungu ana hela nyingi na kama ni kula daima anapendelea kula vilivyo bora sijajua kwa maendeleo tulionayo hapa duniani kiasi cha kuanza kufuga broiler wa biashara na wanaliwa kwelikweli.

Nachojua hii teckonolojia ni ya kwao mataifa yaliyoendelea sasa swali ni je na wao wanawatafuna hawahawa broiler na je ulaya huko wanafuga pia wa kienyeji kama hawa wa kwetu.?
Nilikuwa najua Mavyakula ya huko ulaya ni kama yale ya KFC tuu...kumbe hadi kienyeji unapata.
 
Hadi makuku mataahira yanayokua kwa wiki 2 tu? Ndiyomaana Vijana siku hizi wanaota manyonyo, kuku mataahira ni sumu tupu, pia ni tasteless kabisa sababu ya midawa, kuwa makini usijizolee kansa zinazoepukika.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
Kuku kukua kwa muda mrefu sana sio sifa nzuri, ni kwa sababu ya genes mbaya zisizo bora za udumavu na pia kukosa matunzo sahihi ya chakula na dawa. Pia kuku wa aina hiyo ni muendelezo wa umaskini tu kwa anayefuga.
 
Kuku kukua kwa muda mrefu sana sio sifa nzuri, ni kwa sababu ya genes mbaya zisizo bora za udumavu na pia kukosa matunzo sahihi ya chakula na dawa. Pia kuku wa aina hiyo ni muendelezo wa umaskini tu kwa anayefuga.
Heri kujifunza zaidi kuliko kujua kila kitu maana ujuaji mwingi huondoa maarifa.
Jikite kwenye siasa tu hapa umechemka, sana sana una ubishi tu usio na faida.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Sijawahi fika Wala kuishi ulaya.

Nimefanya kazi na WA Canada na wa Australia walisema namna unavyoona huku Kuna kuku wa kisasa na kienyeji na kwao ni vilevile tu kienyeji wapo na bei Iko juu zaidi. Sema wa kwao wameboreshwa.

Pia nimewahi sikiliza mahubiri ya mchungaji mmoja wa kisabato anaitwa Mark Finley yeye alisema Hali kuku wa kisasa ni mzungu anaishi marekani.
 
Kuku kukua kwa muda mrefu sana sio sifa nzuri, ni kwa sababu ya genes mbaya zisizo bora za udumavu na pia kukosa matunzo sahihi ya chakula na dawa. Pia kuku wa aina hiyo ni muendelezo wa umaskini tu kwa anayefuga.
Kwahiyo Hawa broiler tuwaweke kundi la kuku aina Gani ?
 
Swali la kujiuliza je wazungu wanakula kuku wa nyama au wa Mayfair....bro kuku wa Mayfair waxungu hawali wanakula hao mnaoita wa wk wa nyama cause ndo special kwa kuliwa wa mayai wakimaliza kazi zao wanawateketeza
Kuku wa kizungu(layers, broillers, saso na kroillers etc) ni kuku waliobuniwa Marekani kwa ajili ya kuondoa shida ya upungufu wa kitoweo nchini kwao na baadaye kuuza teknolojia hiyo kwenye mataifa mengine.

Wanakula kama kawaida, hata kwetu si watu wanakula vizuri tu?


Kwani food value yake ipoje?

Maana Waafrika tunaishi kwa kukaririshwa mambo, sijui mayai/kuku wa kizungu hawafai etc etc, ukimuuliza anayesema hivyo akwambie terms za kisayansi alizotafiti kuonesha kuwa hawafai, utakuta hana.
 
Hadi makuku mataahira yanayokua kwa wiki 2 tu? Ndiyomaana Vijana siku hizi wanaota manyonyo, kuku mataahira ni sumu tupu, pia ni tasteless kabisa sababu ya midawa, kuwa makini usijizolee kansa zinazoepukika.
Hakuna uhusiano wowote wa kuku wa kisasa na vijana kuota manyonyo au kansa. Dawa za kuku ni dawa kama wewe unavyopatiwa chanjo au antibiotics ukiumwa, acha kusikiliza stori za watu wajinga wa mtaani na kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Kuku wa kizungu(layers na broillers, saso, kroillers) ni kuku waliobuniwa Marekani kwa ajili kuondoa shida ya upungufu wa kitoweo nchini kwao na baadaye kuuza teknolojia hiyo kwenye mataifa mengine.

Wanakula kama kawaida, hata kwetu ni watu wanakula vizuri tu.


Kwani food value yake ipoje?

Maana Waafrika tunaishi kwa kukaririshwa mambo, sijui mayai/kuku wa kizungu hawafai etc etc, ukimuuliza anayesema hivyo akwambie terms za kisayansi alizotafiti kuonesha kuwa hawafai, utakuta hana.
Waafrika wengi wana ujinga mwingi sana wa kurithi na bahati mbaya sana wanarithishana huo ujinga kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
 
Nachojua mzungu ana hela nyingi na kama ni kula daima anapendelea kula vilivyo bora sijajua kwa maendeleo tulionayo hapa duniani kiasi cha kuanza kufuga broiler wa biashara na wanaliwa kwelikweli.

Nachojua hii teckonolojia ni ya kwao mataifa yaliyoendelea sasa swali ni je na wao wanawatafuna hawahawa broiler na je ulaya huko wanafuga pia wa kienyeji kama hawa wa kwetu.?
Kisasa tena wanakua frozen hata mpaka mwaka mmoja
 
Back
Top Bottom