Mliokaririshwa uongo kuwa mishahara ya walimu ni midogo kuliko watumishi wengine wa serikali, nawaanikia hapa

Mliokaririshwa uongo kuwa mishahara ya walimu ni midogo kuliko watumishi wengine wa serikali, nawaanikia hapa

10. Afisa utumiishi Hawa ndio wazee wa madili ya watumishi hewa.
emoji117.png
Mtu anafariki, ripoti haiendi hazina kusitisha mshahara. Inatolewa ripoti ya mwajiriwa kubadili account yake, mshahara wa marahemu wanaula hata miaka 10 mfulurizo bila yeyote kujua.
emoji117.png
mtu anamakosa ya kinidhamu,kasimamishiwa mshahara. Ripoti haiendi hazina, inabadilishwa tu account. Wanaupiga kimya kimya. Ukisamehewa ukarudishiwa mshahara, ule wa nyuma hata uulizii.
emoji117.png
mtu anaripoti Ila haendi kituo Cha KAZI, au anaacha kazi anaenda zake private kwa muda.
wanakula dili na afisa utumishi, wanaugawana nusu nusu huku yeye Yuko zake private sector anapiga Ela nyingine.

Kama Kuna mtumish mwngne wa halmashaur nmemsahau nikumbushe.

Ila kiuhaisia mwalimu nje ya mshahara sijui atapiga dili gani atoboe,

ukiachilia mbali suala la twisheni ambalo bado kipato chenyewe Ni kidg mno na jasho linalomtoka Ni jingi mno

Sijui atapiga dili gan jingine maana vitabu vyote vya serikali vimeandikwa "HAKIUZWI", boksi lenyewe la chaki Mtaani halizidi hata elfu 2.
AKSANTE baba mkuru sasa kama mtumishi ikikutokea hivi uwafanyeje sababu linanihusu sana hili umenifungua macho! JF idumu!
 
Sahihi kabisa. Kinachotofautisha walimu na kada zingine ni bonuses, n.k n.k nisiende mbali sana.
 
Walimu wengi ni masikini tena wanadharaulika kwasababu ni wachafu hawajipendi, hawavai nguo Safi kila siku nguo hiyo hiyo kauka nikuvae, wake zao ni Walevi wa pombe za kienyeji... Ndio maana wanawake wengi hukataa kuolewa na mwalimu. Mtu akishajua wewe ni mwalimu basi anakushusha heshima na unadharaulika mpaka na watoto wadogo maana wanajua wewe ni fukara tu Wali maharage.
Ndo ivoivo! ilikuwaga wanajeshi/polisi/magereza/nk! tangu enzi za Nyerere kwa kuwa vilikuwa vinapatikana bureeee!! watu walizi dharau sana hizo kada, lkn leo post za jeshi ni hot cake mnoo!

hii kada ya ualimu mnaidharau leo sababu inauhitaji mnooo!! wa watumishi siku ikishiba watumishi itapaa na wala hutasema hivi tena! wala siyo mbali na hapa.....

ni kama lilivyo jeshi la leo watu mpaka wanahonga kupata hizo nafasi lkn wapi!...zamani mlikuwa mna bembelezwa kuingia magereza eti mnaita kazi za jasho,hawakusoma lkn leo je???!
 
Kujisifia wizi na madili kinyume na maadili kwa kada zingine ni aibu kwa Taifa na siku zote hakuna mwisho mzuri. WAlimu wana pesa za halali kwa mfano tuition ambazo ni nyingi sana mitaani. Mwalimu akistaafu bado taaluma yake inahitajika kwenye jamii na anaendelea kupiga pesa ya halali na yenye heshima! Lakini kichwa cha mwalimu kina chaji muda wote hadi uzeeni na anawasaidia sana watoto wake!! Ualimu ni mzuri na unastahili kuheshimiwa sana!
Wee Ni wa mbinguni,
Kubishana na wewe siwezi[emoji4]
 
Ni afadhali niishi kwa kiwango kinachoendana na kipato changu kuliko kupokea rushwa na kujidanganya kuwa una kipato kikubwa, fainali ikifika kuna mmoja anaumbuka! Hivi mlishawahi kushuhudia maisha ya polisi wastaafu huko mitaani!!! Ni fedheha!! Wengi huishia kulinda kwenye majumba na maduka ya watu kwa kutumia virungu!! Mambo ya rushwa kwishney!!
Wee kwanza jinsia gan,
uandishi wako umenipa walakini[emoji848]
 
Kwa haraka haraka tu, nimeelewa kwamba katika kada zote ni walimu pekee wasioiba Mali za umma, umasikini mkubwa kwa sisi wananchi unachombezwa na hao wezi uliowataja, TAKUKURU ingekuwa serious kushughulikia rushwa naamini serikali ingepata pesa nyingi mnooo!

Ila sasa TAKUKURU wapo busy kukimbizana na wanaoinanga CCM, nje ya hapo na wao wanalamba zao asali tu...
Sahii kanisa mkuu,
Wee ndo umenielewa sasa
 
Hizi thread za kuwadhihaki walimu nna uhakika zinaandikwa na majobless,Its either walifeli shule kwa uzembe wao Ama wanassbabu zingine lwzima zitakua baseless tu.

Walimu wanamishahara madogo ama mikubwa how is that your concern? Walimu ni watumishi kama watumishi wengine wanastahili kuheshimiwa kama watumishi wengine,Sioni afya kabisa kila siku mkiwadhihaki Walimu, Haiwezekani kila mtu akawa wakili,daktari ama engineer sasa mnasumbuka nn nao? Unasema laki 7 ni ndogo think twice wewe unaingiza sh ngap
Walimu kinachowabeba,
Wana akili ya maisha Sana,
Wanapata kidg,ila Wana uwezo wa kufanya maendeleo

Kuna afisa maliasili mmoja Huwa nakunywa nae pombe Hadi za laki 8, ila Hana hata kibanda Cha kujistiri na Yuko kwenye late 50s
 
Huu ndo ukweli bila haya makandokando ni ngumu sana mtumishi wa umma kutoboa.! Na serikali isopo boresha masilahi ya watumishi kamwe rushwa haiwezi kuisha
Sahii kabisa
 
Kwenye kata yetu sijaona mtu wa kada nyingine alieomba hizi kazi za muda za sensa ni walimu tu tena ni wengi.

Shule ambayo mkuu wake ndo anafanya usaili ndo wameenda kama walimu shule nzima. Sasa hapo kweli utasema hawa jamaa huko kuna maslahi waanze kugombania hizi kazi ambazo naamini tu ni za shurba na kuzurula kwiingi wakati muda huo ungeutumia kupumzika na familia ama kufanya ishu zako nyingine.
Walimu walilazimika kuomba ukarani wa sensa sababu shule zote zimefungwa kupisha zoezi hilo, sasa ulitaka wakae nyumbani wakati mtu angeweza kujaribu bahati yake akapata vi laki viwili vitatu vya ukarani!?
 
Kuna na mabwana afya kaam matrafiki TU, wanatupiga Sana elfu hamsin hamsi Za faini uku mitaani
Hawa wanasababisha vifo vingi kwa kuacha watu wale vyakula vilivyopitwa muda wa kutumika, nimeshuhudia samaki waliovunda wakiuzwa migahawani, mikate, vitumbua, maandazi nk vimeota fungus lakini bado wanauziwa watu
 
Jamii ya watanzania wanavyoelewa ni kwamba kazi ya ualimu ndiyo yenye mshahara mdogo kuliko kazi zingine zote. Hivyo hii imepelekea hadhi ya mwalimu kwenye jamii kushuka sana na mwalimu kuhesabika kuwa ni duni katika jamii. Lakini hii si kweli hata kidogo. Msichana akitaka kuchumbiwa na mwalimu anajisikia mnyonge, na mara nyingi hukataa labda akihisi kuwa umri unamtupa mkono au akiona hajapata chaguo la moyo wake.

Ukweli ni kwamba watumishi wote wa serikali (walimu na kada zingine) mishahara yao iko chini sana! Lakini ukiilinganisha hiyo mishahara yao midogo, mshahara wa mwalimu unakuwa juu kidogo kuliko kada zingine isipokuwa kwa kada ambazo wanasoma miaka mingi zaidi kama madaktari, wafamasia na wahandisi.

Ngoja niwaanikie hapa:

Mishahara ya walimu wanaoanza wenye digrii ya kwanza:
Hadi Juni 2022 walikuwa kwenye TGTS D1 = 716,000/=
Kuanzia Julai 2022 wanakuwa kwenye TGTS D1 = 771,000/=

Mishahara ya kada zingine wasio walimu wenye digrii ya kwanza:
Hadi June 2022 walikuwa kwenye TGS D1 = 710,000/=
Kuanzia Julai 2022 wanakuwa kwenye TGS D1 = 765,000/=

Kwa hiyo hadi Juni 2022 mshahara wa mwalimu ulikuwa unazidi mshahara wa kada nyingine kwa sh 6,000/=.
Kuanzia Julai 2022 mshahara waq mwalimu unazidi mshahara wa kada zingine kwa sh 6,000/= pia.

Kwa wastani mishahara ni midogo kwa wote japo jamii inaamini kuwa mwalimu ndiye mwenye mshahara mdogo wakati siyo kweli. Wahanga wa uongo huu wamekuwa ni wasichana kukataa kuolewa na walimu na kushobokea kada zingine kwa kigezo cha mshahara.

Mtumishi wa serikali akilalamika kuwa mshahara ni mdogo watu wanakimbilia kusema kuwa huyo lazima atakuwa ni mwalimu.

Nashauri tuwaheshimu sana walimu wetu, tusiwabeze bali tuwatie moyo maana kazi yao ni ngumu na ni muhimu sana. Kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa ni kukejeli walimu eti ndio wanaolalamikia nyongeza kiduchu ya mshahara mwaka huu kinyume na matarajio yao.
Nmekuelewa SANA
 
Walimu wakitaka wathaminiwe na selikari ijali maslahi yao,
just simple, walimu wote wasiombe kazi za muda uchaguzi mkuu 2025.

Selikari haiwezi kuwabana majobless eti waibe kura fisiemu iibuke kidedea.

Walimu wote kuacha kuomba kazi za muda uchaguzi mkuu 2025 Hilo haliwezekani kila mtu anajua.
Wangeanza na Sensa mwaka huu
 
Walimu Hawana dili Wala marupurupu ya ziada Kama kada nyingine, hiki Ndo kinawafanya kua maskini Sana

1. Dreva wa halmashaur ana mshahara mdg kuliko mwalimu ila atapiga dili za vifusi,mchanga,kokoto n.k night za misafara n.k

2. Afisa biashara au ardhi wa halmashaur ana mshahara mdg kuliko mwalimu,
Ila atapiga rushwa za leseni za kufa mtu.

3. Afisa mifugo au kilimo atapiga elfu tano tano za sindano mifugo ya watu au atalima mashamba yake uko uchochoroni kwa kutumia dawa au pembejeo za ruzuku za serikali.

4. Mfamasia atakula laki tano tano kila mwezi for free za cheti chake tu kutumika kwny maduka ya dawa ya watu uko mitaani uku katulia tu..

5. Daktar au nesi wa halmashaur,
Hawa dili za semina,mafunzo n.k Ni nyingi mno(covid 19, chanjo, ukoma, malelia n.k). Hapo bado hawajaiba vifaa Tiba na kuviingiza mtaani kwenye hospital binafs.
[emoji117] Kuna na mabwana afya kaam matrafiki TU, wanatupiga Sana elfu hamsin hamsi Za faini uku mitaani

6. Wahasibu na maafisa manunuzi wa halmashaur wanapiga Sana dili za kimahesabu na 10% wakishirikiana na maboss wao (wakurugenz) ili Kupiga Cha juu kwenye tenda na matumiz mbalimbali ya fedha kwny halmashaur.

7. Maengineer wa halmashaur Ndo kabsaa wezi wakubwa, wao kila mradi wa serikali wakipewa kusimamia Lazima umalizike na yeye tayar ana kijumba keshakijenga kwa material zile zile za mradi.

8. Maafisa masjala wao Ni Kama matrafiki au madalali wa viunga vya halmashaur, una faili lako pale kwa mkurugenz au mkuu wa wilaya,ili likimbie chap chap Lazima utamwachia elfu 2 au elfu 5 ya maji.

9. Afisa maliasili wa halmashaur Hawa Ni wazee wa madili na rushwa za misitu,mikaa,mbao na magendo mbalimbali ya serikali.

10. Afisa utumiishi Hawa ndio wazee wa madili ya watumishi hewa.
[emoji117]Mtu anafariki, ripoti haiendi hazina kusitisha mshahara. Inatolewa ripoti ya mwajiriwa kubadili account yake, mshahara wa marahemu wanaula hata miaka 10 mfulurizo bila yeyote kujua.
[emoji117]mtu anamakosa ya kinidhamu,kasimamishiwa mshahara. Ripoti haiendi hazina, inabadilishwa tu account. Wanaupiga kimya kimya. Ukisamehewa ukarudishiwa mshahara, ule wa nyuma hata uulizii.
[emoji117]mtu anaripoti Ila haendi kituo Cha KAZI, au anaacha kazi anaenda zake private kwa muda.
wanakula dili na afisa utumishi, wanaugawana nusu nusu huku yeye Yuko zake private sector anapiga Ela nyingine.

Kama Kuna mtumish mwngne wa halmashaur nmemsahau nikumbushe.

Ila kiuhaisia mwalimu nje ya mshahara sijui atapiga dili gani atoboe,

ukiachilia mbali suala la twisheni ambalo bado kipato chenyewe Ni kidg mno na jasho linalomtoka Ni jingi mno

Sijui atapiga dili gan jingine maana vitabu vyote vya serikali vimeandikwa "HAKIUZWI", boksi lenyewe la chaki Mtaani halizidi hata elfu 2.
 
Walimu Hawana dili Wala marupurupu ya ziada Kama kada nyingine, hiki Ndo kinawafanya kua maskini Sana

1. Dreva wa halmashaur ana mshahara mdg kuliko mwalimu ila atapiga dili za vifusi,mchanga,kokoto n.k night za misafara n.k

2. Afisa biashara au ardhi wa halmashaur ana mshahara mdg kuliko mwalimu,
Ila atapiga rushwa za leseni za kufa mtu.

3. Afisa mifugo au kilimo atapiga elfu tano tano za sindano mifugo ya watu au atalima mashamba yake uko uchochoroni kwa kutumia dawa au pembejeo za ruzuku za serikali.

4. Mfamasia atakula laki tano tano kila mwezi for free za cheti chake tu kutumika kwny maduka ya dawa ya watu uko mitaani uku katulia tu..

5. Daktar au nesi wa halmashaur,
Hawa dili za semina,mafunzo n.k Ni nyingi mno(covid 19, chanjo, ukoma, malelia n.k). Hapo bado hawajaiba vifaa Tiba na kuviingiza mtaani kwenye hospital binafs.
[emoji117] Kuna na mabwana afya kaam matrafiki TU, wanatupiga Sana elfu hamsin hamsi Za faini uku mitaani

6. Wahasibu na maafisa manunuzi wa halmashaur wanapiga Sana dili za kimahesabu na 10% wakishirikiana na maboss wao (wakurugenz) ili Kupiga Cha juu kwenye tenda na matumiz mbalimbali ya fedha kwny halmashaur.

7. Maengineer wa halmashaur Ndo kabsaa wezi wakubwa, wao kila mradi wa serikali wakipewa kusimamia Lazima umalizike na yeye tayar ana kijumba keshakijenga kwa material zile zile za mradi.

8. Maafisa masjala wao Ni Kama matrafiki au madalali wa viunga vya halmashaur, una faili lako pale kwa mkurugenz au mkuu wa wilaya,ili likimbie chap chap Lazima utamwachia elfu 2 au elfu 5 ya maji.

9. Afisa maliasili wa halmashaur Hawa Ni wazee wa madili na rushwa za misitu,mikaa,mbao na magendo mbalimbali ya serikali.

10. Afisa utumiishi Hawa ndio wazee wa madili ya watumishi hewa.
[emoji117]Mtu anafariki, ripoti haiendi hazina kusitisha mshahara. Inatolewa ripoti ya mwajiriwa kubadili account yake, mshahara wa marahemu wanaula hata miaka 10 mfulurizo bila yeyote kujua.
[emoji117]mtu anamakosa ya kinidhamu,kasimamishiwa mshahara. Ripoti haiendi hazina, inabadilishwa tu account. Wanaupiga kimya kimya. Ukisamehewa ukarudishiwa mshahara, ule wa nyuma hata uulizii.
[emoji117]mtu anaripoti Ila haendi kituo Cha KAZI, au anaacha kazi anaenda zake private kwa muda.
wanakula dili na afisa utumishi, wanaugawana nusu nusu huku yeye Yuko zake private sector anapiga Ela nyingine.

Kama Kuna mtumish mwngne wa halmashaur nmemsahau nikumbushe.

Ila kiuhaisia mwalimu nje ya mshahara sijui atapiga dili gani atoboe,

ukiachilia mbali suala la twisheni ambalo bado kipato chenyewe Ni kidg mno na jasho linalomtoka Ni jingi mno

Sijui atapiga dili gan jingine maana vitabu vyote vya serikali vimeandikwa "HAKIUZWI", boksi lenyewe la chaki Mtaani halizidi hata elfu 2.
Mkaguzi wa hesabu wa Ndani umemsahau Chief
 
Walimu kinachowabeba,
Wana akili ya maisha Sana,
Wanapata kidg,ila Wana uwezo wa kufanya maendeleo

Kuna afisa maliasili mmoja Huwa nakunywa nae pombe Hadi za laki 8, ila Hana hata kibanda Cha kujistiri na Yuko kwenye late 50s

Kama wewe sio snitch mshauri mwana[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom